Sunday 30 April 2017

ZILIZOMUBASHARA KATIKA MAGAZETI YA LEO JUMATATU 01 MAY 2017




Nape:Heshima ya binadamu na maana ya kweli ya ubinadamu ni kutokaa kimya pale uovu unapotendeka


Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amemkumbuka marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuamua kutumia maneno yake katika kufikisha ujumbe wake kwa wananchi kupitia ukurasa wake wa twitter 

Mhe Nape Nnauye alikuwa akitoa ujumbe kuwa maana ya ubinadamu na heshima ya binadamu ni kutokaa kimya pale jambo la uovu linapokuwa likitokea, akiwataka wananchi kutokaa kimya wanapoona kuna jambo la uovu linatendeka.
Ili kufikisha ujumbe huo vizuri Mhe. Nape Nnauye ilibidi atumie clip ya video ya marehemu baba wa taifa, Julius Kambarage Nyerere wakati akihotubia kwa mara ya mwisho katika Mkutano Mkuu. Ambapo mwalimu alisema maneno haya kwa lugha ya kiingereza  
"Hotuba yangu ya mwisho kwenye huu mkutano mkuu, nimeelezea matukio na mienendo na mahitaji kwa namna ambavyo sisi Watanzania tuonavyo, kukaa kimya pale tuonapo hatari, kutulia tu pale tuonapo sera hatari ambazo ziko kinyume na kulinda amani na haki, kufanya hivyo itakuwa tunaachia uhuru wetu na utu wetu kamwe hatutafanya hivyo" Mwalimu Nyerere 

Man U yatoka sare na Swansea City,


 Mshambuliaji wa Manchester United, Marcus Rashford akienda chini baada ya kuangushwa na kipa wa Swansea City, Lukasz Fabianski na refa Neil Swarbrick kuamuru penalti ambayo ilifungwa na Wayne Rooney kuipatia timu yake bao la kuongoza dakika ya 45 na ushei katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford, kabla ya wageni kusawazisha kupitia kwa Gylfi Sigurdsson dakika ya 79 


Mbeya City Yapata Mdhamini Wa Vifaa Vya Michezo

 Mfano wa Vifaa vya michezo vitakavyotumiwa na Timu ya Mbeya City kuanzia msimu ujao.

 Mwenyekiti wa Timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda akisaini mkataba wa makubalino na uongozi wa Kampuni ya Sports Master chini yake Fadhili Nsemwa (kulia).

Mwenyekiti wa Timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda (kushoto) akipokea mkataba kutoka kwa Kiongozi wa Sports Master ambao ni wadhamini wapya watakaosimamia maswala yote ya vifaa vya michezo vya Timu hiyo, Fadhili Nsemwa, baada ya kusainiana makubaliano.
Timu ya soka ya Mbeya City imepata mfadhili mpya wa timu hiyo ambaye atakuwa anasimamia maswala yote ya vifaa vya michezo ikiwemo jezi zote za timu hiyo zitakazotumiwa na wachezaji na zile za mashabiki kuanzia mwezi wa saba mwaka huu. Viongozi hao wamesaini mkataba wa udhamini huo uliofanyika katika ukumbi mdogo wa hoteli ya Mbeya Hill View kwa kuwaalika wadau wa mbeya city na vyombo vyote vya habari.

Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe hazipandisha hoteli za Dar kuwa za nyota tano

  Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akizungumza kabla ya kukabidhi vyeti vya kutambua hadhi za Hotel zilizopo jijini Dar es Salaam na kwa kuzipa madaraja mpaka nyota tano  katika soko la utali hapa nchin, katika hafla fupi iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

  Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe  akikabidhi cheti kwa Mkurugenzi wa  Masoko na Mauzo wa Serena Hoteli, Seraphin Lusala baada ya Hoteli hiyo kutambuliwa kuwa na hadhi ya Nyota tano katika mkoa wa Dar es Salaam, katika hafla fupi iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam

  Majaji ambao waliokuwa wakitoa maksi ya hadhi za hoteli hapa nchini wakisimama kujitambulisha kwa wageni waliofika.

  Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Generali Gaudence Milanzi akizungumza na Wamiliki wa Mhoteli jijini Dar es Salaam leo kabla ya kukabidhi vyeti vya madaraja ya hotel zao.

 Afisa utalii kutoka bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Irene Mville akitoa maelekezo kwa wadau wa mahoteli ambao walifika katika hafla ya ugawaji wa madarajana viwango katika Hoteli zilizopo jijini Dar es Salaam .

 Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akiwa katika picha ya pamoja na wamiliki wa Hotel jijini Dar es Salaam.

Manuwari za China zatia nanga Ufilipino

Manuwari za Uchina zimewasili Ufilipino kwa mara ya kwanza baada ya miaka saba huku Ufilipino ikiimarisha uhusiano wake na Uchina.
Manuwari hizo tatu zilitia nanga mjini Davao.
Ziara hiyo inafanywa siku moja baada ya mkutano wa nchi za Kusini Mashariki mwa Asia, ambao ulifanywa Ufilipino ambapo malalamiko dhidi ya harakati za Uchini katika Bahari ya Kusini ya Uchina, hazikuzungumzwa sana.

Kabla ya Rodrigo Duterte kuwa rais wa Ufilipino, nchi hiyo ikilalamika vikali juu ya hatua za Uchina katika bahari hiyo.

Rais John Magufuli:' Napenda muniamini kuwa mimi nipo kwa niaba yenu, najua huu Urais si wangu

 
. Rais John Magufuli ameipa kwaya ya Jimbo Katoliki la Moshi, Parokia ya Kristo Mfalme, Sh1milioni ili irekodi nyimbo.
Pia imeipa kwaya ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri(KKKT) Usharika wa Moshi Mjini, Dayosisi ya Kaskazini mkoani Kilimanjaro  Sh 1milioni ili kurekodi  nyimbo.
 Rais ametoa mchango wake huo leo aliposali katika makanisa hayo mjini Moshi na kuwaomba waumini wa makanisa hayo wamuoembee.
Rais Magufuli amesema hatua zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano zina lengo la kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli ya taifa linalomuamini Mungu.

Papa Francis ataka mzozo wa Korea Kaskazini Marekani upate suluhu

Kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Francis anataka mjadala wa kimataifa uandaliwe wa kususluhisha mvutano unaozidi kutokota kati ya Marekani na Korea kaskazini akisema kwamba swala hilo limekuwa kaa la moto.
Papa Francis amewaambia wanahabari kwamba mzozo baina ya mataifa hayo huenda ukazua vita vitakavyoangamiza watu wengi.
Amesema kwamba umoja wa mataifa umepoteza nguvu zake.
Awali manowari ya kivita ya Marekani iliwasili karibu na rasi ya Korea, saa chache baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la kombora ambalo lilitibuka.
Rais wa Marekani Donald Trump ameishutumua Korea Kaskazini kwa kuiokosea heshima jirani wake China na rais wake.
Hivi majuzi Trump alimulika rais wa China Xi Jinping na kumpongeza kwa kujitahidi kutatua mzozo wa Korea Kaskazini.
Jaribo la kombora la Korea Kaskazini lilijiri saa chache baada ya baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa kujadili mpango wa nuklia wa Korea Kaskazini

Saturday 29 April 2017

ZILIZOTAWALA KATIKA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI 30 APRIL 2017




Jerry Muro:Unaponiondoa mimi na Haji kwenye mpira, mbadala ni nani?

 Image result for jerry muro
Afisa Habari wa zamani wa Yanga Jerry Muro amedai kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF linawagawa mashabiki wa mchezo huo nchini ili liwatawale.
Muro amesema kuwa kitendo cha TFF kumfungia yeye pamoja na Afisa Habari wa Simba Haji S. Manara ni kwa sababu Shirikisho hilo linajaribu kuwagawa wapenda mpira Tanzania ili liwatawale vizuri.

Akizungumza kwenye Clouds 360 ya Clouds TV April 29, 2017 Muro ameweka wazi kuwa atarudi katika nafasi yake katika klabu ya Yanga mara tu atakapomaliza adhabu yake, akisema: “Yah! Mimi ni mwanachama wa Yanga tangu nikiwa mdogo. Nilipokuwa Yanga, nilikuwa nafanya kazi zangu kama kawaida na Yanga siondoki. Akili ndogo inapokuambia kaa pembeni, unakaa pembeni kwa sababu akili kubwa haiwezi kupambana na akili ndogo.

leo Antony Joshua Na Wladimir Klitschko Kuzichapa Wembley Stadium

Mashabiki wa masumbwi duniani wanasubiri kwa hamu pambano la uzito wa juu kati ya bondia chipukizi wa wingereza Antony Joshua dhidi ya mkongwe Wladmir Klitschko mchezo utakao chezwa Leo katika uwanja wa Wembley.
kuelekea mchezo huo mabondia hao walipata fursa ya kuongea na waandishi wa habari na pia zoezi la kupima uzito kuelekea pambano lao la kuwania ubingwa wa uzito wa juu wa dunia.





Asali inavyoweza kutibu magonjwa mbalimbali

Huko Misri kuligunduliwa mwili wa mtoto ambao haukuoza katika mojawapo ya wafalme wa zamani ,mwili huo ulikuwa umetiwa ndani ya chombo kilichojazwa asali.Tukio hili laonyesha kuwa asali ina siri kubwa iliofanya mwili wa mtoto huyu kutooza tangu miaka 4500 iliyopita.

Image may contain: candles 1.Kujikuna
Tia asali ndani ya kikombe na kisha ongeza vaselini na mafuta waridi jipake mahala panapowasha asubuhi na jioni,na jiepushe na vinavyochochea kujikuna.
2.Uzuri wa uso
Upake asali uso wote wakati mwili upo katika mapumziko baada ya robo saa osha uso kwa maji ya vuguvugu na kausha,halafu jipake kidogo mafuta ya zaituni.Endelea kufanya hivi kwa muda wa wiki moja mfululizo.
3.Jeraha(kidonda)
Paka asali penye kidonda na funga bandeji na uepushe umajimaji,usifungue mpaka baada ya siku tatu.
4.Kuungua
Chukua asali na uchanganye na vaselini kiasi kama kama hicho cha asali halafu jipake mahala palipoungua asubuhi na jioni mpaka ile ngozi iliyoungua ibanduke.Au changanya yai katika asali kiasi cha kijiko kimoja na jipake mahala palipoungua kila siku.
5.Kuua chawa na mayai yake
Paka kichwa chote asali pamoja na kukisugua vizuri mpaka uhakikishe kuwa  imeingia vema hadi mashinani halafu jifunge kitambaa iwe kabla ya kulala.Asubuhi osha kwa maji ya uvuguvugu pamoja na kuchana nywele .Endelea namna hii kwa muda wa wiki moja mfululizo.
6.Kukosa usingizi
Chukua glasi ya maziwa na changanya na asali kijiko kikubwa na unywe kabla ya kulala.
7.Maradhi ya kinafsi na wazimu
Mgonjwa ale asali na mgongo wake uumwe na nyuki,na pale alipoumwa apake asali.Aendelee hivyo japo kila mwezi mara moja na aendelee kula asali,kutafuna nta yake na nyuma ya kichwa chake apake sega la nyuki kidogo.
8.Kifafa
Asubuhi kabla ya kunywa chai,anywe asali kikombe kimoja na jioni kikombe kimoja.Aendelee hivyo kwa wiki moja.
9.Magonjwa yote ya macho
Jipake asali asubuhi kama vile unapaka wanja,vilevile kabla ya kulala pamoja na kunywa asali kijiko kimoja.
10.Kiungulia/Asidi
Meza punje ya kitunguu saumu kabla ya kula meza na kikombe cha maziwa yaliyochanganywa asali kijiko kimoja kwa muda wa siku tano.
11.Kuhara/Tumbo la kuendesha
12.Kufunga choo
Kufunga choo ni kinyume cha kuharisha.Chukua maziwa baridi kikombe kimoja korogea asali ndani yake kijiko kimoja halafu unywe,fanya hivyo asubuhi na jioni.
13.Kutapika
Chemsha karafuu na korogea asali halafu kunywa kiasi cha kikombe kimoja kabla ya kula chakula;kutapika na kichefuchefu kutaisha.
14.Kidonda
Chukua asali nusu kikombe na kikombe cha maziwa na changanya unga wa ganda la ndizi lililokaushwa kijiko kimoja,Tumia asubuhi na jioni kwa muda wa mwezi
15.Maradhi ya kifua
Chukua juisi ya figili kikombe kimoja na korogea asali kijiko kimoja.Kunywa asubuhi na jioni.Vilevile unaweza kuchukua ubani dume ukautia ndani ya maji na kuchanganya na asali kijiko kimoja ili kuyapa mapafu nguvu.
16.Harufu mbaya mdomoni
Chukua asali vijiko viwili ikoroge ndani ya maji na kisha chemsha katika moto mdogo mpaka itoe moshi. Vuta puani na mdomoni moshi huo kupitia kwenye paipu au bomba lililofungwa vizuri katika chombo.Endelea na tiba hii pamoja na kutafuna nta ya asali.
17.Kukaukiwa na sauti
Fany kama dawa hiyo iliyotangulia (harufu mbaya)pamoja na kugogomoa asali na chumvi kidogo kwa muda wa siku tatu.
18.Homa ya mafua(Influenza)
Vuta puani moshi wa kiziduo cha asali na kitunguu maji kabla ya kulala pamoja na kunywa asali kijiko kimoja baada ya chakula.Tiba hii hufanywa kwa kuchukua asali na kitunguu maji kidogo kilicho chambuliwa maganda;vikatiwa katika chombo chenye maji na kuchemsha juu ya moto mdogo hadi moshi utoke.
19.Malengelenge ngozini


Friday 28 April 2017

ZILIZITIKISA LEO KATIKA MAGAZETINI JUMAMOSI 29 APRIL 2017




Shabiby:’Hakuna watu wanafiki kama sisi wabunge,

 Image result for Ahmed Shabiby
Mbunge wa Gairo Ahmed Shabiby alisimama Bungeni kuchangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na mawasialiano ambapo kati ya vitu alivyoishauri serikali ni pamoja
na kuacha tabia ya kuingilia baadhi ya majukumu ya bodi inazokuwa ikiziunda kwa ajili ya utendaji.

Shabiby amesema…’Hakuna watu wanafiki kama sisi baadhi yetu wabunge, miaka ya nyuma tulikuwa tunapiga kelele tunashindwa hata na nchi kama Rwanda kwa kutokuwa na ndege, leo ndege zimekuja mnasema ndege sio kipaumbele cha kwanza’ –Ahmed Shabiby

‘Mimi nasema vyote ni vipaumbele lakini viongozwe kwa mujibu wa sheria za kibiashara, mfano unaunda bodi inawataalamu alafu yanatoka maagizo ya kuingilia hiyo bodi’ –Ahmed Shabiby

Zlatan Ibrahimovic akataa mshahara wa Man United

 Image result for Zlatan Ibrahimovic
Mshambuliaji wa kimataifa wa Sweden anayeichezea Man United ya England Zlatan Ibrahimovic amerudi kwenye headlines baada ya maamuzi yake kuandikwa na vyombo vya habari, Zlatan ameripotiwa na mtandao wa dreamteamfc.com kuwa amekataa kulipwa mshahara na Man United.
Zlatan Ibrahimovic atakuwa nje ya uwanja katika kipindi cha miezi 9 baada ya kuumia goti lake la kulia wakati wa mchezo wa marudiano wa  Europa League dhidi ya Anderltch ya Ubelgiji, Zlatan anayelipwa mshahara wa pound 250000 kwa wiki alijiunga na Man United kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Waziri Kairuki Akikabidhi Ripoti Kwa Rais Magufuli

Rais Magufuli Wenye Vyeti Feki Jela Miaka 7

Rais Magufuli Na Wizi Unaofanywa Na Wawekezaji Nchini

Polisi waizuia CUF upande Maalim Seif.kufanya Usafi

 Image result for maalim seif
Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, imepiga marufuku usafi  ulipangwa kufanywa na Chama cha Wananchi CUF upande maalim seif.
 Hayo yamekuja baada ya Wanachama wa CUF zaidi ya elfu tano na wabunge wa CUF 42 ambao wanamuunga mkono Maalim Seif kupanga kwenda kusafisha ofisi ya chama chao CUF Makao Makuu Buguruni siku ya Jumapili ya tarehe 30 mwezi huu wa nne.

Akiongea na waandishi wa habari Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya CUF, Abdallah Mtolea akiwa ameambatana na wabunge wengine 41 amesema wameamua kufanya usafi katika ofisi ya chama chao baada ya kuona ofisi hiyo imekuwa ikitumiwa vibaya na Profesa Lipumba na genge lake kufanya mipango ya kuvamia mikutano ya watu, na matukio ya kihalifu.

"Siku ya Jumapili ya tarehe 30 mwezi wa nne mwaka huu, wanachama wa Chama Cha Wananchi (CUF) ambao hawamkubali Professa Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti wa CUF wameamua kwenda kufanya usafi kwenye ofisi zao za Buguruni ofisi kuu za chama, hatua hii imekuja baada ya kuona ofisi ile inatumika vibaya kimekuwa ndiyo kijiwe cha wahuni kupanga matukio ya kihalifu kwenda kuvamia mikutano, kuvamia watu sisi kama wanachama tumesema hapana hatuwezi kuacha ofisi yetu itumike vibaya hivyo" alisema Mtolea

Mbali na hilo Mtolea amesema wazo hilo lilianzia Temeke lakini limepokewa vyema na sehemu zingine hivyo baadhi ya wanachama kutoka Zanzibar, Tanga na wanachama wa maeneo jirani wataunga na wabunge 42 kufanya usafi huo hapo Buguruni.

Tangazo la kuitwa kazini kwa Madaktari

Image may contain: text

Thursday 27 April 2017

ZILIZOLETA MASHIKO KATIKA VYUMBA VYA HABARI MBALIMBALI MAGAZETINI IJUMAA 28 APRIL 2017




Taifa la Venezuela lajiondoa muungano wa mataifa ya Marekani

Venezuela imetangaza kujiondoa kutoka kwa shirika la Umoja wa Mataifa ya Marekani Kusini OAS, ikidai mataifa ya jumuiya hiyo yanaingilia maswala ya ndani ya Venezuela.
Waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Bi Delcy Rodriguez ametoa kauli hiyo punde tu baada ya kikao cha jumuiya hiyo ya OAS kupiga kura ya kuitisha kikao maalum cha mawaziri wa mambo ya nje kujadili mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini humo.
Mataifa jirani ya Venezuela yameelezea wasiwasi wao kuhusu kuzorota kwa hali ya kisiasa na kiuchumi inayoendelea nchini humo.
Wakati huohuo mtu mwengine tena amefariki huko mjini Caracas katika maandamao ambayo yameikumba Venezuela kwa wiki ya tatu sasa yaliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 30.
Mtu huyo alifariki baada ya kugongwa na bomu la kutoa machozi lililorushwa na polisi waliokuwa wakijaribu kuwatawanya waandamanaji.
Waandamanaji hao wamekuwa wakimtaka rais wa nchi hiyo ajiuzulu kutokana kuzorota kwa uchumi wa nchi hiyo jambo lililosababisha upungufu mkubwa wa chakula.

Vikao vya Bunge

unnamed
 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Tulia Ackson  akiongoza kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
unnamed
Naibu Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Ajira Kazi na watu wenye Ulemavu  Mhe. Anthony Mavunde akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamadi Masauni akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 1
Naibu Waziri wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Edwin Nyonyani akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 2
 Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Rita Kabati akiuliza swali  katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 3
 Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe. Martha Umbula akiuliza swali  katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 4
Mbunge wa Kilombero Peter Lijualikali (CHADEMA) akiuliza swali  katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 5
Mbunge wa Kalenga (CCM) Mhe Mhe.Godfrey Mgimwa akiuliza swali  katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 6
Wabunge wakifuatilia hoja mbalimbali katika kikao cha kumi na tatu cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 7
Mshindi wa Medali ya Dhahabu katika mbio za Mumbai za mwaka 2017 Bw.Alphonce Felix Simbu akiwaonyesha Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hawapo pichani)  medali na Tuzo aliyoshinda katika mbio hizo leo Mjini Dodoma Aprili 27, 2017.
A 8
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Harrison Mwakyembe akipokea Tuzo kutoka kwa Mshindi wa Medali ya Dhahabu katika mbio za Mumbai za mwaka 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu katika viwanja vya Bunge leo Mjini Dodoma.Wengine pichani ni Mkuu wa Utawala na Mafunzo JKT Col.K.J.Mziray,Luteni Col.J.P Meidini,Mkuu wa Kambi JKT Makuyuni Meja Mvula na Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Multichoice Tanzania Bw.John Mshana.
A 11
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akipokea Tuzo kutoka kwa Mshindi wa Medali ya Dhahabu katika mbio za Mumbai za mwaka 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu katika viwanja vya Bunge leo Mjini Dodoma.Wengine pichani ni Mkuu wa Utawala na Mafunzo JKT Col.K.J.Mziray,Luteni Col.J.P Meidini,Mkuu wa Kambi JKT Makuyuni Meja Mvula na Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Multichoice Tanzania Bw.John Mshana.
Picha Zote na Daudi Manongi- Dodoma MAELEZO,DODOMA