
– Mchungaji huyo wa Kanisa la Mount Zion General Assembly Afrika Kusini alikuwa akionyesha wafuasi wake uwezo wa imani
Mwanamke mmoja Afrika Kusini aliaga dunia kutokana na jaribbio la mchungaji wake kumtumia kufanya muujiza

Mchungaji Lethebo Rabalungo alimuita mwanamke huyo kutoka kwa kusanyiko kanisani, na kumtaka kulala chini ambapo aliwaagiza wasaidizi kumwekelea spika kubwa mgongoni.
Wasaidizi hao walipanda juu ya spika hiyo huku mchungaji akiendelea kuelezea muujiza wake.
Kutokana na kitendo hicho, mwanamke huyo alijeruhiwa kifuani na kufariki baadaye kutokana na majeraha hayo kwa mujibu wa kituo kimoja cha radio nchini humo.
Kulingana na mchungaji huyo, mwanamke huyo alifarikia kwa sababu hakuwa na imani ya kutosha!
No comments:
Post a Comment