Saturday 30 April 2016

Basi la Kampuni ya Sabena limepinduka na Watu Wanne Wamefariki Hapo Hapo na 29 Kujeruhiwa


 

Watu wanne wamekufa papo  hapo na wengine 29 kujeruhiwa baada ya basi la HBS linalodaiwa kuwa ni Mali ya kampuni ya Sabena Walilokuwa Wakisafiria kutoka Jijini Mbeya kwenda Tabora kuacha njia na kupinduka katika eneo la Maji mazuri, barabara kuu ya Mbeya – Chunya wilayani Mbeya.
 
Basi hilo likiwa limebeba abiria Wengi kuliko uwezo wake, lilianza Safari Yake ya kuelekea Tabora likitokea jijini Mbeya, lakini inadaiwa kuwa likiwa kwenye Mtelemko na kona kali za Mlima Mbeya likafeli breki na ndipo Dereva Wake akaamua kuruka na kuliacha likijiendesha lenyewe hali Ambayo ilisababisha lipoteze Mwelekeo na kuanguka mtaroni.

Muuguzi wa Zamu katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya nyanda za Juu kusini, Jesca Kahangwa amethibitisha kupokea miili ya watu wanne na Majeruhi 29 wa ajali hiyo, Huku akidai kuwa hali za Majeruhi Wengi Bado ni Mbaya.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amewahi katika eneo la ajali na baada ya kupata maelezo ya chanzo Cha ajali hiyo, akaliagiza jeshi la polisi kuwatafuta na kuwakamata haraka Dereva, kondakta na mmiliki wa Gari hilo kwa kosa la kuendesha Gari bovu Barabarani.

Magazeti ya leo Jumapili 1 Mei 2016

Mr Blue amemtupia Shutuma Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi amemuibia Wimbo Wake wa Freedom





Msanii  wa Muziki wa Hip Hop, Bongo Kheri Sameer ‘Mr Blue’ Ameendelea kumporomoshea lawama Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambaye pia Ni msanii wa Muziki wa Hip Hop, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kuwa Usumbufu aliokuwa anampa ili kuiachia ngoma yake ya Freedom Ulimsababishia ‘rabsha’ ndani ya ndoa yake. 

Shutuma hizo anazozitoa Blue ni Mwendelezo wa ‘drama’ inayoendelea kati yake na Sugu ambayo kwa sasa ndiyo Habari ya Mjini kufuatia Madai ya Blue kuwa Mheshimiwa huyo alimzunguka kwa kuuchukua Wimbo wake huo ambao mwanzo yeye alimshirikisha, Akaurekodi Upya huku akifuta Mashairi yake lakini kama haitoshi ‘Akashuti’ video, Jambo ambalo Blue Analiona kuwa ni Uonevu.
 
“Kwanza Sugu alinisababishia Matatizo ndani ya Ndoa Yangu mpaka Nikawa sipokei simu zake. Alikuwa ananipigia Simu kila Muda na kila Siku akiuliza ‘project’ inatoka lini hadi mke wangu akawa anauliza kuna nini kati yetu.
 
 Mwanzoni nilimweleza hali Halisi lakini kwa namna Sugu alivyokuwa Ananisumbua ilifika hatua mke wangu akadhani kuna Jambo lingine Tofauti, kukawepo na rabsha za hapa na pale lakini Sasa Nimeweka Mambo sawa,” alisema Blue.

Alipotafutwa Sugu kuhusu suala hilo, Hakupokea Simu na hata Alipotumiwa Ujumbe mfupi, hakujibu lolote.

Mkuu wa Mkoa Dar es salaam Paul Makonda ameongoza Wakazi wa Jiji kufanya Usafi


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi wakiongoza maelfu ya Wakazi wa Jiji la Dar es salaam katika matembezi maalum ya kampeni ya kuhamashisha usafi katika jiji hili #Dar es salaam Ya Makonda, Usijifanye Mstaarabu kuwa  Mstaarabu. Matembezi hayo Yalimeanzia katika Uwanja wa Karume, Ilala na kuishia katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es salaam.
Sehemu ya wananchi wa Jiji la Dar es salaam wakishiriki Matembezi ya maalum Ya kampeni ya kuhamashisha usafi, kuunga mkono kauli ya Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda aliyeongoza matembezi hayo. #Dar es salaam Ya Makonda, Usijifanye Mstaarabu kuwa  Mstaarabu.

TPDC limekanusha Taarifa Zilizosambazwa katika Mitando ya Kijamii na kuhusika Kufungua Akaunti ya ESCROW Katika Benki ya Stanbic



 
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, linapenda kutoa taarifa sahihi juu ya taarifa ambazo zimekuwa zikiandikwa na vyombo mbalimbali vya habari, pamoja na mitandao ya kijamii kuhusu TPDC kufungua Akaunti za ESCROW katika Benki ya Stanbic.

Ni vyema ikaeleweka kwamba, Akaunti ya  ESCROW  ni Akaunti  maalumu inayoweza kufunguliwa  baina ya  Kampuni, Taasisi,  au Mashirika mbalimbali ya binafsi na yale ya umma kwa matumizi maalumu. 

Lengo la Akaunti ya ESCROW ni kuhifadhi fedha au kupitisha malipo kwa ajili ya shughuli maalum ikiwemo miradi au kazi yoyote maalumu na malipo haya hufanyika baada ya pande mbili kuridhia.

TPDC ilifungua Akaunti tatu za Esrow baada ya Serikali  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BOT)  kutoa idhini kufunguliwa kwa akaunti kwenye Benki ya Stanbic, ikiwa ni moja ya masharti yaliyowekwa na mkopeshaji ili  kutoa mkopo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mipya ya gesi asilia, kutoka Benki ya Exim ya China. 

Mkopeshaji alipendekeza Akaunti hizo zifunguliwe kwenye benki ya Stanbic na ambapo taratibu za manunuzi zilizingatiwa, ikiwemo ushindanishaji wa watoa huduma.

 Akaunti hizo tatu zilizofunguliwa ni pamoja na:
1. Akaunti ya Mapato ya Gesi
Lengo la akaunti hii ni hifadhi mapato yote yatakayo tokana na mauzo ya gesi kwa njia ya bomba jipya.

2.  Akaunti ya Uendeshaji
Akaunti hii ina jukumu la kuhifadhi fedha zinazohitajika kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa mradi wa miundombinu hiyo mipya ya gesi asilia.

3.  Akaunti ya Kulipia Deni
Akaunti hii imefunguliwa kwa ajili ya kulipa madeni yatokanayo na mkopo.

Akaunti hizi zinadhibitiwa na masharti yaliyowekwa kwenye makubaliano (Mkataba) ya Menejimenti ya Akaunti hizo yaliyosainiwa kati ya Benki ya Stanbic (kama Benki ), TPDC (kama mtumiaji wa mwisho), Benki ya Exim ya China (kama Wakopeshaji) na Wizara ya Fedha (kama mdeni kwa niaba ya Serikali ya Tanzania).

TPDC inapenda kuufahamisha umma kwamba, baada ya taratibu zote hizo kufuatwa, si sahihi kuuhusisha mchakato huu na tuhuma zozote na ukiukwaji wa sheria za nchi. 

Aidha, ifahamike kwamba Akaunti ya ESCROW ni akaunti ya kawaida kabisa katika utekelezaji wa miradi kama huu wa gesi asilia.

TPDC Kwa Maendeleo ya Taifa!
Imetolewa na:
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji- TPDC
S.L.P 2774
Dar Es Salaam

Tanesco Wamezindua Huduma Mpya Kwa Wateja Unaoitwa Tanesco Huduma

Na Mwamvita Mtanda
Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco), limezindua Huduma mpya inayotoa nafasi kwa wateja kutoa na kupata Taarifa kupitia Mfumo wa Mawasiliano uliounganishwa kwenye Simu za kiganjani unaoanza kwa Majaribio katika Mkoa wa kihuduma wa Kinondoni Kaskazini.

Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema jana Jijini Dar es salaam kuwa, mfumo huo ambao uko kwenye programu Maalumu, Utasaidia kuboresha Utendaji Kazi wa Shirika.

“Mfumo huu Utaongeza kasi ya Uwajibikaji wa watendaji kuwahudumia Wananchi, lakini kwa sasa Tumeuanza kwa Majaribio katika Mkoa wetu wa Kinondoni Kaskazini, Wateja wetu watatoa Taarifa za Matukio yanayowakabili hata wale Wanaoomba Rushwa, watujulishe tupate Ushahidi Tuchukue hatua,” alisema Mramba.

Alisema mfumo huo Umeundwa kutokana na Ushirikiano kati ya Tanesco na Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (Costech) na alisema itawapunguzia Usumbufu wateja wa kupiga Simu kwenye vituo vya Huduma Wanapokuwa na Malalamiko Binafsi au ya maeneo Wanayoishi.

“Naamini majaribio haya yatakuwa na Mafanikio, Yatawawezesha Wateja wa Tanesco wote nchini kuunganishwa kupata huduma hiyo,” alisema Mramba.

Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dk Hassan Mshinda alisema Hatua hiyo imewapa Moyo wa kuendelea kujituma zaidi kwa kuwa vijana wao Wamepata nafasi ya kuonyesha kiwango cha ubunifu kwenye Masuala ya Teknolojia kulingana na Dunia inavyokwenda.

Meneja Mwandamizi wa Mauzo na Masoko wa Tanesco Kinondoni, Nicholaus Kamoleka alisema Mfumo huo unaitwa ‘Tanesco  Huduma’ wateja wataipata kwa kuiomba kupitia Soko la programu la Google liitwilo ‘Play Store’.   


TCRA:Wafanyabiashara wa Simu


 
Na Chrispino Mpinge
 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kiama kwa Wafanyabiashara wa vifaa vya Mawasiliano, kuacha kuwahadaa Wananchi kwa kutoa Punguzo ili kuwashawishi kununua simu Bandia na kutishia kuwafunga miaka 10 Jela, Faini ya Sh30 Milioni au Vyote kwa pamoja Watakaobainika.

Hatua hiyo imekuja Wakati Mamlaka hiyo ikiwa katika Hatua ya kutekeleza Mfumo wa Rajisi ya namba za Utambulisho wa vifaa vya Mawasiliano vya Mkononi, huku ikitarajia kuzima Simu feki ifikapo Juni 16.

Akizungumza na vyombo vya habari jana, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCRA, Mhandisi James Kiraba alisema Kuna Wafanyabiashara wajanja Wanaobadilisha Namba za Utambulisho za vifaa vya elektroniki (IMEI) ili Kuwahadaa Wateja kuwa Simu zao siyo Feki.

Kwa Ujanja huo, Namba ya Utambulisho inakuwa inatumika na Simu Zaidi ya Moja na kutambulika na mfumo licha ya kuwa ni feki.

Pamoja na kuonekana ni halisi kwa kipindi Wanachozinunua, alisema simu Hizo Zinazobadilishwa IMEI nazo zitazimwa Juni 16 kwa kuwa ni feki.

“Mamlaka inawakumbusha Wauzaji wa Vifaa vya Mawasiliano vya Mkononi kuwa ni kosa kubadilisha Namba Tambulishi za vifaa vya simu za mikononi (mobile devices), kwani Adhabu yake ni kifungo kisichozidi Miaka 10 au Faini isiyopungua Sh30 Milioni au vyote kwa Pamoja,”alisema.

Alisema kumekuwa na udanganyifu kwa baadhi ya wauzaji wa simu kwa kutoa Punguzo kwa wananchi ili kuwashawishi kuzinunua simu Bandia kwa Bei nafuu.

Kiraba alisema Wananchi Wanapaswa kuwa Makini na hilo, huku Wakihakikisha kuwa simu zao zimehakikiwa ili kuzuia Usumbufu wa aina yoyote, Utakaoweza kujitokeza wakati kipindi cha Mpito kitakapomalizika.

Alisema idadi ya namba Tambulishi ambazo zilikuwa Hazina Viwango (Bandia) Zimeendelea kupungua kutoka asilimia 30 Desemba mwaka jana Hadi kufikia asilimia 13 Machi.

Alisema Uchambuzi wa Februari ulionyesha idadi ya namba Tambulishi Ambazo zilikuwa Hazina Viwango zilikuwa sawa na asilimia Tatu, vilevile idadi ya namba Tambulishi ambazo zimenakiliwa Zilikuwa sawa na asilimia 18 huku simu Halisi zilikuwa sawa na asilimia 79.

“Uchambuzi wa Machi unaonyesha idadi ya namba tambulishi ambazo hazina viwango zilikuwa sawa na asilimia nne, huku idadi ya namba Tambulishi ambazo zimenakiliwa zilikuwa sawa na asilimia 13, uchambuzi Huu unahusisha makampuni yote ya simu nchini,” alisema

Kujuana Vizuri Kabla ya Kuanzisha Mahusiano


 

 Na Kalonga Kasati

Kumekuwa na imani potofu kwa wanawake kwamba Hawawezi kumwambia ukweli Mwanaume anampenda Kwanza Mpaka Mwanaume aanze lakini ukweli usiopingika ni Kwamba wao pia Hupendi na Mara nyingi wao Wakianza kupenda Hupenda kweli kufikia Stage Hata ya kuhisi kuumwa. Hizi ni dalili za Mwanamke anaekupenda ila anagoma kukwambia tu.
Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama Unampenda na kumthamini au la mfano wa Mambo hayo ni kama kujifanya anaumwa na kauangalia Respond yako kwake ni kiasi gani Unamjali na kiasi gani Utahangaika kwa ajili yake.

Kucheka kwa Nguvu Hata kwa kitu kisicho chekesha Endapo Wewe Umezungumza. Mara Nyingi Ataonesha Uso wa furaha Hata kama si furaha ya kweli


Hujisikia wivu anapokuona na Wasichana Wengine. Ukiwa unachart nao na Ukiwaita Majina Ya kimahaba. Hapendi na hupenda yale afanyiwe Yeye tu Hata kama Sio Mpenzi wako.

Anakumbuka siku zako Muhimu. Hukumbuka kama Vile siku yako ya kuzaliwa hatoweza kuisahau kufanya ipite Bila kukutakia heri ya Siku ya kuzaliwa kama sivyo Ukifaulu Mtihani Au chochote katika Maisha yako atakuwa Mbele kukupongeza.

Eye contact hupendelea sana kukuangalia machoni Muda Wote ambao Mtakuwa Mkizungumza pamoja akidhani kuwa utamuelewa ni kiasi Gani anakupenda kupitia vile Anavyokuangalia. Ila Wengine Huona aibu kuwatazama Wavulana Wanaowapenda hivyo Huweka Jicho la wizi na kukuvizia.

Hupenda kukaa muda mwingi na wewe. Hawezi kupoteza Hata Sekunde Ukimuhitaji kwa Mazungumzo. Anajisikia furaha kukaa na Wewe Muda Mrefu bila kuchoka. Anaweza akaacha Kila kitu anachokifanya ili ajumuike na Wewe na akikaa na Wewe hupendelea Sana Mwanzoni Kukujua Wewe Zaidi na Hukujengea Mazingira ya Wewe Uwemuwazi ili Umwambie Mengi kuhusu Wewe na pia akiwa na Wewe atakuwa Muwazi zaidi Hadi Mavazi aliyovaa Hupenda Sana kujua Yako na kukuambia yake na Hupenda kujua ni Mavazi Gani Yeye akivaa Anakuvutia zaidi Na atajitahidi kuwa anavaa ya style hiyo kukufurahisha.

Kama Msichana anakupenda yupo Tayari kusacrifice. Ni kitu ambacho Hakuna mtu ambaye Anaweza akafanya kwa Mtu Mwingine. Utamuona Vipi huyo Msichana alivyo kwako na kwa Wengine. Yaani yupo Tayari akose lakini Wewe Upate na kwa Mwingine anaweza Akamwambia Hana alichoombwa lakini akakupa Wewe kama Pesa na vitu vingine.

Mikwaruzano ikitokea katika Urafiki wenu Hayupo tayari kukupoteza kabla hajakwambia Nakupenda.Kwa kuwa anakupenda endapo ikitokea mikwaruzano Basi atafanya Juu chini Kuyaweka Mambo sawa ili asikukose.

Mwanamke anaekupenda hupenda kujua Mengi sana kuhusu Wewe na hapo inamsaidia kukununulia Zawadi za Mitego kama Boxer , na Mara nyingi Hupenda Rangi Nyeupe, au kukununulia perfume , aSbuni ya kuoge ya Manukato,soksi, vest, bukta, Saa,raba, t-shirt. Na kama Mkitoka Wote Mkaenda Shopping ataakutega kwa kukuonyesha Vitu na Wewe Ukionekana Umependa kitu Hatonunua siku hiyo ila atanunua iSku inayofuata na kukuletea kama suprise.


Mwanamke anaekupenda ili akujue zaidi Hupendelea msosi mle Sehemu Mmoja na kama ikitokea Mwanaume Hawezi kuhama Sehemu anayokula Mwanamke Yupo Radhi kubadili na kumfuata Mwanaume Hata kama Sehemu hiyo yeye Haipendi na kama Unakula kwako Basi Atakutega na kuja kupika kwako ili Mle na atakuwa anapenda Kununua vitu vya kupika ili tu Akutekena Uone Upendo wake.

Ukiona Dalili kama Hizi Mwanaume Tafadhali Fanya Mpango wa kumweka ndani (oa) Mwanamke huyo kabla ujachelewa alafu Ukaja kuangukia kwa wale Wanawake Wenye sifa ya Mbaya

Hafla ya Kuagwa Kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro

  
Hafla ya kumuaga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya mstaafu Abass Kandoro leo. Amewashukuru sana Wananchi wa Mkoa wa Mbeya kwa Ushirikiano Waliompa katika Uongozi wake wa Miaka Minne Mkoani Mbeya 
Mkuu mots wa Mkoa wa Mbeya Amos Mskalla amewaomba Wananchi Ushirikiano katika kutekeleza Majukumu yake amewahidi ataanzia alipoishia Mtangulizi wake na amewaekeza kuwa amekuja Mbeya kufanya kazi na Siasa na Dira yake ni kutekeleza ilani ya Chama Tawala, kushughulika na Kero za Wananchi, kusimamia Mipango ya Maendeleo na kuhakikisha Mkoa Wa Mbeya Una amani na Utulivu
   

Wolper:Nilikuwa Navaa Nguo za Kiume Kutokana na Wakati Ule Sasa Nimeshakuwa Mchumba wa Mtu


Akiongea kwenye kipindi cha Nirvana, kinachoruka kupitia EATV, Wolper alisema ‘Nilikuwa Navaa vile kutokana na Wakati ule, Sasa hivi nimeshakuwa na Mchumba’.
“Nilikuwa navaa vile kutokana na Wakati ule ulivyokuwa. Kuna watu walikuwa Wanapenda, lakini Sasa hivi Nimeshakuwa Mchumba wa mtu. Ni kweli lazima nivae Gauni, kwahiyo Mtu unatakiwa Ujibadilishe wewe Mwenyewe Usisubiri kubadilishwa,” aliongezea.
Wolper aliendelea kusema, “hata hivyo Bado Sijaacha kabisa, kidogo unakuwa Unagusia Mashabiki zako wanakuwa wanakupenda.”
Hata hivyo Wolper Japo amekiri kuwa na Mchumba Mpya kwa Sasa lakini Hayupo aTyari kuweka Mahusiano yake Hadharani kama Mwanzo alivyokuwa anafanya

....

Elizabeth Michael Maarufu kama Lulu amevishwa Pete ya Uchumba na Dj Majay

 Lulu Amepost Picha Kadhaa Akionyesha Pete yale aliyovalishwa na kuandika maneno haya:

Simplicity z the key.
Kwenye picha nyingine ameandika: Pale Unaposikia Kwa…Kwa…Kwa…Kwa Ya Rihanna Wakati WA kupiga picha #simplicityisthe

Maswali Mengi Kuhusu Kifo cha Papa Wemba





BADO kifo cha Mwanamuziki wa Dansi na Rhumba, Shungu Wembadio ‘Papa Wemba’ kinazidi kuzua Maswali mengi huku watu Mbalimbali wakijenga hoja kuwa huenda Mwanamuziki huyo Mwenye Heshima Afrika aliwekewa sumu kwenye moja ya maiki alizotumia Wakati akitumbuiza Tamashani huko Ivory Coast.
 
Hoja hiyo inayosapotiwa pia na Mtandao wa Kinshasa-makomba.com imeibuka kufuatia video iliyosambaa mitandaoni inayomuonesha Mwanaume Mmoja Mrefu, Mweusi akipanda Jukwaani kisha kuchukua moja ya maiki alizokuwa anazitumia Papa Wemba na kwenda nayo kusikojulikana.
 
Aliirudisha Muda Mchache Baadaye na Papa Wemba alipoitumia tu Ndipo alidondoka chini na kupoteza Maisha usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita.
 
Hata hivyo, taarifa za awali zilidai Mwanamuziki huyo alikuwa Anasumbuliwa na Ugonjwa wa shambulio la Moyo lakini kutokana na Video hiyo huenda Taarifa nyingine ikaibuka.