Mbunge wa Viti Maalum wa Chadema, Upendo Peneza amesema hana sababu za
kuhama chama hicho kikuu cha upinzani nchini huku akiwashangaa
wanaochukua uamuzi huo.
Peneza amesema kuhama chama kunasababisha hasara kwa Taifa kwa kuingia
katika uchaguzi wa marudio huku akipendekeza uchunguzi ufanyike kwa
waliohama ili kubaini ukweli wa sababu wanazozitoa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Desemba 15, Peneza amesema
hajafikiria kuhama chama lakini anasikitika watu walioaminiwa na
wananchi wakajiuzulu kwa kutoa sababu zisizoeleweka.
“Nimehusishwa mimi kuhama chama changu, sina sababu za kuhama ila
ninachotaka ni hawa wanaohama watueleze sababu za kutuingiza katika
hasara ya kurudia uchaguzi,” amesema Peneza.
“Sioni sababu ya kwenda kuunga mkono halafu utuingize gharama, yaani
furaha zako utuingize sisi gharama, hapana…watueleze sababu zao,”
ameongeza
Amesema kuna haja ya kupitia Katiba au kuendeleza mchakato wa Katiba ili
kuwazuia kugombea wale wanaojiondoa kwa sababu zisizoeleweka.
Peneza amesema “kama unasema unaunga mkono, useme umewafanyia nini
wananchi wako au kuunga mkono kwani lazima uchukue kadi ya chama
kingine, Watanzania tunachezewa na watu na huu ni mchezo wa kisiasa
unafanyika.”
Akizungumza kwa msisitizo, Peneza amesema “ninapinga haya kwa sababu
pesa za wananchi hazitumiki vizuri, tunabana matumizi, tunapinga
mafisadi halafu fedha badala ya kwenda katika maendeleo lakini
tunakwenda katika uchaguzi.”
“Tusiharibu hela kwa kile wanachosema tunamuunga mkono, kama Rais
atajenga daraja la Mwanza kwenda Sengerema, nitampongeza, kama chama
changu kitanifukuza haya,” amesema Peneza
“Kiuhalisia shida bado kubwa, mbunge wa Siha angesimama akasema
amenijengea shule, ametatua matatizo ya wakulima, ardhi sawa ila hayo
hayajatekelezwa unamuungaje mkono.”
Kuhusu kuhusishwa kwake na kuhama, Peneza amesema wakati akigombea
alijua kuna CCM yeye aliamua kuwa Chadema ingawa akadokeza kwamba hawezi
kusema atakuwa Chadema maisha yote.
Msajili Msaidizi wa vyama vya siasa nchini, Sisty Nyahonza amesema
sheria inaruhusu kuchukua mkondo wake kwa Mbunge yoyote atakayezidisha
kutumia gharama kubwa katika chaguzi mbalimbali, ambapo amesema gharama
ya juu ni milioni 88.
Hayo amesema kupitia kipindi cha East Africa Breakfast cha East Africa
Radio kuwa sheria hiyo imeanza mchakato mwaka 2006 na kukamilika 2010,
inasema mtu achaguliwe kutokana na uwezo wake wala sio pesa.
Gharama ya kuendesha kampeni za uchaguzi inatokana na ukubwa wa jimbo
lenyewe lakini kuna kiwango maalumu ambacho taasisi imekipanga, kiwango
cha chini kinaanzia milioni 33 huku kiwango cha juu ni milion 88.
''Kila jimbo lina kiwango chake , kama kiwango ambacho kimepangwa
kikipita tunayo nguvu ya kuchunguza namna gani gharama kubwa imetumika
ili muhusika achukuliwe hatua.
Alipoulizwa juu ya kujiridhisha kama kweli wagombea wametumia kiasi
ambacho kimepangwa na taasisi hiyo amesema wana njia nyingi ikiwemo
kushirikiana na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU).
''Tuna njia nyingi za kufahamu kama tuna shaka na matumizi ya kuendesha
kampeni zimezidi, tunashirikiana na Taasisi ya kuzuia na kupambana na
Rushwa, tuna uwezo wa kufuata ripoti zote ambazo zimefanyika kupitia
chama husika pamoja na kutafuta taarifa kwa wasamalia wema''.
Kwa uchaguzi ambao umefanyika mwaka 2015 kiwango cha chama cha siasa
kimeruhusiwa kutumia kiasi cha bilion 17 kwa Rais, Wabunge na Madiwani.
Ambapo katika kampeni za Rais sheria inataka atumie shilingi bilioni 6
hadi mwisho wa uchaguzi, wakati madiwani wanaoishi mijini wametengewa
milioni 8 huku wale wa vijijini watumie milion 6.

Korea Kaskazini imetoa picha za jaribio la kombora lake jipya ambalo
inadai kuwa linaweza kushambulia popote pale nchini Marekani.
Picha hizo zinaonyesha kiongozi wa Korea Kaskazini Ki Jong un na maafisa
wengine kadha ya ngazi za juu jeshini wakisherehekea kombora la
Hwasong-15 wakati likipaa.
Wengi wameshangazwa na ukubwa wa kombora hilo. Picha hii ambayo
haijulikanai ilichukuliwa lini na iliyotolewa na vyombo vya habari vya
taifa inaonyesha Kim akilikagua kombora hilo.
Michael Duitsman, mtafiti katika kituo kimoja alisema kuwa kombora hilo
ni kubwa kuliko kombora la kwanza la Hwasong-14 "ni nchi chache tu
zinaweza kuunda kombora kama hilo na Korea Kaskazini imejiunga nazo."
Pia linaonekana kuwa na kichwa kikubwa ikimaanisha kuwa linaweza kubeba bomu zito la nyuklia kwenye kichwa chake.
Yote haya yanaashiria kuwa kombora hilo lina uwezo kwa kusafirisha bomu la nyuklia kwa muda mrefu.
Lilisherehekewa kwa sigara
Kim mwenye furaha anaonekana akicheka kwa furaha wakati kombora hilo
linapaa. Linaaminiwa kuwa kombora la kwanza la Korea Kaskazini lililopaa
mbali zaidi katika kilomita 4,475.
R
ais Uhuru Kenyatta wa Kenya amemuandikia barua Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kupinga kitendo cha
mauaji ya askari wake 14 waliokuwa wakilinda amani nchini Kongo, na
kumpa pole kufuatia msiba huo mkubwa.
Katika barua hiyo, Rais Kenyatta amesema kushambuliwa kwa askari, ambao
walikuwa wakihudumia kwa sababu nzuri ya kuanzisha amani ya kudumu
nchini DRC ilikuwa mbaya, huku akiwapa pole watanzania na ndugu wa
marehemu, na kuwaombea wale waliojeruhiwa waweze kupona haraka.
Uhuru Kenyatta ameendelea kwa kusema kwamba Kenya itaendelea
kushirikiana na watu na serikali ya Tanzania katika kulinda amani ya
Kongo na maeneo ya maziwa makuu, na kuangalia kesho bora ya maeneo hayo.
Rais Kenyatta amesema Kenya inathamini jukumu muhimu lililofanywa na
watunza amani tangu imehusika katika mipango mingi ya kulinda amani.
Kuf
uatia zoezi la serikali la kupanua na kuboresha miundo mbinu
mbalimbali nchini hususan ya barabara k
atika jiji la Dar es Salaam
ambapo imelazimu baadhi ya maeneo kubomolewa ili kupisha zoezi hilo la
upanuzi, Kanisa la Ufufuo na Uzima la Askofu Josephat Gwajima nalo
limekumbwa na kadhia ya kubomolewa.
Kanisa hilo lililoko jirani kabisa na Barabara ya Morogoro ambayo
serikali imepanga kuipanua ili kurahisisha usafiri na kupunguza foleni,
lilitakiwa kubomolewa kutokana na kuwa ndani ya eneo la hifadhi ya
barabara hiyo.
Mchungaji Biyagaza wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko chini ya Askofu
Gwajima, ameeleza kuwa serikali iliwapatia notisi ya siku 30 ili
wabomoe kipande cha jengo la kanisa hilo kilichopo ndani ya eneo la
hifadhi ya barabara.
“Ni kweli tunayo notice ya mwezi mmoja ya kuhakikisha kwamba eneo ambalo
ni hifadhi ya barabara tunaliacha. Na hifadhi ya barabara ni mita 90
kuanzia katikati. Bahati nzuri wale waliokuja kuweka alama zao
walipofika hapa na wahandisi , mafundi na baadhi ya watu wa kanisani
walikuwepo. Basi tukawaambia wapime mita 90 zinapoishia. Kwa hiyo
wakapima mita 90 zilipoishia wakaweka alama, wakasema basi nyie mnaweza
mkabomoa upande huu na upande huu mkauacha kwa ajili ya hifadhi ya
barabara,” alisema Mchungaji Biyagaza.
“Sisi baada ya hapo tukaona tujipange kwa ajili kuachia eneo la barabara
ili shughuli nyingine ambazo ni mpango wa maendeleo ya serikali ziweze
kuendelea na sisi tuweze kuendelea na eneo letu vizuri. Kwa hivyo kile
kipande chote ambacho ni cha barabara na tukaongeza ndani kidogo chote
tumekiondoa. Na hili eneo linalobaki tunapaimarisha ili nyumba ya Bwana
iweze kufanya kazi yake ya kutoa huduma za kiroho,” aliongeza.
Mchungaji Biyagaza alieleza japokuwa eneo la jengo limepungua, eneo
lililobakia linaimarishwa ili kanisa hilo liweze kuendelea kutoa huduma
za kiroho kwa waumini wake.
Nai
robi, Kenya. Mahakama imesema haijapata mawasiliano rasmi kutoka kwa
Muungano wa Nasa kuhusu hatua ya kumuapisha kiongozi wake Raila Odinga.
Msajili Mkuu wa Mahakama, Anne Amadi amesema Mahakama haina taarifa kuhusu sherehe iliyopangwa kufanyika Desemba 12,2017.
“Hatujaarifiwa chochote kuhusu hafla ya kumuapisha Raila Odinga inayopangwa na muungano wa upinzani,” amesema.
Muungano wa Nasa umeanza matayarisho ya hafla ya kumuapisha kiongozi huyo kwa kuunda kamati ya kusimamia shughuli hiyo.
Kuteuliwa kwa kamati hiyo ya watu saba kumefanyika siku chache baada ya
Odinga kutangaza Jumanne iliyopita kuwa ataapishwa kupitia mabunge ya
kaunti, hatua ambayo Serikali imesema ni kinyume cha sheria.
Gazeti moja la Kenya limesema muungano huo umetuma kadi za mwaliko wa
hafla hiyo iliyopangiwa kufanyika Desemba 12,2017 Taifa hilo
litakaposherehekea siku ya uhuru.
Kadi za kidigitali za mwaliko zenye jina la Odinga hazionyeshi mahali hafla hiyo itafanyika.
“Umekaribishwa. Njoo ushuhudie rais wa wananchi Raila Amollo Odinga
akiapishwa tarehe 12 Desemba saa sita mchana. Taarifa kuhusu
itakapoandaliwa hafla hii itatolewa baadaye,” ndivyo inavyosomeka kadi
hiyo ambayo inasisitiza kuwa inaruhusu mtu mmoja pekee kwa kila kadi.
Baraza la Vijana Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamefanya
uteuzi wa viongozi wake ili kuziba mapengo kufuatia baadhi ya viongozi
wao kukihama chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi hivi karibuni.
Katika uteuzi huo, Bavicha wamemteua Patrick Ole Sosopi kuwa Mwenyekiti
mpya wa BAVICHA kwa atakayetumikia nafasi hiyo kwa mwaka mmoja kabla ya
uchaguzi kufanyika mwakani 2018, baada aliyekuwa mwenyekiti wa baraza
hilo, Patrobas Katambi kuhamia CCM.
Marek
ani imetoa wito kwa mataifa mbalimbai kukata uhusiano wake wa
kidiplomasia na kibiashara na Korea Kaskazini, ikiwa ni hatua ya kupinga
majaribio ya makombora ambayo yamekuwa yakifanywa na taifa hilo.
Balozi wa Marekani Nikki Haley, ametoa pendekezo hilo katika mkutano wa
dharura wa baraza la usalama la umoja wa mataifa unaoendelea mjini New
York.
Bi. Haley amesema kuwa Rais wa Marekani amemtaka Rais wa China Xi
Jinping kusitisha biashara ya mafuta ghafi na Korea Kaskazini, kama
sehemu ya kutekeleza hatua ya kuwekewa vikwazo kwa taifa hilo.
Kupitia hatua hii ya kuiwekea vikwazo Korea Kaskazini tunapaswa
kusitisha asilimia tisini ya biashara na Korea Kaskazini pamoja na
asilimia 30 yamafuta yake.
Mwaka 2003, China ilisitisha kupelekea mafuta Korea Kaskazini ,muda
mfupi baadaye taifa hilo likasogea katika meza ya majadiliano.
''Tumefikia hatua ya kuitaka China kuchukua hatua Zaidi katika hili, ni
lazima isitishe kuipatia mafuta Korea Kaskazini," alisema Haley.
Wajumbe wa baraza la usalama la umoja wa mataifa wanakutana mjini Ne
York kujadili hatua ya Korea kaskazini na majaribio ya makombora ya
masafa marefu.

Everton, Wayne Rooney amesema bao alilofunga dhidi ya West Ham United litabaki katika kumbukumbu yake daima.
Rooney alisema hakuwahi kufunga bao maridadi katika maisha yake ya soka
tangu alipoanza kucheza soka Everton, Manchester United na timu ya taifa
ya England.
Nahodha huyo wa zamani wa Man United na England aliiongoza Everton
kupata ushindi mnono wa mabao 4-0 ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa
Goodison Park.
Nguli huyo alifunga mabao matatu ‘hat trick’ kwa mara ya kwanza tangu
aliporejea Everton katika usajili wa majira ya kiangazi kutoka Man
United.
Pia ushindi wa Everton ni ukaribisho wa kocha mpya Sam Allardyce ‘Big
Sam’ aliyetua Goodison Park baada ya kuwa nje ya uwanja muda mrefu tangu
alipojiuzulu kuinoa England.
Rooney alifunga bao la kwanza kwa shuti kali akiwa katikati ya uwanja
dakika ya 66 akimtungua kipa mkongwe Joe Hart umbali wa mita 54.
“Hili ni bao bora zaidi kati ya mabao yangu niliyowahi kufunga. Ni mara
ya kwanza kufunga ‘hat trick’ nikiwa Everton ni hili ndilo bao maridadi
tangu nilipoanza kucheza soka,”alisema Rooney.
Mbali na kufunga mabao hayo, Rooney mwenye miaka 32 alikuwa nahodha
katika mchezo huo na alicheza kwa kiwango bora dakika zote 90.
Pia alidokeza alifunga bao zuri kwa mkwaju wa penalti kwa kuwa anatambua udhaifu wa Hart tangu wakiwa wote timu ya taifa.
“Bao la kwanza lilikuwa muhimu. Nimejifunza sana kupiga penalti nyingi
dhidi ya Joe Hart na najua jinsi ya kumfunga kwa kuwa anajua udhaifu
wake,” alisema Rooney.
Majira ya saa 7:20 leo hii Alhamisi Novemba 30, imetokea hitilafu kwenye
Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha umeme kukatika takriban kwenye
mikoa yote iliyounganishwa kwenye Gridi hiyo.
Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji,
mafundi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO wameanza
kufuatilia kujua chanzo chake hasa ni nini na taarifa Zaidi zitatolewa
kila baada ya muda ili kuufahamisha umma na watuamiaji wa umeme.
Wataalamu wa anga za juu wamegundua sayari isiyo na joto sana na yenye ukubwa unaokaribia sana na wa dunia.
Sayari hiyo inapatikana karibu na mfumo wetu wa Jua
Mandhari katika sayari hiyo ambayo imepewa jina Ross 128 b yanaifanya kuwa pahala pazuri pa kutafuta viumbe au uhai anga za juu.
Sayari hiyo inapatikana umbali wa miaka 11 kwa kasi ya miali ya jua, na
ndiyo sayari ya pili kwa karibu zaidi ambayo ina mazingira
yanayokaribiana na ya dunia.
Sayari ya aina hiyo iliyo karibu zaidi hufahamika kama Proxima b, na
wataalamu wanasema mazingira huko hayaonekani kuwa mazuri sana kiasi cha
kuweza kuwa na viumbe.
Proxima b iligunduliwa 2016, na huzunguka kwenye mzingo ulio kwenye
nyota kwa jina Proxima Centauri, ambayo hufahamika kama "nyota nyekundu
mbilikimo". Nyota hiyo huwaka sana na ina maana kwamba milipuko kwenye
nyota hiyo huenda ikarusha miali nururishi yenye sumu kwenye sayari ya
Proxima b.
Sayari hiyo mpya, Ross 128 b, huzunguka sayari ambayo haitofautiani sana
na Proxima Centauri (pia ni nyota nyekundu mbilikimo), lakini hailipuki
sana.
- Mpango wa Marekani kupeleka watu Mars
- Mpango wa kupeleka watu wakaishi Mars
- Sababu ya chombo cha Ulaya kutoweka Mars
Mmoja wa waliogundua Nicola Astudillo-Defru kutoka kituo cha kutazama
anga za juu chenye makao yake Geneva, Uswizi aliambia BBC kwamba kwa
sababu Proxima Centauri hulipuka na kutoa miali nururishi yenye sumu,
"nafikiri ndio, Ross 128 ni pahala pazuri zaidi pa uhai kunawiri."
"Lakini bado hatufahamu anga ya Ross 128 b iko vipi. Kwa kutegemea vitu
vilivyo kwenye anga yake na uwezo wa mawingu kuakisi mwanga, huenda
kukawa na maji ambayo yanaweza kufanikisha uhai kama hapa duniani, au
iwe sayari kama vile Zuhura ambayo haiwezi kufanikisha uhai."
Sayari hiyo mpya iligunduliwa na darubini yenye uwezo mkubwa kwa jina
Harps iliyopo katika kituo cha kufuatilia anga za juu cha La Silla
nchini Chile.
Ingawa kwa sasa sayari hiyo ipo miaka 11 kwa kasi ya miali ya jua kutoka
kwenye dunia, nyota asili Ross 128 inasonga kuelekea kwa dunia na
huenda ikaipita Proxima Centauri na kuwa mfumo wa nyota ulio karibu na
dunia zaidi katika kipindi cha miaka 79,000.
- Proxima Centauri ni 'nyota nyekundu mbilikimo'; ni ndogo na pia haina joto sana kama Jua
- Inakaribia zaidi lakini kuna uwezekano ikawa imeunganishwa kwa mvuto na Alpha Centauri A & B
- Kwa mtu anayetumia jicho lake kutazama juu angani Alpha Centauri A & B huonekana kama nyota moja
- Sirius A ndiyo nyota inayong'aa zaidi na inayotambulika kwa urahisi zaidi angani usiku
- Jupiter ndiyo sayari kubwa zaidi mfumo wetu wa Jua. Iwapo ingelikuwa na uzito mara 80 zaidi ya sasa, basi ingegeuka na kuwa jua
- Mambo muhimu kuhusu sayari ya Mars
- Mmarekani wa kwanza kuizunguka dunia afariki
- Japan yatuma mtambo wa kufagia anga za juu

Kenya. Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatarajiwa kutangaza matokeo
ya uchaguzi wa marudio kwa kura ya utais uliofanyika Oktoba 26 na
kutangaza ikiwa itaandaa uchaguzi katika majimbo 25 ambako uliahirishwa.
Makamu wa Rais wa tume hiyo, IEBC, Consolata Nkatha alisema jana jioni
kwamba walikuwa wamepokea matokeo kutoka majimbo sita kati ya saba
yaliyokuwa yamesalia na kwamba kufikia Jumatatu asubuhi matokeo yote
yatakuwa yamejumlishwa.
“Tumepokea matokeo kutoka majimbo sita sasa na tutakuwa katika nafasi ya
kutangaza matokeo ya mwisho kesho (leo) asubuhi. Tutafanya kazi usiku
kucha kuhakikisha uhakiki na ujumlishaji unakamilika. Pia tutatangaza
ikiwa tutaendesha uchaguzi katika majimbo 25 ambako uliahirishwa au la,”
alisema Nkatha.
Majimbo hayo yaki kwenye kaunti ambazo tume iliahirisha uchaguzi ambazo ni Kisumu, Migori, Siaya na Homa Bay.
Mawasiliano na IEBC yamekuwa haba lakini inafahamika kwamba makamishna
wa tume walifanya kikao cha saa kadhaa na wanasheria wao juzi kufikiria
kama wajaribu kuitisha uchaguzi katika majimbo 25.
Jana jioni Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati alisema tume yake
ilikuwa imehakiki matokeo ya majimbo 259 kati ya 265, yakiwemo ya nchi
za nje.
Kutoka katika majimbo hayo, Chebukati alisema watu 7,447,014
walijitokeza kupiga kura sawa na asilimia 43.04. Matokeo yaliyokuwa
yakitangazwa moja kwa moja kutoka jengo la Bomas of Kenya Rais Kenyatta
alijikusanyia kura 7,393,405 sawa na asilimia 98.3 ya kura halali.
Kamp
uni ya Udalali ya Yono imesema itapiga mnada kwa mara
ya pili nyumba za kifahari za mfanyabiashara Saidi Lugumi baada ya ule
wa kwanza uliofanyika Septemba 7 kukwama.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo, Scholastica Kevela amewaeleza
waandishi wa habari leo Jumatatu kuwa lengo la mnada huo ni kufidia Sh
14 bilioni anazodaiwa Lugumi.
"Sio kweli nyumba hizi zimedoda ila thamani halisi katika mnada wa
kwanza haukufikiwa na ndio maana tunarudia tena Novemba 9," amesema
Kevela.
Amesema baada ya mnada wa awali kukwama walirudi kujipanga na Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) imewapa maelekezo mengine ikiwamo thamani ya
nyumba hizo.
Wateja hawajajitokeza kununua mali za Lugumi
"Wale wanaotaka majumba haya ya Lugumi waje siku hiyo na tayari Serikali
kupitia TRA imetupa maelekezo mapya hasa thamani ya majumba hayo
imepanda kuliko ya awali ilivyokuwa," ameongeza
Mku
rugenzi huyo amesema nyumba hizo zitakazopigwa mnada ziko Mbweni JKT nyumba mbili na nyumba moja ipo Upanga.