Mashabiki wamliza Joe Hart
M
echi ya marudiano ya klabu bingwa Ulaya kuwania kufuzu hatua ya
makundi kati ya Manchester City dhidi ya Steaua Bucharest ilikuwa na
hisia za aina yake kwa mlinda mlango wa Man City Joe Hart.
Claudio Bravo akiwa tayari ameshatua katika timu hiyo na akitarajiwa
kutangazwa muda mwishoni mwa juma hili, Joe Hart, 29, alipewa unahodha
katika mechi ya usiku wa jana ambayo inatajwa huenda ikawa mechi yake ya
mwisho akiwa mchezaji wa Manchester City.
A
likuwa akishangiliwa na mashabiki kwa kila alichokifanya kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mchezo huo.
Wakati wa kipindi cha pili katika mchezo huo, mashabiki wa Manchester
City walisimama kwa pamoja na kuimba “Stand up if you love Joe Hart“.
Alisajiliwa na Man City mwaka 2006 kutoka Shrewsbury Town, Joe ahart
alionekana akijitahidi kuzuia machozi lakini akashindwa na kujikuta
akiangua kilio.
No comments:
Post a Comment