Thursday 25 August 2016

Bundesliga: Bayern vs W.Bremen nani kuianza vyema ligi

 Baada ya kuisubiri kwa muda wa miezi 3, hatimaye Bundesliga inarejea tena. Msimu unaanza kwa mechi kubwa kati ya mabingwa watetezi FC Bayern vs Werder Bremen. Wageni wa mchezo huo katika dimba la Allianz Arena wanaweza sasa wasiwe na nguvu kama ambavyo walikuwa kipindi wanashinda ubingwa mnamo mwaka 2004, lakini kikosi cha Viktor Skripnik bado wanategemewa kutoa ushindani mkubwa kwa Carlo Ancelotti ambaye atakuwa anaiongoza Bayern kwa mara ya kwanza katika Bundesliga.
Kocha huyo wa kiitaliano tayari ameshaanza na mwanzo mzuri kwa kushinda Germany SuperCup na mchezo wa kwanza wa DFP Cup, lakini malengo makubwa ya klabu yapo katika Bundesliga – “Malengo yetu makuu ni kushinda ligi,” Ancelotti alisema wakati anawasili na kuanza kwa ushindi wa pointi 3 kesho Ijumaa itakuwa ni msingi mzuri kuelekea kutimiza malengo.

 Bremen watakuwa wanamtegemea kwa mara nyingine tena mchezaji wa zamani wa Bayern na mmoja wa wafungaji bora wa ligi Claudio Pizarro wakiwa wanajiandaa kuleta msha
ngao kwa wapenzi wa Bayern.

Takwimu za Mchezo

 *Ancelotti anakuwa kocha wa kitaliano kufundisha soka ndani ya Bundesliga, baada ya  Giovanni Trapattoni, Nevio Scala na Roberto Di Matteo.

*Pizarro ndio mfungaji bora wa muda wote wa Bundesliga kutoka nje ya Ujerumani – akiwa na magoli 190, kati ya hao 103 ameifungia Bremen, na 87 ameifungia Bayern.

*Robert Lewandowski alimaliza akiwa mfungaji bora msimu uliopita akiwa na magoli 30.

*Mpaka kufikia leo hii timu hizi zimekutana mara 34 mpaka sasa, katika mechi hizo kila timu imefunga wastani waagoli 3.5 kwa kila mechi. FC Bayern wanaongoza kwa kuwafunga Werder mara 21, sare zipo 6 na Werder nao wameshinda mara 7. Ijumaa hii huu utakuwa mchezo wa kwanza na utaonyeshwa live on Startimes kupitia channel #SportFocus

Majeruhi Upande wa Bayern: Badstuber, Costa, Coman (ankle), Boateng (misuli)

Majeruhi Upande wa Bremen: Garcia, Kruse, Bargfrede

No comments:

Post a Comment