Friday 30 June 2017

ZILIZOCHUKUA NAFASI KATIKA KURASA ZA MBELE MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 01 2017




Waziri Ummy Mwalimu amepokea taarifa kutoka kwa tume huru aliyoiunda kuchunguza Mapacha mawili

1
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakijadili kwa umakini na katibu mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wakiongea na waandishi wa habari(Hawapo kwenye picha) juu ya taarifa ya kuibiwa kwa mtoto mmoja wa Bi. Hasma Juma katika hospitali ya Temeke jijini Dar Es salaam.
2
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. BaKari Kambi akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari (Hawapo kwenye picha) wakatati wa uwasilishwaji wa taarifa ya tuhuma za kuibiwa kwa mtoto  mmoja wa Bi Hasma Juma uliofanyika mapema leo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.
3
Waandishi wa habari wa vituo tofauti wakifuatilia kwa umakini uwasilishwaji wa taarifa ya tuhuma za kuibiwa mtoto mmoja wa Bi Hasma Juma uliowasilishwa leo na mwenyekiti wa kamati Dkt. Charles Majige ambae pia ni Daktari bingwa wa Magonjwa yakina mama , uliofanyika leo mapema katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.
4
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akijibu maswali yaliyoulizwa na Waandishi wa Habari juu ya tuhuma za kuibiwa kwa mtoto mmoja wa Bi.Hasma Juma katika Hospitali ya Temeke jijini Dar es salaam.
5
Mwakilishi wa familia ya Bi Hasma Juma Jordan Jaddah akifuatilia kwa umakini Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati  akisisitiza juu ya taarifa iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa kamati ya Uchunguzi  Dkt. Charles Majige juu ya kuibiwa kwa mtoto mmoja wa Bi. Hasma Juma.

NA WAMJW DAR ES SALAAM
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amepokea taarifa kutoka kwa tume huru aliyoiunda ili kuchunguza malalamiko ya Bi. Asma Juma kuhusu kuibiwa mtoto mmoja kati ya mapacha wawili katika hospitali ya Rufaa ya Temeke Dar es salaam.
Akipokea taarifa  kutoka kwa Mwenyekiti wa tume hiyo Daktari bingwa wa magonjwa ya kinamama Dkt. Charles Majige  Waziri Ummy amesema kuwa Bi. Asma Juma(29) hakuwa na watoto mapacha kama ilivyodaiwa na mlalamikaji huyo kutokana na kipimo cha Utra sound kukosea katika uchukuaji picha ya mtoto akiwa tumboni.
“Nimepokea taarifa kutoka kwa tume huru niliyoiunda hivi karibuni na imethibitisha kuwa Bi. Asma Juma hakuwa na watoto mapacha ila uchukuaji mbaya wa picha ya mtoto aliyekuwa tumboni uliofanywa katika zahanati ya Huruma ukatoa matokeo hayo” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa wanafamilia ya Bi. Asma wanatakiwa kumfariji ndugu yao na sio kumkumbushia jambo hili mara kwa mara kwani litamharibu kisaikolojia na kushindwa kutekeleza wajiu wake kwa mtoto kama mama mzazi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati hiyo Dkt. Charles Majige Amesema kuwa Bi. Asma aliamini hivyo kwa sababu Hospitali ya temeke hawakumchukua vipimo vya picha bali walitumia taarifa ya vipimo vya awali .

Profesa Makame amekagua ujenzi wa jengo la Tatu la Abiria la uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA

unnamed
Meneja ujenzi wa kampuni ya BAM International, Bw. Rey Blumrick akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa wa hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa Jengo la 3 la Abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, wakati Waziri huyo alipokagua ujenzi wa jengo hilo leo mchana.
1
Meneja ujenzi wa kampuni ya BAM International, Bw. Rey Blumrick akifafanua Jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (Katikati), wakati Waziri huyo alipokagua ujenzi wa  Jengo la 3 la Abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, leo jijini Dar es Salaam.
2
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (wa nne kushoto), akiwa katika pichaa ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), na watendaji mbalimbali mara baaada ya kukagua ujenzi wa Jengo la 3 la Abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, leo mchana.
3
Muonekano wa sehemu ya Jengo la 3 la Abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Kukamilika kwake kutawezesha jengo hilo kuhudumia abiria wapatao milioni 8 na nusu kwa mwaka.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amekagua ujenzi wa jengo la Tatu la Abiria la uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), na kuelezea kuridhishwa kwake kwa hatua ya ujenzi iliyofikiwa.
Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi huo Waziri Profesa Mbarawa amemhakikishia mkandarasi BAM International anayejenga jengo hilo kuwa Serikali italipa madai yake kwa wakati kwa kadri atakavyoyawasilisha.
“Nia yetu ujenzi huu ukamilike ifikapo Septemba mwakani, hivyo tunamtaka mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi na wasimamizi kumsimamia kikamilifu ili vifaa vinavyofungwa katika jengo hilo viwe na ubora uliokusudiwa na vidumu kwa muda mrefu”, amesisitiza Profesa Mbarawa.
Prof. Mbarawa amesema kukamilika kwa jengo la tatu la abiria la uwanja wa ndege wa Julius Nyerere kutawezesha uwanja huo kuweza kuhudumia abiria wapatao milioni 8 na  nusu kwa mwaka na hivyo kukuza uchumi wa nchi kwa kuwezesha watalii na wageni wengi zaidi kufika nchini.

Jeshi la Laua Majambazi wanne Kibiti usiku wa kuamkia leo

Jeshil la Polisi limeua Watu wanne wanaozaniwa kuwa ni majambazi kwenye kijiji cha Pagae , Kibiti Mkoani Pwani
Taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari na DCP Lebaratus Sabas Mkuu wa Opereshini Maalumu ya Jeshi hilo Tanzania ambapo amesema kuwa majambazi hao wameuwa jana Majira ya Usiku
kwenye barabara inayotoka Pagae kuelekea Nyambunda.
taarifa hiyo ya DCP Sabas inasema  kuwa Askari Polisi wakiwa doria walikutana na kikundi cha watu kinachokadiriwa kuwa na watu sita wakitokea barabara kuu ya lami wakifuata barabara hiyo inayoelekea Nyambunda kilomita 100 kutoka barabara kuu.
"Watu hao walipogundua kuwa watu waliokuwa mbele yao ni Askari Polisi  walikimbia vichakani na ghafla wakaanza kuwashambulia askari kwa risasi.
Askari Polisi walijibu mapigo na kuanza kupambana na watu hao. "
Katika mapambano hayo askari Polisi walifanikiwa kuwajeruhi kwa risasi watu wanne katika kundi hilo la wahalifu  hao.
Aidha katika mapambano hayo zilipatikana silaha mbili aina ya Smg na magazine mbili pamoja na risasi 17 zilizokuwa zinatumiwa na wahalifu hao.
Watu hao wanne ambao wanasadikiwa kuwa miongoni mwa wahalifu wanaendesha vitendo vya mauaji katika wilaya za Mkoa wa Pwani.

Ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway Borge Brende

1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway Borge Brende aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
2 3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha  na Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway Borge Brende wanne kutoka (kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga wanne kutoka (kulia)pamoja na vingozi wengine wa Tanzania na Norway mara baada ya mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam.

Bungeni leo Ijumaa Juni 30 2017

PIX 1.1 Mhe.Ndugai
Spika  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai  akiongoza    kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 2 Mhe.Jafo
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais(TAMISEMI) Mhe,Selemani Jafo akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 3 Mhe.Wambura
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 4 Mhe.Mwigulu
Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha hamsini na nne cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 5 Mhe.Kamwelwe
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Isack Kamwelwe akijibu maswali mbalimbali ya wabunge   katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 6 Mabula
Naibu Waziri Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Angeline Mabula  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge    katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 7 Mhe.Ngonyani
Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Eng,Edwin Ngonyani  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge  katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 8 Mhe.Simbachawene
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe.George Simbachawene  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge  katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 9 Mhe.Cosato
Mbunge wa Mafinga Mjini Mhe.Cosato Chumi akiuliza swali katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 10 Mhe.Bashungwa
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dk.Ashatu Kijaji akiteta jambo na Mbunge wa Karagwe Mhe.Innocent Bashungwa katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 11 Mhe.Shally
Mbunge wa Viti Maalum Mhe.Shally Raymond akiuliza swali katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 12 Mhe.Mwanjelwa
Mbunge wa Mbeya  Mhe.Dk Mary Mwanjelwa akiuliza swali katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 13 Mhe.Mwantakaje
Mbunge wa Bububu Mhe.Mwantakaje Juma akiuliza swali katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.
PIX 14 Washindi wa medali za dhahabu
Washindi wa Medali za Dhahabu katika Mashindano ya Kimataifa ya Mazingira na Sayansi yaliyofanyika nchini Marekani Kutoka kushoto Ndg.Rashid Kikwete,Kassi Juma Nkamia na Abdallah Rubeya wakiwa bungeni kujifunza shughuli balimbali za  Bunge.
PIX 15 Mhe.Maghembe na Mbatia
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Prof Jumanne Maghembe akimsikiliza Mbunge wa Vunjo Mhe.Eng.James Mbatia  katika kikao cha hamsini na saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 30, 2017.

Picha Zote na Daudi Manongi- Dodoma MAELEZO, DODOMA

Kinyerezi II Kuzalisha Megawati 30 za umeme

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Medard Kalemani ameagiza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuhakikisha mradi wa umeme wa Kinyerezi II unazalisha megawati 30 za umeme nchini ifikapo Desemba mwaka huu.

Kalemani amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi huo leo asubuhi (Juni 30) ili kujua hali ya utendaji.
Amesema taarifa aliyopewa tangu alipowasili ni kuwa mradi huo utazalisha megawati 240 utakapokamilika mwakani ila 30 zikamilike Desemba mwaka huu.

"Mradi wa Kinyerezi II tunategemea utupatie megawati 240, lakini lazima tuanze kupata hizo mapema, kwa taarifa niliyosikia tutaanza na megawati 30 sasa niseme megawati hizo tupate ifikikapo Desemba," amesema Kalemani.

Amesisitiza kuwa zitakazobakia apewe ratiba za utekelezaji wake ili hadi kufikia Septemba 2017 megawati zote ziwe tayari.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanesco, Tito Mwinuka ameomba ushirikiano baina ya Serikali na Shirika hilo ili kufika malengo ya agizo la Naibu Waziri.

"Tushirikiane pamoja Tanesco na Serikali kuhakikisha fedha zinapatikana kwa wakati ili kwamba mradi ukamilike kwa wakati," amesema Mwinuka.

Kalemani ameongeza kuwa hakutakuwa na uongezaji wa muda katika miradi yote miwili ya Kinyerezi I na II hivyo kuwataka wahusika kufanya kazi kwa nguvu na weledi ili kumaliza kazi.
Amesema mradi wa Kinyerezi I umefikia asilimia 35 hali ambayo hairidhishi huku ukitegemewa kutoa megawati 185 kufikia Agosti 2017.

Ufaransa: Polisi yamkamata mtu aliyejaribu kuvamia msikiti

Polisi nchini Ufaransa imemkamata mtu mmoja katika jiji la Paris baada ya kujaribu kuendesha gari kwa kasi mbele ya umati wa watu nje ya msikiti mmoja.
Shambulizi hilo lilitokea katika kitongoji cha Créteil na hakuna aliyejeruhiwa.
Mtu huyo hakuweza kutimiza azama yake baada ya kushindwa kuvipita vizuizi vilivyokuwepo mbele ya msikiti huo.
Vyombo vya habari vya Ufaransa vinasema mshambuliaji huyo ana asili ya Armenia.
Lengo la shambulizi hilo bado halijajulikana.

Ujerumani yatinga fainali kombe la mabara, yaipiga Mexico 4 - 1

Leon Goretzka (kulia) akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Ujerumani mabao mawili dakika za sita na nane katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Mexico leo kwenye mchezo wa Nusu Fainali Kombe la Mabara leo Uwanja wa Olimpiki Fisht mjini Sochi. Mabao mengine ya mabingwa hao wa dunia yamefungwa na Timo Werner dakika ya 59 na Amin Younes dakika ya 90 na ushei, wakati la Mexico limefungwa na Marco Fabian dakika ya 89 na sasa Ujerumani itakutana na Chile katika fainali Julai 2 Uwanja wa Krestovsky mjini Saint Petersburg, Urusi

Mastaa waliohudhuria kwenye harusi ya Messi, Argentina

 WACHEZAJI wenzake wa sasa na wa zamani Lionel Messi katika timu ya Barcelona wamewasili Argentina kwa ajili ya harusi ya mwenzao huyo anayemuoa Antonella Roccuzzo kesho.
Sergio Busquets, Jordi Alba, Carles Puyol, Cesc Fabregas, Xavi na Samuel Eto'o wote wameonekan katika picha iliyopostiwa kwenye ukurasa wa Instagram na mke wa Puyol, Vanessa Lorenzo.
Messi amewakaribisha wenzake wote katika kikosi cha Barcelona kwenye sherehe hiyo mjini Rosario, ambako wageni wamekodiwa hoteli ya nyota tano.
Mke wa Sergio Aguero, Karina ataimba wimbo wa kwanza katika sherehe hiyo.
Messi pia ameagiza kipikwe chakula cha kiasili cha 'locro' na 'empanada' ambacho ni nyama rosti kabisa ya Kiargentina pamoja na 'maanjumati' mengine.
Messi na mpenzi wake wa tangu utotoni hatimaye wataoana baada ya kukutana tangu wana umri wa miaka mitano mjini Rosario, Argentina walipokulia na wakaendelea kuwa pamoja hata mwanasoka huyo baada ya kuhamia Hispania alipofikisha umri wa miaka 13 kwenda kujiendeleza kisokaa. Na sasa wamerejea nyumbani kwao kabisa kwa sherehe hiyo kubwa kesho.
Messi na Roccuzzo, ambao wana watoto wawili, Thiago na Mateo, watafunga ndoa yao katikati ya mji wa Rosario, Santa Fe.


Thursday 29 June 2017

KURASA ZA MBELE MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 30 2017




Mawakili wapya wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma ya uwakili

unnamed
Mgeni Rasmi Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (katikati) akifuatilia jambo wakati wa sherehe za 56 za kuwakubali na kuwasajiri, Mawakili wapya 248 mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
1
Baadhi ya ndugu wa Mawakili wapya wakisubiri  zoezi la kuapishwa kwa ndugu zao mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
2
Baadhi ya Mawakili wapya wakisubiri zoezi la kuapishwa mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
3
Mgeni Rasmi Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma (wanne toka kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Majaji na Mawakili wapya mara baada ya kuwaapisha mapema hii leo katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Picha na Eliphace Marwa -Maelezo

Na. Eliphace Marwa – Maelezo
29/06/2017       
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma amewataka Mawakili wapya kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma ya uwakili na kutumia taaluma zao kwa kutoa msaada wa kisheria kwa jamii. 
Aliyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Sherehe za 56 ya kuwapokea na kuwaapisha Mawakili wapya 248 iliyofanyika katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Aidha Kaimu Jaji Mkuu amewahimiza Mawakili wapya kujiendeleza kitaaluma kwa sababu kuwa wakili sio mwisho wa taaluma kwani wanahitajika kusoma sheria za nchi mbalimbali Duniani ili kuweza kuingia mikataba ya kimataifa. 
Alisema mawakili wapya wanatakiwa washiriki katika kutoa haki, wawe waaminifu kwa mahakama na wateja kwani wakienda kinyume haki itapotea.
“Mawakili wote wanatakiwa kuwa waaminifu kwa wateja wanaowahudumia na kushirikiana na mahakama katika kutoa haki na wasiwe mawakala wa rushwa bali wawe mawakala wa kutenda haki,” alisema Kaimu Jaji Mkuu Prof. Ibrahim.
Aidha Kaimu Jaji Mkuu aliwataka mawakili hao kufika maeneo ya nje ya mji ili wasaidie upatikanaji wa haki kwani kumekuwa na changamoto kubwa ya mawakili katika maeneo ya nje ya miji.
Naye Rais wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika (TLS) Tundu Lissu amewataka Mawakili hao kutumia taaluma hiyo katika kuisaidia jamii kujua haki zao na utawala wa sheria japo kuna changamoto mbalimbali zinazoikabili tasnia ya sheria nchini.