Tuesday 28 February 2017

Jinsi ya kuandika barua ya kuomba kazi


Je ulishawahi kuandika barua ya maombi ya kazi na kutuma kwa waajiri wengi na wote au wengi ya hao hawakukujibu hata kama unajua unazo sifa za hiyo kazi?

Jibu la hapo ni rahisi

hapo Uandishi wa barua zako una shida tu..


Barua ya maombi ya kazi iwe na sura hii

  1. Wewe nani
  2. Umezipataje hizo taarifa za nafasi za kazi
  3. Unafikiri wewe utapeleka kitu gani nzuri ambayo wengine walioomba hiyo nafasi hawana ila wewe unayo/unazo (Usieleze habari za degree, diploma au vyeti vyako kwani na wenzako wanazo, pia usieleze juu ya uzoefu wako wa kazi kwani na wao wanazo tena kukuzidi)
  4. Eleza utayari wako wa usaili na kuanza kazi
  5. Acha mawasiliano yako ya haraka kama simu ya kiganjani na barua pepe (usiache mawasiliano ya kupitia kwa watu wengine kama shangazi mjomba, mama, baba na marafiki au jirani)
  6. Eleza kwamba umeambatanisha wasifu wako

No comments:

Post a Comment