Tuesday 31 May 2016

Magazeti ya leo Jumatano Juni 1 2016

 



Waamuzi wanne kutoka Gabon kuchezesha mechi ya Taifa stars na Misri


Waamuzi wanne kutoka Gabon, ndio watakochezesha mchezo wa kimataifa kati ya Taifa Stars ya Tanzania na Mapharao wa Misri utakaofanyika Jumamosi Juni 4, 2016 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mchezo huo utakaoanza saa 10.00 jioni ni wa kutafuta nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika Gabon ambako mwamuzi wa kati atakuwa ni Meye Bastrel atakayesaidiwa na Mihundou Ganther na Vinga Theophile wakati Mwamuzi wa akiba (mezani) atakuwa Otogo Eric.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli azinduanembo mpya ya Tuzo za Rais kwa Wazalishaji bora wa Viwanda

MSRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizindua nembo mpya ya Tuzo za Rais kwa Wazalishaji bora wa Viwanda  PMAYA The President’s Manufacure of the Year  pamoja na Mwenyekiti wa Wenyeviwanda Tanzania CTI Dkt. Samwel Nyantahe katika Ukumbi wa Serena Jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU / HASSAN SILAYO-MAELEZO

Katibu mkuu wa wizara ya afya azindua baraza la wafanyakazi muhimbili

MP1Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Maendeleo  Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Mpoki Ulisubisya akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) LEO. Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamedi Janabi, Katibu wa baraza hilo, Dk Kissa Mwambene. Kushoto ni Mwenyekiti wa baraza hilo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MNH, Makwaia Makani.PICHA NA JOHN STEPHEN, HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI (MNH)

Wakazi Dar waanza kunufaika naTeknolojia ya moovn kwa Usafiri



 
Suala la ukuaj iwa teknolojia ulimwenguni limeendelea kuthibitisha kuwa ni suala m tambuka kutokana na kukua kwake kwa kasi ya ajabuikiwa ni pamoja na kugusa takribani sekta zote katika ulimwengu wa leo.