Sunday 31 July 2016

Jinsi ya kulima Vanila

 

Vanilla (Vanilla fragrans) asili yake ni Amerika ya kati huko Mexico, Guatemala na Costa Rica ambako ilianza kutumika tangu karne ya 15.
 Zao la vanilla lilifika barani Ulaya karne ya 16, kisha likapelekwa visiwa vya Reunion, hatimaye kusambazwa Mauritius, Madagasca, Shelisheli, Tahiti na Comoro kati ya karne ya 18 na 19. Zao hili kwa sasa linazalishwa kwa wingi sehemu za Madagasca, Comoro na Reunion. Hapa Tanzania zao hili liliingizwa mkoani Kagera mwaka 1962 kutokea nchini Uganda.
Hata sasa Mkoa wa Kagera ndio unaozalisha zao hili katika wilaya za Bukoba na Muleba, na pia huko Zanzibar. Zao hili linaleta fedha za kigeni kwa nchi na kuleta ajira kwa wananchi. Vanilla ni zao ambalo hutumika kuongeza ladha katika vyakula na vinywaji vya aina mbalimbali. Matumizi makubwa ya zao hili ni kuongeza harufu nzuri na ladha ya vyakula na vinywaji mbalimbali.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOST 1 2016


 

Samatta uwanjani leo ligi kuu Ubelgiji

Mbwana Samatta leo anatarajiwa kuonekana tena katika nyasi za Ulaya pale timu yake ya Genk itakapovaana na KV Oostende katika muendelezo wa mechi za ufunguzi katika Ligi Kuu ya Ubelgiji maarufu kama Jupiler Pro League.
Mchezo ambao utachezwa kunako dimba la Cristal Arena, nyumbani kwa Genk utaanza saa 1 kamili za usiku kwa majira ya Tanzania na Afrika Afrika Mashariki kwa ujumla.

Ikumbukwe tu, huu ndio msimu ambao Samatta anaanza kuanzia mwanzo mara baada ya msimu uliopita kuukuta mwishoni kufuatia ksajiliwa katika dirisha dogo akitokea TP Mazembe ya DRC.

Ruvu Shooting yazitishia nyau Simba na Yanga ligi kuu

Klabu ya mpira wa miguu ya Ruvu Shooting ya mkoani Pwani, inayoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara(VPL) imetamba kufanya makubwa msimu ujao wa Ligi hiyo na kuwataka mabingwa wa ligi hiyo, Yanga kutarajia upinzani mkali kutoka kwao katika kupigania taji hilo.
Akizungumza kutoka Mlandizi yalipo maskani ya timu hiyo, Ofisa Uhusiano wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, alisema kuwa malengo yao msimu ujao ni kuwa miongoni mwa timu tatu za juu na ikiwezekana kutwaa ubingwa kama walivyofanya Leicester City ya England ambayo msimu uliopita ilipanda daraja na kubeba taji.

Alisema kuwa kikosi chao kipo katika maandalizi kabambe na kwamba Jumatatu wanatarajia kutambulisha wachezaji wao, wakati watakapovaana na Mbeya City katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi.

Wanafunzi wapewa Adhabu ya kung'oa Kisiki cha Mti uliopandwa na mkolon

Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu KATOKE ( TTC ) kilichopo Kagera Wilaya ya Muleba walalamika juu ya adhabu wanazopewa na uongozi wa hapo Chuoni pindi wanapofanya makosa..
Mwanafunzi akieleza hali ya Shuleni hapo..
Mnamo tarehe 27/07/2016 saa 3:28Pm kengele iligongwa kwa ajili ya kwenda paredi ambapo huwa ni siku ya (EK) Yaan elimu ya kujitegemea ambapo huwa tunatakiwa kwenda paredi kwa ajili ya kugawiwa majukumu ya kazi. Kengele inapaswa igongwe saa 3:30pm au saa 4:00pm inategemeana na ratiba ya siku ila inayofahamika ni saa 4:00pm kwa siku ya jumatano. 

Kamati ya utendaji Chadema Moshi yavunjwa

Moshi. Baraza la uongozi la Chadema mkoa Kilimanjaro limeivunja kamati ya utendaji ya chama hicho wilaya ya Moshi mjini, inayoongozwa na Mbunge wa moshi Mjini, Jaffar Michael.
Uamuzi wa kuivunja kamati hiyo umo katika barua ya mwenyekiti wa Chadema mkoa Kilimanjaro, Philemon Ndesamburo kuwa umetokana na minyukano isiyoisha ndani ya kamati hiyo.

Mwili wa Senga wasafirishwa leo kwenda Mwanza kwa mazishi

Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga (58) umesafirishwa leo kwenda nyumbani kwao, Shushi-Nyambichi, Kwimba mkoani Mwanza kwa ajili ya maziko hapo kesho Akizungumza wakati wa kuuga mwili wa marehemu Dar es Salaam mapema leo, msemaji wa familia, Charles Kapama amesema maziko yatafanyika kesho saa nane mchana baada ya mwili kuwasili kijijini.

IGP Mangu akagua miundombinu ya kipolisi mkoani Shinyanga

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi katika wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga jana, kulia ni kamanda wa Polisi mkoani humo, Muliro J. Muliro.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akifuatilia jambo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Mhe. Fadhil Nkhulu (aliyesimama) anayefuata ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab R. Telack, pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi.

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akifafanua jambo wakati alipomtembelea ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, Mhe. Simon S. Berege (katikati), akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi, kulia ni kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Muliro J. Muliro.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu, akiangalia kwa umakini ramani ya mipango miji inayoonesha mahala itakapokuwepo Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga, katikati (aliyevaa tai) ni Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Msalala Mhe. Simon S. Berege, wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miundombinu ya kipolisi katika mkoa wa Shinyanga.

Saturday 30 July 2016

Ujumbe alioandika Mbowe kwenye ukurasa wake wa Twitter



Jana usiku nilipata wito nikitakiwa kwenda Polisi Kanda Maalum Ya Dar es salaam na Zonal Crime Officer Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Wambura, akihitaji nifike leo Jumamosi 30/07/2016, lakini leo nipo Marangu Kilimanjaro kuhudhuria maziko ya Baba yake mzazi Devotha Minja, Mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA.

Mbeya wakiuka agizo la Rais Magufuli la kufanya usafi.

Baadhi ya wananchi wamewataka viongozi wa wilaya ya Mbeya kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaOkiuka agizo la Rais, Dk. John Pombe Magufuli la kujitokeza kufanya usafi siku ya jumamosi ya kila mwezi.
Utekelezaji wa agizo la Rais Dk. John Pombe Magufuli la kufanya usafi wa mazingira kila siku ya jumamosi ya mwisho wa mwezi limeanza kukiukwa na baadhi ya wananchi kutokana na idadi ndogo ya watu ambao imejitokeza mwezi huu kufanya usafi mitaani, hali ambayo imesababisha baadhi ya wananchi kutaka hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya yanaokiuka agizo hilo.

Kiwanda cha Dangote chapigwa faini ya milion 15

 Naibu Waziri Ofisi ya makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina ( katikati) Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Bw. Khatib Kizinga (kushoto) wakipata maelezo toka kwa Bw. Sultani Pwaga wa kiwanda cha Gas cha Madiba Mjini Mtwara wakati wa ziara ya Naibu Waziri Mpina kiwandani hapo.

Serikali imekitoza faini ya shilingi milioni 15, kiwanda cha kutengeneza simenti cha Dagonte Industry Limited kilichopo mjini Mtwara, kwa kosa la kukiuka sheria ya mazingira
Serikali kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC limekitoza faini ya shilingi milioni 15, kiwanda cha kutengeneza simenti cha Dagonte Industry Limited kilichopo mjini Mtwara, kwa kosa la kukiuka sheria ya mazingira ya mwaka 2004 na kanuni zake.
Katika siku ya pili ya ziara ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina mkoani Mtwara imebainika kuwa kiwanda hicho cha Dangote chenye muda wa miezi mitatu tangu kianze kazi ya kutengenza simenti, kimefanya uchafuzi wa mazingira kwa kukosa sehemu maalum ya kuhifadhi taka katika kiwanda hicho, kutokuwa na utaratibu mzuri wa kuhifadhi taka zitokanazo na makaa ya mawe kiwandani hapo.

Mashabiki wa Simba waanza kurudisha imani kwa timu yao

Imani ya mapenzi mashabiki wa Simba imeanza kurejea hasa kutokana na kikosi chao kipya kuonyesha soka safi.
Katika mechi mbili za kirafiki ambazo Simba imecheza mjini Morogoro, imeweza kuonyesha soka safi na kufanya mashabiki kufurahi.

Azam FC kumaliza kambi kwa kupimana na Jang'ombe

Timu ya Azam FC itashuka kucheza mechi yake ya kirafiki na timu ya Jang’ombe uwanja wa Amaan ikiwa ni maandalizi ya mchezo wa ngao ya jamii dhidi ya Yanga utakaopigwa Agosti 17 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Afisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd Maganga amesema kocha wa timu hiyo Zeben Hernandez atautumia mchezo huo kwa ajili ya kuendelea kuangalia viwango vya wachezaji wa timu hiyo ili kupata kikosi chake cha kwanza.

Jaffar amesema, licha ya kocha huyo kutafuta kikosi cha kwanza katika mchezo huo lakini atautumia mchezo huu pia kutazama uwezo wa wachezaji wa kigeni ambao wanafanya majaribio katika timu hiyo na baada ya hapo wataweka utayari kwa kwa mechi ya Ngao ya Jamii.

Mchezo huo utakuwa wa mwisho kwa Azam FC visiwani humo ambapo kesho inatarajiwa kurejea jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuendelea na kambi ya maandalizi ya ngao ya jamii na ligi kuu ya soka Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 20 mwaka huu.

Jaji kiongozi wa mahakama kuu Mheshimiwa Ferdinand Wambali ametembelea mahakama ya mwanzo kigamboni

1Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Mheshimiwa Ferdinand Wambali akimsikiliza Mhandisi wa Mahakama ya Tanzania, Khamadu Kitunzi akimwonyesha Ramani ya jengo la Mahakama ya Mwanzo Kigamboni linaloendelea kujengwa jana jijini Dar es Salaam. Jengo hilo linajengwa kwa kutumia teknolojia ya Moladi.
2Jengo la Mahakama ya Mwanzo Kigamboni linalojengwa kwa kutumia Teknolojia ya Mola

Wizara ya Elimu kuhamia Dodoma Agosti

 

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesema imejipanga kuhakikisha inahamia Dodoma kabla au ifikapo Agosti 15 mwaka huu.
Kumekuwa na hekaheka kwa taasisi na wizara mbalimbali za umma kuhamia Dodoma ili kuunga mkono tamko la Rais John Magufuli ambaye Jumamosi ya wiki iliyopita aliuahidi  Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Serikali yake itatekeleza ndoto ya siku nyingi ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ya kuhamia katika mji mkuu huo.
Jana Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekuwa ya tatu kutangaza kuhamia Dodoma baada ya ile ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo na Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.

Mwili wa Senga kuagwa Sinza kesho

 
Mwili wa aliyekuwa Mpiga picha Mkuu wa gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga, unatarajiwa kuagwa kesho nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam, baada ya kuwasili leo ukitokea New Delhi nchini India.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mhariri Mtendaji wa gazeti hilo, Neville Meena, mwili huo utawasili saa 7:00 mchana katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) kwa ndege ya shirika la Ethiopia  (Ethiopia Airlines) na kupelekwa moja kwa moja Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kuuhifadhi.

Kaka wa Rais Magufuli amefariki

 
Kaka wa Rais Dk. John Magufuli, Anthon Lubambagwe, amefariki dunia kutokana na maradhi ya kifua.
Taarifa ya kufariki kwa Lubambagwe ilitolewa jana na msemaji wa familia, Nebart Mlambi, aliyeeleza kuwa marehemu huyo alifariki saa 8:30 mchana katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure, jijini Mwanza alipokuwa amelazwa akitibiwa.
Mlambi alisema marehemu Antony ni mtoto wa Helman Gwape Lubambagwe ambaye ni baba mkubwa na Rais Magufuli.
“Mzee alianza kuugua Aprili mwaka huu na kutibiwa katika Kituo cha Afya cha Igoma, akapata nafuu lakini alizidiwa tena Julai 27, mwaka huu tukampeleka Hospitali ya Sekou Toure.

Wakazi zaidi ya 100 wamendolewa kwa nguvu katika nyumba zinazomilikiwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA

Dodoma. Wakazi zaidi ya 100 wamendolewa kwa nguvu katika  nyumba zinazomilikiwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) baada ya kukaidi agizo la kuhama kwa hiari ili kupisha ukarabati.
Wamiliki hao waliondolewa na kampuni ya udalali ya Mvina, zoezi liloanza  asubuhi leo chini ya usimamizi wa polisi walikuwa na mabomu ya machozi na bunduki.
Awali wapangaji hao walipewa notisi ya kuhama kwa hiari ya siku 90 lakini baadaye wakaongezewa wiki moja iliyoisha leo.

Rais wa Uturuki awasamehe waliomtukana

Rais Tayyip Erdogan

Rais Erdogon wa Uturuki ametangaza msamaha kwa watu wote waliokabiliwa na mashtaka ya kutukana, katika kile alichotaja kama ishara ya heri njema.
Zaidi ya watu 2,000 walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya kumtukana Rais kwa muda wa miaka miwili iliyopita.
Akizungumza katika hafla katika mji mkuu wa Ankara kuwakumbuka zaidi ya watu 200 wanaodaiwa walifariki katika jaribio la mapinduzi, rais Erdogon aliyakebehi mataifa ya Marekani na Ulaya.

Ndondo Cup kuwaka moto leo

 
Dar es Salaam. Safari ya mashindano ya Ndondo Cup iliyoanza  miezi mitatu iliyopita, inafikia tamati leo kwa mchezo wa fainali kati ya Kauzu FC dhidi ya Temeke Market.
Mchezo wa leo unaotarajia kuwa na ushindani wa aina yake utapigwa kwenye Uwanja wa Bandari uliopo Temeke na unatarajiwa kuvuta mashabiki wengi wa soka jijini Dar es Salaam.

Taarifa ya zitto kabwe kwa viongozi wa vyama vya siasa

 
Maelekezo ya Kiongozi wa Chama ( KC ) kwa wanachama wote wa ACT Wazalendo ( KC/01/2016 ).

Tangu kukamilika kwa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 Utawala mpya umekuwa ukifanya kila juhudi kuminya uwezo wa Vyama vya Siasa kufanya Kazi zake kwa kisingizio kuwa huu ni wakati wa kufanya Kazi na kwamba Siasa zisubiri mwaka 2020. 
Chama chetu kilipinga kwa nguvu zote uzuiaji huu wa shughuli za kisiasa kwani ni kinyume cha Katiba ya Nchi na Sheria ya Vyama vya Siasa, sheria namba 5 ya mwaka 1992 kama ilivyofanyiwa marekebisho Mara kwa Mara.
Mnamo tarehe 5 Juni 2016 Chama chetu kilifanya Mkutano wa Hadhara Mbagala jijini Dar Es Salaam na kutangaza Operesheni Linda Demokrasia. Lengo la Operesheni hiyo ( Tamko la Mbagala 2016 ) ni kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kuwa Nchi ya kidemokrasia na kuepuka mwelekeo wa Utawala wa Imla ambao ni utawala wa kidikteta. Chama chetu asili ya uundwaji wake ni kupinga tabia za kidikteta tulizokumbana nazo ndani ya Vyama tulivyokuwamo. 

Faida za kula chungwa katika mwili wa binadamu


Ni msimu mwingine wa machungwa, yamejaa tele kila kona. Shilingi 100 tu unapata chungwa. Lakini siyo ajabu kama kuna watu msimu unaisha hawajala hata chungwa moja, wala suala la matunda halipo kabisa katika orodha ya milo yao!
Inawezekana pia hata kwa wale wanaokula, japo kidogo, hula kama kiburudisho tu bila kujua faida zake mwilini. Katika makala ya leo nitakujuza faida 13 unazoweza kuzipata unapokula chungwa, ambalo limesheheni virutubisho kibao.
Kumbuka kuwa hata chungwa moja tu ukila lina kidhi yale mahitaji muhimu ya mwili ya kila siku (daily requirement), iwe chungwa lenyewe au juisi yake halisi.


Amani Alfred Naburi ameshinda shindano la insha lijulikanayo kama “Lugha nyingi, Dunia Moja

 

Mwanafunzi wa  Kitanzania, Amani Alfred Naburi
Mwanafunzi wa Kitanzania, Amani Alfred Naburi, ni mmoja wa kati ya wanafunzi 60 kutoka Vyuo Vikuu mbalimbali duniani ambao wameshinda shindano la Insha lijulikanayo kama “Lugha nyingi, Dunia Moja” ( Many languages, One World) lililoandaliwa kwa ushirikiano baina ya United Nations Academic Impact ( UNAI) na ELS Educational Services, Inc.

Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu yatangaza kufungua ofisi leo

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB), imetangaza kuwa leo na kesho ofisi za bodi hiyo zitakuwa wazi ili kutoa muda kwa kuwahudumia wananchi mbalimbali.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Jerry Sabi, bodi imeamua kufungua ofisi zao ili kutoa nafasi kwa wanaohitaji huduma na pia kwa wadaiwa kwenda kutoa malalamiko yao.

Mghana wa Azam ajipeleka Yanga

MIDO mpya ya Azam, Enock Atta Agyei aliyekuwa akiichezea Medeama ya Ghana, amesema nafasi ya kwanza kwake kwa timu za Tanzania ilikuwa Yanga kama kocha Hans Pluijm angetaka iwe hivyo lakini matajiri wa Chamazi wakazama kwenye waleti fasta wakafanya yao.
Atta amesajiliwa juzi na Azam kwa mkataba wa miaka miwili na muda wowote
kuanzia jana alitarajiwa kutua nchini ili kujiunga na Azam akitokea Medeama.
mara ya kumalizika kwa mchezo wa Jumanne kati ya Yanga dhidi ya Medeama, Atta alisema anajuana vizuri na kocha wa Yanga,Pluijm na alikuwa anataka kuzungumza naye ili ampe nafasi.
Kiungo huyo mshambuliaji alisema Pluijm ni moja ya makocha wenye heshima kubwa katika soka Ghana na kila mmoja katika kikosi cha Medeama alitamani pate nafasi acheze katika kikosi cha Mholanzi huyo.

Friday 29 July 2016

Ufugaji wa kuku wa kienyezi

 
Wafugaji wengi wa Tanzania wanafuga kuku wa kienyeji. Ndege hawa kwa kawaida wanafugwa sehemu za vijijini ambapo wanaachiwa huru kuzurura.
Kuna uwezekano mkubwa sana wa kizazi kujirudia kwa kuwa jogoo anaweza kumpanda mtetea ambaye alitokana naye, au kumpanda mtetea ambaye wamezaliwa pamoja. Kuzaliana kwa namna hiyo kunasababisha matatizo makubwa, ikiwa ni pamoja na kudumaa, kupunguza uzalishaji wa mayai, kuwa na vifaranga dhaifu ambavyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa, na mengineyo mengi yasiyokuwa ya kawaida. Ufugaji huru ambao una udhibiti ni muhimu sana ili kuepuka kizazi kujirudia. Kuku wanaweza kuwekwa kwenye makundi na kuachiwa kwa makundi ili kuzuia uwezekano wa kuzaliana kwa kizazi kimoja.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 30 2016

 

Wizara ya Nishati na Madini imetoa semina ya siku moja kwa Wakuu wa Mikoa ambayo Bomba la Mafuta litapita kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga

MHO1Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akizungumza wakati akufungua semina  siku moja kwa Makatibu Wakuu wa Wizara zinahusika moja kwa moja na ujenzi wa Bomba la Mafuta na Wakuu wa Mikoa ambayo  Bomba hilo linapita kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania.
MHO2Sehemu ya Makatibu Wakuu wa Wizara zinahusika moja kwa moja na ujenzi wa Bomba la Mafuta na Wakuu wa Mikoa ambayo  Bomba hilo linapita kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania wakati wa semina ya siku moja juu ya ujenzi wa bomba hilo.
MHO3Sehemu ya Makatibu Wakuu wa Wizara zinahusika moja kwa moja na ujenzi wa Bomba la Mafuta na Wakuu wa Mikoa ambayo  Bomba hilo linapita kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania wakati wa semina ya siku moja juu ya ujenzi wa bomba hilo.
MHO4Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa( kulia) katika mahojiano ya mubashara( live) na Kituo cha Televisheni cha Taifa (TBC 1), na Mtangazaji wa kituo hicho Anna Kwambaza( kushoto)

Na Zuena Msuya, Dar Es Salaam
Wizara ya Nishati na Madini imetoa semina ya siku moja kwa  Wakuu wa Mikoa ambayo Bomba la Mafuta litapita kutoka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania na Makatibu Wakuu wa Wizara zinahusika moja kwa moja na Ujenzi wa Bomba  hilo.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo jijini Dar es salaam, Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter amesema, semina hiyo itawawezesha Viongozi hao kuwa na uwelewa mpana juu ya ujenzi wa bomba hilo pia kushirikiana kwa karibu na kufanikisha kukamilisha mradi wa bomba hilo kwa wakati uliopangwa.

Wauawa kwa kushindwa kulipa deni la biskuti India

India Dalit

Mtu mmoja na mkewe kutoka jamii ya Daliti inayobaguliwa tangu jadi nchini India wameuawa, mmoja akiwa amekatwa kichwa na mwengine kunyongwa kwa kushindwa kulipa deni la Rupee kumi na tano ambalo ni karibu senti ishirini na mbili tu.
Polisi kaskazini mwa taifa hilo wamethibitisha kisa hicho ambapo yasemekana mfanyi biashara anayetokea jamii ya hadhi ya juu,aliwaua wanandoa hao kwa kushindwa kulipa deni la biskuti walizokuwa wamewachukulia watoto wao.

Taarifa muhimu kwa wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu walioko Dar es salaam


Treni ya pugu kuanza kazi jumatatu ya tarehe 01/08/2016.

TRENa: Frank Shija, MAELEZO
Kampuni ya Reli ya Tanzania (TRL) imefanya mabadiliko ya muda wa Treni ya Abiria kulekea mikoa ya Kigoma na Mwanza ambapo kuanzia tarehe 02 Agosti 2016 Treni itaanza kuondoka saa tisa(9) mchana badala ya saa 11 jioni muda wa sasa.
Mabadiliko hayo yametangazwa na Meneja Uhusiano wa TRL Midladjy Maez wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake leo Jijini Dar es Salaam.
Maez amesema kuwa mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa nafasi kwa treni ya pili ya huduma za Jiji kutoka kituo Kikuu cha Reli cha Dar es Salaam kwenda Pugu ambayo itaanza kutoa huduma mapema siku ya Jumatatu ya tarehe 01/08/2016.
Aliongeza kuwa mabadiliko hayo yanahusu treni za abiria za huduma za kawaida zinazoondoka siku za Jumanne na Ijuma na kubainisha kuwa kwa upande wa huduma za treni ya Deluxe zitaendelea na muda wake wa kawaida.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amefanya ziara magwepande

rw1Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisalimiana na Afisa Uhusiano wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Bi. Edna John wakati alipotembelea ujenzi wa mradi wa nyumba za wafanyakazi eneo la Bunju B jijini Dar es salaam.
rw2Mtendaji Mkuu wa wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch.Elius Mwakalinga  akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Kulia) kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mradi wa nyumba za wafanyakazi eneo la Bunju B jijini Dar es salaam.
rw3Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch.Elius Mwakalinga  wakati alipokagua  ujenzi wa mradi wa nyumba za wafanyakazi eneo la Bunju B jijini Dar es salaam.
rw4Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch.Elius Mwakalinga  wakati alipokagua  ujenzi wa mradi wa nyumba za wafanyakazi eneo la Bunju B jijini Dar es salaam.
rw5Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akikagua baadhi ya miundombinu iliyopo katika mradi wa ujenzi wa nyumba za wafanyakazi zilizopo Bunju B jijini Dar es salaam.

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wamechangia kiasi cha Tsh. Milioni 100

indexWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi  Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akimkabidhi  hundi Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa hafla ya makabidhiano  madawati  ikiwa ni fedha zilizochangwa na watumishi wa wizara hiyo ikiwa sehemu ya kutekeleza agizo la Rais Mhe. John Magufuli  mapema hii leo katika shule ya Msingi Chamanzi iliyopo wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam . Picha na Beatrice Lyimo-MAELEZO

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Dar es salaam
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wamechangia kiasi cha Tsh. Milioni 100 ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha umma kuhusu zoezi la upatikanaji wa madawati katika shule za msingi na Sekondari nchini.
Akikabidhi mchango huo kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kwa niaba ya watumishi wa wizara hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi  Augustine Mahiga amesema kuwa watumishi hao wametoa fedha hizo kwa shule ya msingi Chamazi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais la upatikanaji wa madawati katika shule za msingi na sekondari nchini. 

Siri ya jezi namba 10 Barcelona

Kila timu kubwa duniani ina utamaduni wake wa kuthamini na kuzipa uzito wa juu namba za jezi, ambazo zimetumiwa na mastaa wake wa zamani.
Si kila mchezaji hupewa namba hizo pindi anaposajiliwa na mastaa wengi wamekuwa wakitoa masharti ya namba za jezi wanazotaka kuvaa.
Pale Manchester United kwa sasa kuna mgogoro wa chini kwa chini baada ya kinda wa Ufaransa, Anthony kuporwa jezi namba tisa na kukabidhiwa gwiji, Zlatan Ibrahimovic.
Katika kikosi cha Man United, jezi namba 7, 8,9, 10 na 11 zimekuwa moto kutokana na kutumiwa na magwiji na mastaa wakubwa duniani. Awali, namba 7 ilikuwa ikitumiwa na Eric Cantona kisha David Beckham na baadaye Cristiano Ronaldo, ambapo wote wameitendea haki vilivyo.

Usajili wa Pogba kwenda Manchester United kukamilika ndani ya masaa 48 yajayo


Klabu ya Manchester United inatarajiwa kumsaini kiungo wa Juventus Paul Pogba ndani ya masaa 48 yajayo baada ya kukubali kulipa ada ya wakala wake.
Taarifa za ndani ya klabu hiyo zimedai kuwa tayari zimeshakubaliana na Juventus kwa ada ya uhamisho wa mchezaji huyo ambaye anatarajiwa kufanya vipimo vya afya yake muda wowote huko nchini Marekani alipokuwa kwa kwenye mapumziko yake ya kujiandaa na msimu mpya.
Pogba anatarajiwa kuweka rekodi ya kuwa ndiye mchezaji ghali zaidi kuuzwa kweye tasnia ya soka huku ikikadiriwa kuwa United wamekubali kulipa kiasi cha zaidi ya paundi milioni 100 ili kuipata saini ya mchezaji huo mwenye miaka 23 anayewaniwa na timu nyingine ya Madrid.

Mwigulu anasa Wachina 72 wakiishi kinyemela nchini

Mwigulu Nchemba

WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza katika Mgodi wa Dhahabu wa Nyamahuna mkoani  Geita na kukuta Wachina 72 kati ya 100 wakiishi na kufanya kazi bila vibali.
Akizungumza katika mgodi huo unaomilikiwa na Mtanzania, Andrew Obole, Mwigulu alisema alifika hapo kutokana na kuona taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya jamii.
Mwigulu alisema taarifa hizo zilimuonyesha Masanja Shokera akicharazwa bakora na raia wa mmoja wa China, Lee Swii, kwa madai ya kuiba mawe ya dhahabu Julai 6, mwaka huu.