Monday 31 October 2016

YALIOJIRI LEO MAGAZETINI LEO JUMANNE 01 NOV 2016

 

Kidato cha nne kuanza mitihani kesho

Jumla ya watahiniwa 408,442 wa kidato cha nne wanatarajia kuanza mitihani ya kidato cha nne itakayoanza kesho, ikiwa ni idadi pungufu ya waliofanya mtihani huo mwaka jana.Tokeo la picha la KIDATO CHA NNE MTIHANI
Akizungumza na wanahabari leo Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania Dk Charles Msonde amesema mwaka jana kulikuwa na watahiniwa  448,382 waliofanya mitihani huo.
Dk Msonde amesema maandalizi yote ya mitihani hiyo itakayomalizika Novemba 18, mwaka huu yameshakamilika.
Amewataka wanafunzi, walimu na wasimamizi kujiepusha na udanganyifu wa mitihani kwani baraza hilo halitasita kuchukua hatua za kisheria, ikiwamo kuwafutia matokeo.


Kifo cha muuza samaki chazua maandamano

Maandamano baada ya muuza samaki kukanyagwa na lori hadi kufa nchini Morocco


Maelfu wa raia wa Morocco walifanya maandamano wikendi hii katika miji kadhaa baada ya muuza samaki mmoja kukanyagwa hadi kufa na lori la kubeba takataka alipokuwa akijaribu kuchukua samaki wake ambao alikuwa amepokonywa na maafisa wa polisi.
Kifo cha Maouhcine Fikri katika mji wa kaskazini wa Al-Houciema siku ya Ijumaa kilizua hasira kali miongoni mwa raia katika mitandao ya kijamii.
Kifo chake kinafananishwa na kile cha muuza matunda wa Tunisia mwaka 2010 ambacho kilisababisha maandamano makubwa.
Mfalme wa Morocco King Mohammed VI amewaagiza maafisa wake kutembelea familia ya Fikri.
Wizara ya maswala ya ndani pamoja na ile ya Haki zimeahidi kuanzisha uchunguzi.

Malinzi ameteuliwa CAF

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika, Issa Hayatou ameteua Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kuwa miongoni mwa wajumbe 11 wa Kamati maalumu ya mageuzi ya muundo wa CAF itakayokuwa na jukumu la kufanya mabadiliko mapya ya shirikisho, imefahamika.
Tokeo la picha la gamaly malinzi
 Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, katika Kamati hiyo ikayoongozwa na Rais Issa Hayatou mwenyewe, Malinzi ameteuliwa katika Kamati hiyo iliyotangazwa leo Oktoba 30, 2016 kutoka ukanda wa Afrika Mashariki.

Rais Dkt John Pombe Magufuli alipowasili Ikulu ya Kenya, Jijini Nairobi

key1
Rais Dkt John Pombe Magufuli, akilakiwa na Mwenyeji wake, Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta alipokaribishwa Ikulu, Nairobi nchini Kenya leo. Rais Magufuli yupo nchini Kenya kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
key2
Rais Dkt John Pombe Magufuli (kulia) akiwa na Mwenyeji wake, Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta wakipokea salamu za kijeshi, katika viwanja vya Ikulu ya Kenya, Jijini Nairobi leo.
key3
Rais Dkt John Pombe Magufuli akikagua gwaride la Jeshi la Kenya, alipowasili Ikulu jijini Nairobi leo.
key4 key5
Rais Dkt John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mwenyeji wake, Rais wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta, alipowasili Ikulu ya Kenya, Jijini Nairobi leo.
key6
Rais Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Naibu Rais wa Kenya, Mh. Willam Ruto.

Wahariri waukubali Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari

nap7
Anitha Jonas – MAELEZO
Wahariri wa vyombo vya habari wameukubali Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari baada ya kuusoma kwa umakini nakuona namna gani utasaidia kuinua tasnia ya habari nchini.
Hayo yamebainishwa katika mahojiano maalum  kwa njia ya simu na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari akiwemo Mhariri wa Televisheni ya TV 1, Bw.Said Mwishehe huku akieleza faida za Muswada huo pamoja na kutoa maoni yake kwa kuiomba serikali kuangalia vizuri baadhi ya vipengele na kama kipengele cha 54 na 55 katika Sehemu ya Nane ili kuvipunguzia makali na kuondoa suala la kuonekana kubana uhuru wa vyombo vya habari.
“Kuna umuhimu kwa wadau wa habari kuunga mkono muswada huu badala ya kuupinga kwani una mambo mazuri yatakayosaidia kuboresha tasnia hii ya habari na kuipa heshima kama taaluma nyingine badala ya kuonekana kuwa waandishi wa habari ni watu wababaishaji tu na wasiyo na taaluma iliyo imara,”alisema Bw.Mwishehe.
Pamoja na hayo Mhariri huyo aliendelea kusema amefurahishwa na muswada kwa namna unavyojali maslahi ya waandishi wa habari pale unapoeleza kuwa wamiliki wa vyombo vya habari watahitajika kuwakatia bima waandishi wa habari  kwa hiyo itakuwa jambo la busara kwani waandishi wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu yanayohatarisha afya zao pasipo kuwa na bima inayomlinda akiwa kazini.
Aidha, Bw.Mwishehe aliwasihi wadau wa sekta ya habari kutuma maoni yao kwa vile vipengele vya muswada vinavyoonyesha kutokuwa sawa na pia ameiomba serikali kuwa na utayari wa kuyapokea maoni hayo  kwa ajjili ya kuboresha muswada huo na kuufanya bora na wenye tija katika tasnia ya habari nchini.
Naye Mhariri wa Gazeti la Mtanzania, Bw.Revocatus Makaranga alisema Muswada huo wa habari una mambo mazuri yanayoipeleka tasnia mahali pazuri ikiwemo suala la waandishi wa habari kuhitajika kujiendeleza katika elimu ya juu  na hii itasaidia kukuza upeo wa mwandishi na kumfanya awe na uwezo mkubwa na kufanya kazi kwa kujiamini kama ilivyo kwa waandishi wa nchi zilizoendelea.
Bw.Makaranga aliongeza kusema muswada una vipengele ambavyo ipo haja ya serikali kuvifanyia marekebisho ikiwemo suala la adhabu inayotolewa kwa waandishi ya kuwafungia pale wanapokuwa wamekosea.
Pia mhariri huyo ameipongeza serikali kwa muswada huo ambao utaleta picha mpya ya kimaendeleo katika tasnia ya habari ikiwemo suala la  kuanzishwa kwa Mfuko wa mafunzo kwa wanahabari nchini ambapo utasaidia kutoa elimu kwa waandishi mara kwa mara na kuwajengea uwezo wa utendaji.
Kwa upande wake, Mhariri Mkuu wa kituo cha Redio Efm, Bi Scolastika Mazula alisema katika muswada huo wa habari yapo mambo mazuri yenye tija katika sekta ya habari kama suala la kuanzishwa kwa Mfuko wa mafunzo kwa wanahabari ni jambo jema sana kwani utasaidia kutoa fursa za waandishi kujiendeleza kimasomo na kuifanya fani ya habari kuwa na wasomi zaidi tofauti na inavyoonekana kwa sasa.
“Suala la elimu kwa waandishi ni bora liwekwe wazi kisheria kwani tansnia hii ya habari inahitajika kuheshimika kama ilivyo tansia nyingine badala ya kuonekana wababaishaji”, alisema Mazula.
Pamoja na hayo Bi. Mazula aliendelea kutoa maoni yake kuhusu Muswada kwa kusema kuwa  suala la kuanzishwa kwa bodi ni zuri ila ingekuwa vyema kama bodi hiyo itakuwa na asilimia kubwa ya wadau wa habari na ijitegemee na Waziri mwenye dhamana ya habari na Mwanasheria Mkuu wasiwe na mamlaka sana katika bodi hiyo.
Pamoja na hayo naye Katibu wa Jukwaa la Wahariri, Bw.Neville Meena alisema kwa sasa wanajukwaa wameshatoa maoni yao kuhusu muswada huo na watayawasilisha kwa ajili ya kusaidia kuboresha muswada huo na kuufanya uwe na tija na manufaa zaidi katika kuendeleza tasnia ya habari nchini.

Alichokisema Jokate kuhusu shindano la Miss Tanzania

Kwa miaka mingi mfululizo, haijawa rahisi kwa shindano la Miss Tanzania kumalizika bila malalamiko, lawama au kashfa. Awamu hii pia, yamekuwepo malalamiko kadhaa kuhusiana na maandalizi yake na jinsi shindano lilivyofanyika huku kukiwepo kasoro kadhaa.Tokeo la picha la jokate

Lakini mrembo aliyewahi kushiriki shindano hilo miaka ya nyuma, Jokate Mwegelo, ameyatetea mashindano hayo akisema kuwa waandaji wamefanya kazi nzuri na wanastahili pongezi. Haya ni maelezo yake aliyoandika kupitia Twitter.
Fainali za mashindano ya Miss Tanzania zitafanyika Mwanza kwa miaka mitatu zaidi. Brilliant idea. I support this move. Open up mikoa zaidi. Ukiacha mapungufu fainali za Miss Tz ni shindano pekee la urembo ambalo huwezi kusikia mshindi amedhulumiwa zawadi yake au show ikapwaya.

Show ya Mwanza ilifanyika nje viingilio 100k,50k,20k na ilijaa watu licha ya mapungufu ya production. Nilikuwepo so najua ninachoongea.
Wadada wawili walipewa jukumu la kusimamia fainali hizi. Hao wadada wanakaa mkoani Mwanza. Nawapongeza kwa kufanikisha licha ya changamoto.

Kamati just needs to perfect the craft of moulding contestants to be competitive and of coarse giving us the ideal winner who will thrive. Ni rahisi sana kuchambua na kukosoa mashindano haya humu ila ukilinganisha na mashindano mengine ya urembo nchini angalau wanafanya vizuri.

Wanafanya vizuri kufikia warembo wengi kupitia mikoa mbalimbali na sio DSM tu au mikoa ya karibu. Vipaji vinatoka sehemu mbalimbali.
We need a sole company to deal na production. Creative themes and execution. Sio tu kwenye show za urembo na kwenye matamasha mengine.
Mshindi wa Miss Tanzania mwaka huu ni Diana Edward.

Jinsi mchora Katuni wa Kenya alivyomchora Rais John Magufuli




View image on Twitter
View image on Twitter


Gado @iGaddo

Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa mwaka 2016 utanufaisha waandishi wa habari?

5b
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma
Baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano Serikalini (GCU) wamemesema Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari wa mwaka 2016 ni muhimu kwa taifa na unalenga kuleta tija kwa taifa zima.
Muswada huo unalenga kuwanufaisha waandishi wa habari, wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na wananchi wa kawaida nchini.
Wakipongea kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hii, Wakuu hao leo wa wamesema muswada huo una manufaa na fursa nyingi kwa taifa na wananchi tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Zawadi Msalla amesema kuwa sheria hiyo inatoa mwanya mkubwa kwa tasnia ya habari nchini kuwa ni miongoni mwa taaluma inayoheshimika kama kada nyingine kwa kuwa na chombo kitakachowasimamia wanahabari hao.
“Uanzishwaji wa Baraza Huru la Habari ni moja ya takwa lililowekwa na Sera ya habari na Utangazaji ya mwaka 2003 iliyoitaka Serikali kuanzisha chombo huru kitakachosimamia masuala ya habari hivyo,muswada huu utakapokuwa sheria utakuwa umetekeleza agizo la Serikali la kuanzisha chombo huru kitakachosimamia masuala ya habari”, alisema Msalla.
Zawadi ameongeza kuwa kuanzishwa kwa Sheria hiyo itasaidia kuleta uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari kufanya kazi yao ipasavyo kwani kwa sasa mmiliki wa chombo cha habari asiporidhishwa na maamuzi ya kutopewa leseni anakata rufaa kwa Waziri mwenye dhamana na asiporidhishwa na maamuzi yaliyotolewa na Waziri huyo amepewa fursa ya kwenda mahakamani.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Morogoro, Andrew Chimesela amepongeza juhudi za Serikali kwa kazi ya kuandaa Muswada ambao utasaidia kuwa na Sheria itawanufaisha wadau wote wa habari nchini.
Baada ya kupitishwa Muswada na Bunge, kuidhinishwa na kusainiwa na Rais hatimaye kuwa Sheria, Chimesela kuwa ziandaliwe kanuni ambazo zinaendana na wakati huu wa sasa tofauti na ilivyokuwa wakati wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.
Aidha, amekubaliana na uamuzi wa kuundwa kwa Bodi ya Ithibati kwa sababu bodi hiyo itakua na kazi ya kuangalia maslahi ya wanatasnia pamoja na kudhibiti nidhamu na maadili ambayo yanapaswa kwenda sambamba na tasnia habari ili iweze kuheshimika kama taaluma nyingine za Wanasheria, wahasibu na sekta ya afya.
Naye Mkuu wa Kitengo cha GCU kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, Englibert Kayombo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), wameunga mkono uanzishwaji wa Bodi ya Ithibati kwasababu itasaidia kutambua wanahabari wenye taaluma halali kwenye sekta ya habari nchini.
 “Binafsi naunga mkono jitihada zinazofanywa na Wizara za kurasimisha tasnia hii ya habari ili iwe na hadhi sawa na tasnia zingine, ni vyema kuratibu kazi za waandishi wa habari ili waweze kutoa habari zenye kujenga taifa letu imara lenye mfumo mzuri wa kazi za kihabari”, alisema Kayombo.
Baada ya kuanzishwa na kufanya kazi Sheria hiyo, ni dhahiri itavifanya vyombo vya habari nchini kuajiri watu wenye taaluma ya habari tofauti na hali ilivyosasa na wananchi watarajie kupata habari za ukweli na uhakika.

Kitabu cha Timiza malengo yako chazinduliwa



Imeelezwa kwamba watu wengi wamekuwa wakishindwa kufanikiwa kimaisha kutokana na kutokuwa na mipango ya kimaisha ambayo wanaweza kuifanyia kazi ili waweze kufanikiwa kama jinsi ilivyo kwa baadhi ya watu ambao wanaonekana kuwa na mafanikio.
Hayo yamesemwa na Mwandishi wa kitabu cha TIMIZA MALENGO YAKO, Joel Nanauka wakati wa uzinduzi wa kitabu hcho ambacho kinnaelezea mbinu 60 ambazo zinatumiwa na watu waliofanikiwa kimaisha kuweza kufikia alengo ambayo wamejiwekeakatika maisha yao.
Nanauka alisema watu wengi wamekuwa wakitamani kufanikiwa lakini wamekuwa hawajui ni hatua gani za kupitia na kufanikiwa na baada ya yeye kufanya utafiti wa muda mrefu kwa watu mbalimbali duniani waliofanikiwa na wasiofanikiwa, ameweza kupata mbinu 60 ambazo ndiyo zinatofautisha watu wa matabaka hayo mawili
Alisema kupitia kitabu hicho msmaji ataweza kufahamu ni mambo gani anatakiwa kufanya na yapi hatakiwi kufanya ili kufanikiwa kama wengine kwa kuzingatia mbinu ambazo pia zimekuwa zikitumiwa na watu waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali kama biashara, michezo, sanaa na hata uongozi.
“Watu wengi wanapenda kufanikiwa lakini kama huna malengo huwezi kufanikiwa, watu wengi hawajui wanatumia njia gani ili kufanikiwa na hadi wanaondoka duniani wanaondoka na ndoto walizokuwa nazo, ndoto ambazo zilitakiwa kubaki zikifanya kazi duniani,
“Sababu ya kuandika kitabu hiki ilianza nipotaka kujua utofauti wa waliofanikiwa na wasiofanikiwa, aliyefanikiwa kwa aliye Marekani na Tanzania na asiefanikiwa aliye Tanzania a Mareani, nilianza kusoa kwanini wengine wanaweza kufanikiwa katikati ya mamilioni ya watu na baada ya kupata mawazo ya jumla ndiyo nikapata mbinu 60 ambazo zipo katika kitabu cha TIMIZA AHADI YAKO,” alisema Nanauka.
Nanauka alisema kitabu hicho kitakuwa kikuzwa kwa Tsh. 10,000 na anaamini kila ambaye ataweza kusoma kitabu hicho ataweza kupata kitu kipya ambacho kitaweza kumsadiakufanikiwa na kufika ndoto abazo anatamani kuzifikia.
“Matumaini yangu kila atakaesoma kitabu hiki maisha yake yabadilike kutokana na mambo ambayo atayasoma na kila mtu hatajutia kusoma kitabu hiki, nimekiandaa kwa muda mrefu kwa kufanya tafiti nyingi na kuweka mifano ambayo naamini itabadili maisha ya watu wengi wataokisoma,” alisema Nanauka.

Ziara ya Rais Dkt John Pombe Magufuli nchini Kenya

nair1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisindikizwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016
nair2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Naibu Balozi wa  Kenya nchini Mhe Boniface Muhia katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili  leo Oktoba 31, 2016
nair3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea saluti toka kwa Inspekta jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016
nair4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiagana  na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa  tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016
nair5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipungia wakati akipanda ndege kwenye  Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016
nair6
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi,  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na viongozi wengine wakipunga mikono kumuaga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati akianza  safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016

Rambo alivyomuibukia Pacquiao Gym

Bondia Mfilipino, Manny Pacquiao akiwa na gwiji wa filamu za kibabe Marekani, Sylvester Stallone maarufu kama Rambo au 'Bondia Rocky' mjini Las Vegas, Marekani. Pacquiao yupo katika maandilizi ya mwisho na pambano na Jessie Vargas Novemba 5 mjini Las Vegas uzito wa Welter na mwishoni mwa wiki alitembelewa na Rambo katika gym ya Wild Card mjini Hollywood

Alikiba, Diamond, Ommy wakutana kwenye kipengele kimoja Tuzo za ASFA 2016

Waandaaji wa tuzo za mitindo za Uganda, Abryanz Style and Fashion Awards wametangaza majina ya mastaa watakaowania vipengele mbalimbali.
Wakali wa muziki wa Afrika mashariki, Diamond, Alikiba, Ommy Dimpoz na Sauti sol wamekutana kwenye kipengele kimoja cha ‘Most stylish artiste’ Huku Juma Jux, Nedy Music na Idris Sultan wakikutana kwenye ‘Male Most dressed Celebrity
Jokate Mwegelo, Wema Sepatu na Wolper Stylish watachuana na Vera Sidika, Huddah Monroe na Kate Peyton kweney ‘Female Most dressed Celebrity’

Hii ndio orodha kamili ya Nominees,
FASHION DESIGNER OF THE YEAR

Martin Kadinda (Tanzania)

Sheria Ngowi (Tanzania)

Bobbins & Seif (Uganda)

Moise Turahirwa (Rwanda)

Makeke International (Tanzania)

Jamila Vera Swai (Tanzania)
MOST STYLISH ARTISTE

Males

Sauti Sol (Kenya)

Ali Kiba (Tanzania)

Diamond Platnumz (Tanzania)

Ommy Dimpoz (Tanzania)

Females

Vanessa Mdee (Tanzania)

Avril (Kenya)

Vicotria Kimani (Kenya)

Aika Navy kenzo(Tanzania)
BEST DRESSED CELEBRITY

Males

Nick Mutuma(Kenya)

Juma Jux(Tanzania)

Nedy Music(Tanzania)

Idris Sultan(Tanzania)

Georgie Ndirangu(Rwanda)

Jamal Gaddafi(Kenya)

Females

Jokate Mwegelo(Tanzania)

Vera Sidika(Kenya)

Huddah Monroe(Kenya)

Wema Sepatu(Tanzania)

Kate Peyton (Rwanda)

Wolper Stylish(Tanzania)
MOST FASHIONABLE MUSIC VIDEO

Mamacita – Tinie Tempah ft. Wizkid

Colours of Africa – Diamond Platnumz ft. Mafikizolo

Soft Work – Falz the bahd Guy

Vanessa Mdee – Niroge

No Kissing – Patoranking ft. Sakordie

Aje – Ali Kiba

If I start to talk – Tiwa Savage ft. Dr. SID

Tulale Fofofo – Micasa FT. Sauti Sol

Kontrol – Maleek Berry.
MOST STYLISH COUPLE

Barbie and Bobi Wine (Uganda)

Bonang Matheba & AKA (South Africa)

Annabel Onyango and Marek Fuchs (Kenya)

Zari Tlale and Diamond Platnumz(Tanzania)

Mr & Mrs Ayo Makun(Nigeria)

Elikem and Pokello(Zimbabwe)
CROSSING BOARDERS WITH FASHION

Jidenna

Ugo Mozie

Lupita Nyongo

LOLU ESQ
BEST DRESSED MEDIA PERSONALITY/ENTERTAINERS OF THE YEAR(AFRICA)

Males

Uti Nwachukwu

Falz the bahd Guy

Idris Sultan

Friday James

Ebuka Obi

Derenel Edun

Georgie Ndirangu(Rwanda)

Females

Vimbai Mutinhri

Toke Makinwa

Stephanie Coker

Bolanle Olukanni

Berla Mundi

Bonang Matheba(SouthAfrica)

Tracy Wanjiru(Kenya)

Bondia Thomas Mashali auwawa, mwili wake waokotwa vichakani Dar

Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali, hatunaye.Tokeo la picha la thomasi mashali

Yassin Abdallah maarufu kama Ustaadhi, mmoja wa viongozi wakongwe wa mchezo wa ngumi amethibitisha na kusema mwili wa Mashali upo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
"Tumethibitishiwa hizo taarifa za majonzi kabisa, mwili upo Muhimbili na msiba upo kwao Tandale," alisema Ustaadhi.

Sunday 30 October 2016

YALIOJIRI MAGAZETINI LEO JUMATATU OCT 31 2016

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi0HTHl6Q0s9Bvcedh4nCTXQ9UrOdZAJWgsv51kvuhoe0JIq7DFF33GKdB2LfwpTFCvWxzTK2b_DyoowU6AljumCEQssFinZxDswc8uq7F7xZMCqyHRj_d624Wxm1xYLa_tgH2SFtmEvmfC/s1600/1.PNG

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Taasisi ya Twaweza wameunga mkono Mswada wa Huduma za Habari ya mwaka 2016

twaweza
Na Mwandishi Wetu Dodoma
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Taasisi ya Twaweza wamesema kuwa Muswaada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 ni bora kuliko Miswada iliyowahi kuwasilishwa nchini.
Haya yamebainishwa katika maoni yao waliyowasilisha kwenye Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii leo Mjini Dodoma katika juhudi za kuufanya Muswada huo kuwa bora zaidi na kupelekea kuapa sheria yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
TLS na Twaweza wamebainisha kuwa Muswada huu ni bora zaidi  na utasaidia kuwajengea wadau wa habari nchini heshima kwa kutoa huduma bora kupitia  vyombo vya habari kwa kuzingatia taaluma ya Habari waliyonayo hatua ambayo inautofautisha na muswada uliowasilishwa Bungeni mwaka 2015.
Kwa mujibu wa maoni yalitolewa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) yamesema Muswada huo mzuri zaidi na unaifuta Sheria ya  Magazeti ya Mwaka 1976 hatua ambayo wameipongeza Serikali kwani Sheria hiyo  iliwahi kuainishwa kuwa miongoni mwa Sheria 40 na kusadikiwa na Tume ya Jaji Francis Nyalali kama Sheria kandamizi.
Kwa upande wa Taasisi ya Twaweza wao wamesema kuwa Muswada huo utaanzisha utaratibu ambao utawatambua waandishi wa habari kwa kuanzisha Baraza Huru la Habari pamoja na Bodi ya Ithibati ya wanahabari amabazo zitasimamia kanuni na maadili ya wanahabari, kusimamia viwango na mienendo ya kitaaluma na kuendeleza vigezo bora vya maadili na nidhamu miongoni mwa wanahabari.
Kwa mantiki hiyo, maoni yaliyowasilishwa kwa Kamati hiyo yanaendana na Muswada ambao unasisitiza  kuanzisha mahusiano na taasisi nyingine za taaluma ya habari ndani na nje ya nchi ili wadau wa habari waweze kubadilishana mawazo na kuwa na namna bora ya kuhabarisha umma katika masuala mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Aidha, Baraza huru la habari kutakuwa suluhisho katika kusimamia na kusikiliza malalamiko ambayo yatawasilishwa kwenye baraza hilo kulingana na kanuni za maadili ya taaluma ya habari hatimaye kuifanya tasnia ya habari kuheshimika tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali.
Uboreshwaji wa Muswada huo unalenga kuleta Sheria itakayosimamia Tasnia ya Habari ili iweze kuendana na wakati pamoja na Sheria za kimataifa na namna bora ya kuwahudumia wananchi.

Jenerali Mstaafu George Marwa Waitara Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).

waitara-anatembea
Rais wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 30 Oktoba, 2016 amemteua Jenerali Mstaafu George Marwa Waitara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania  (TANAPA).
Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi huo umeanza tarehe 29 Oktoba, 2016.
Jenerali Mstaafu George Marwa Waitara ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu.
WAKATI HUO HUO,Rais Dkt. Magufuli amemteua Dkt. Eligy Mussa Shirima kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI)
Uteuzi wa Dkt.Shirima umeanza tarehe 29 Oktoba 2016.
Kabla ya uteuzi huu Dkt. Eligy Mussa Shirima alikuwa Mtafiti Mkuu na Msimamizi wa Utafiti wa Nyama ya Ng’ombe Makao Makuu ya TALIRI. 
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
30 Oktoba, 2016

Italia yagongwa tena na tetemeko la ardhi

Tetemeko lingine baya la ardhi, limegonga maeneo ya katikati mwa Italia, mahali ambapo watu 300 waliuwawa mwezi Agosti mwaka huu.
Taarifa za awali zinasema kuwa uzito wa tetemeko hilo limefikia 6.6 katika vipimo vya Richa.
Majumba kadhaa yameporomoka, likiwemo kanisa la St Benedict mjini Norcia.
Hakuna taarifa zozote kuwahusu wahasiriwa au maafa.
Kitovu cha tetemeko hilo lilikuwa kusini mashariki mwa mji wa Perushia.
Uzito wa tetemeko hilo umesikika hadi mjini Roma, umbali wa kilomita 150.

Pluijm Kwenye Benchi La Yanga Leo Tena

Baada ya kurejea, Kocha Hand van der Pluijm amesema hata mechi dhidi ya Mbao FC leo, pia itakuwa ngumu kwao.
Pluijm raia wa Uholanzi aliamua kuandika barua kuachia ngazi, lakini uongozi wa Yanga ukamuangukia na kumfanya abadili uamuzi wake huo.
Leo Yanga inapambana na Mbao FC kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mechi ya kwanza baada ya Pluijm kurejea.
"Najua itakuwa mechi ngumu, timu zote zinajiandaa na inakuwa faraja kwao kushinda dhidi ya Yanga ambao ni mabingwa.
"Wachezaji wangu wako tayari na wanajua sisi ni kina nani na wanaocheza na sisi wanataka nini," alisema.
Yanga imeonyesha kurejea katika kiwango chake kwa kushinda mabao mengi katika kila mechi, ikianza na kuitandika Kagera Sugar mabao 6-2 na JKT Ruvu mabao 4-0.

Sumaye adai Amepata taarifa ya Kutimuliwa Nyumbani kwake pia

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye amesema kuwa baada ya kutangazwa mchakato wa kunyang’anywa shamba lake la Mwabwepande, amepata taarifa ya kutaka kuondolewa anapoishi pia.
Sumaye ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache baada ya Waziri Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kueleza kuhusu kuanza rasmi kwa mchakato wa kumnyang’anya mwanasiasa huyo shamba la Mwabwepande kwa madai ya kutoliendeleza kwa muda mrefu.
“Hapa ninapoishi naambiwa kuna maelekezo yametoka juu kuwa sijapaendeleza. Sasa kama sijapaendeleza mbona ninaishi hapahapa,”
Aidha Sumaye amesema kuwa ingawa alimsikia Waziri Lukuvi akieleza kuwa tayari wameshampa notisi ya siku 90 kuhusu kunyang’anywa shamba lake la Mwambwepande, hadi jana hajaipata notisi hiyo licha ya kufanya jitihada za kuifuatilia.

Alisema kuwa anashangazwa na uamuzi huo wa Waziri kwani kesi inayolihusu shamba hilo bado inaendelea mahakamani kutokana na uvamizi wa wananchi na kwamba Mahakama imezitaka pande zote mbili kutofanya chochote kwenye ardhi hiyo.
Mwanasiasa huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chadema alisema kuwa anachokifahamu ni kwamba alipokea notisi ya kuondolewa katika shamba lake la Mvomelo kwa madai ya kushindwa kuliendeleza kwa muda mrefu.
“Ninachokijua ninaandamwa kisiasa. Shamba langu la Mvumelo naambiwa sijaliendeleza. Kwenye hilo shamba nimejenga nyumba ya kuishi, ghala, kuna trekta na vifaa vingine. Ninalima mazao na nimefuga zaidi ya ng’ombe 200, nina kondoo 300 na nimechimba visima viwili vya maji halafu serikali inasema sijaliendeleza,” alisema Sumaye.
Alisisitiza kuwa ingawa anaamini anaandamwa kisiasa kwa kunyang’anywa mashamba yake, hatarejea CCM hata akinyang’anywa mashamba yote aliyoanayo.
Sumaye alihama CCM mwaka jana, miezi michache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu na kujiunga na harakati za kumpigia kampeni mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa. Baada ya uchaguzi huo alitangaza kujiunga rasmi na Chadema.

Samatta Atokea Benchi Genk Ikiua 2-1 Ubelgiji

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amecheza benchi timu yake, KRC Genk ikishinda 2-1 dhidi ya Westerlo katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji, Uwanja wa Laminus Arena.
Kiungo Mspaniola, Alejandro Pozuelo aliifungia bao la kwanza Genk dakika ya 54 kabla ya mshambuliaji Mgiriki, Nikolaos Karelis kufunga la pili dakika ya 66, wote wakimalizia pasi za mshambuliaji Mjamaica, Leon Bailey.

Na ni Nikolaos Karelis aliyempisha Samatta, Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' dakika ya 66 mara tu baada ya kufunga bao la pili. Bao pekee la wageni lilifungwa na kiungo Mbelgiji, Jamo Molenberghs dakika ya 82.
Huo unakuwa mchezo wa 31 kwa Samatta tangu amejiunga na Genk Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya DRC, 18 msimu uliopita na 12 msimu huu, akifunga mabao nane, matatu msimu huu na matano msimu uliopita.
Katika mechi hizo, ni 16 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na tano msimu huu, wakati 14 alitokea benchi nane msimu uliopita na 11 msimu huu – na mechi tisa hakumaliza akitolewa, sita msimu uliopita na tatu msimu huu.

Saturday 29 October 2016

YALIOTUFIKIA LEO MAGAZETINI OCT 30 2016 JUMAPILI



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYB2f_hlGTxMYOKjPj07TaDFaDZ1BsGMcD_vcfsPxumMukM5a4Qs4vbjTyMMmk3E-voCPJjXl3Fre4Oy989BONQgKCMIfRAeC0OSeKYl5nyr1UGQb45eI4Ky83-VCjJ0ix97dAhh1H838-/s1600/1.PNG

ACT wamjibu Ole-Sendeka



  Chama cha ACT-Wazalendo kimefungua milango kukaribisha uchunguzi juu ya mali na madeni ya kiongozi wake mkuu Zitto Kabwe.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu wa Kamati ya Bunge na Serikali za Mitaa ya ACT, Habib Mchange alisema chama hicho hakina shaka kwamba kiongozi wake ni msafi.
"Tunavitaka vyombo vya uchunguzi vianze kazi hiyo mara moja na tutafurahi ukihusisha pia akaunti zake binafsi "alisema Mchange

9 wauawa katika shambulio Maiduguri Nigeria

Watu 9 wameuawa na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa baada ya walipuaji wa kujitoa muhanga wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Boko Haram kuushambulia mji wa Maiduguri uliopo kaskazini mashariki mwa Nigeria, maafisa wanasema.

Inaarifiwa kuwa washambuliaji hao walizunguka mjini ndani ya bajaji.
Mlipuko wa kwanza ulitokea wakati walipuaji wawili wa kujitoa muhanga walipojaribu kuingia katika kambi - ambayo maelfu ya watu wanaishi baada ya kulazimika kuyatoroka makaazi yao kufuatia kuzuka uasi.

Jamaa mmoja aliyeshuhudia mkasa huo ameeleza kuona watu waliojeruhiwa wakivuja damu.
Muda mfupi baadaye kumetokea mlipuko wa pili karibu na ghala la mafuta.
Jeshi la Nigeria limepiga hatua kubwa katika vita vyake dhidi ya Boko Haram.
Lakini wanamgambo hao wa kiislamu bado ni tishio na hutekeleza mashambulio ya kujitoa muhanga kila mara.

Ndege yashika moto ikipaa

Watu zaidi ya 20 wamejeruhiwa baada ya ndege ya Shirika la American Airline Boening B767 Flight number 383 iliyokuwa ikitokea Chicago kuelekea Miami imeungua moo. Injini ya kulia ya ndege hiyo imelipuka wakati ikijiandaa kupaa katika uwanja wa ndege wa O’Hare.
Viongozi wa ndege hiyo wanasema kuwa abiria saba na mhudumu mmoja walijeruhiwa lakini walikimbizwa hospitali kwa uchunguzi.
Hata hivyo baadaye uongozi wa ndege hiyo ulisema kuwa watu zaidi ya 20 walikimbizwa

Guardiola arusha kijembe cha chini chini kwa Man United kwa matumizi ya mipira mirefu

Pep Guardiola ameendelea kuwachimba Manchester United chini chini kwa matumizi yao makubwa ya mipira ya mirefu na kudadavua anachopenda hasa kifanyike kwenye timu yake.

Guardiola leo atakuwa na kibarua kigumu mbele ya West Brom kwenye dimba la Hawthorns, mchezo ambao utakuwa mgumu kwake kufuatia kucheza michezo sita mfululizo bila ushindi, rekodi ambayo ni mbaya zaidi kuwahi kutokea katika maisha yake ya ukocha.

Man City walifungwa bao 1-0 dhidi ya mahasimu wao Man United katika Uwanja wa Old Trafford katikati ya wiki hii kwenye mchezo wa Kombe la EFL.

“Goli tulilofungwa katika mchezo dhidi ya United lilitokana na mpira mrefu, tukashindwa kuudhibiti na hatimaye tukafungwa.

“Wakati mwingine unaruhusu goli kwasababu umeshindwa kuzuia mipango ya goli kama ilivyotokea kwetu na wakati mwingine unaweza kutumia pasi ndefu na ukaruhusu goli vile vile.

Guardiola alienda mbali zaidi kwa kusema: “Kwa aina ya washambuliaji tulio nao kama Kelechi, Kun Aguero, si vyema kwangu kutumia pasi ndefu, labda kwa siku zijazo nikinunua straika mwenye urefu wa sentimeta 220 nitaweza kutumia mfumo huo.

Rais Dkt Magufuli Atengua Uteuzi Wa Mkurugenzi Wa Upelelezi Makosa Ya Jinai (Dci) Diwani Athumani Leo

Taarifa kutokea Ikulu Dar es salaam leo October 29 2016 ni pamoja na hii ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Nchini (DCI) Diwani Athumani.

Mjumbe wa Shirikisho la Soka Afrika,Said El Maamry kumaliza mgogoro wa beki Hassan Ramadhani Kessy

said-el-maamry
Mjumbe wa heshima wa Shirikisho la Soka Afrika,Said El Maamry

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Mjumbe wa heshima wa Shirikisho la Soka Afrika,Said El Maamry anatarajia kuwakutanisha viongozi wa Simba na Yanga ili kumaliza utata wa beki Hassan Ramadhani Kessy na kuotoa mgogoro uliopo katika usajili kwa pande zote mbili.
El Maamry anakutana na pande hizo mbili kujadili suala la beki Hassan Kessy ambaye Simba inamlalamikia kusajili na Yanga huku akijua ana mkataba na wana msimbazi na Kessy anailalamikiwa Simba.
“Kweli El Maamry amekubali na leo, ndiyo tunakutana kwa ajili ya kulimaliza suala hilo na Simba,” alisema mmoja wa viongozi wa Yanga kutoka makao makuu ya Yanga, Jangwani jijini Dar es Salaam.
  Alisema kuwa Lengo letu ni kulimaliza hili suala, kwa kuwa hii nafasi ya El Maamry ni nzuri kwa maana hiyo ya kulimaliza, tunaamini tutafikia mwafaka na kumuacha mchezaji akili yake awaze mpira tu na sio mambo mengine.
Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ambayo inashughulikia suala hilo, ilitoa nafasi kwa Yanga na Simba kufikia mwafaka kabla yenyewe haijatoa maamuzi.
Lakini kama Yanga itashindwa na kuamliwa kulipa, itakuwa tatizo kwao kwa kuwa tayari imeshamtumia Kessy katika mechi kadhaa za ligi kwa upande mwingine msemaji wa TFF alishawahi kusema kuwa ishu ya Kessy sio usajili na kuwaondoa mashabiki wa Yanga kuwa hawawezi kukatwa pointi zozote kwani usajili wake ulipitishwa. Beki huyu ameingia matatani na klabu yake ya zamani yaani Simba kwa madai kuwa alivunja mkataba na kujiunga na Yanga huku akijua kabisa ni kosa hivyo kamati itatoa uamuzi sahihi na sio wa kukomoana hekima na busara zitatumika kumaliza suala hilo ambalo limekuwa ngumzo kwa wadau.
Baada ya kamati hiyo kukaa na kupata maamuzi, iliona inawezekana pia Yanga na Simba kukutana na kulimaliza suala hilo badala ya kutoa maamuzi ambayo yatakuwa yanauumiza upande mmoja

Mariah Carey anataka alipwe mamilioni na ex wake bilionea

Mariah Carey anaweza kubaki na pete ya dola milioni 10 aliyovishwa na mchumba wake James Packer waliyeachana. Lakini hiyo haitoshi, muimbaji anataka zaidi.
Wawili hao waliachana baada ya kuzuka ugomvi walipokuwa wakila bata kwenye yacht nchini Ugiriki mwezi September kufuatia tetesi kuwa diva huyo anachepuka na dancer wake, Bryan Tanaka.
Kwa mujibu wa ripoti, Carey anataka alipwe dola milioni 50 kutoka kwa Packer baada ya kumhamishia LA na anadai kuwa ameathirika na kuachana kwao kiasi cha kukatisha ziara yake ya Amerika Kusini.

Hata hivyo vyanzo vilivyo karibu na bilionea huyo vimedai kuwa Carey asahau kupewa hata senti. “Ni ujinga kudai kuwa James ni sababu ya kusitisha ziara yake ya Amerika Kusini. Siku chache zilizopita aliwalaumu mapromota,” kilisema chanzo.
Sababu kubwa inayoelezwa kuwa chanzo cha wawili hao kuachana ni usaliti wa Carey na matumizi makubwa ya fedha. Wawakilishi wa muimbaji huyo wanakanusha.

Rais Magufuli atimiza miaka 57 awashukuru wananchi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli leo Oktoba 29, 2016 anasherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake ambapo anatimiza miaka 57.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa ‘twitter’  Rais Dkt. Magufuli amewashukuru watanzania wote kwa kumtakia heri na kuahidi kuendelea  kuchapa kazi kwa maslahi ya taifa.

“Ninamshukuru Mungu kufikia siku yangu ya kuzaliwa,ninawashukuru watanzania nyote kwa kuniombea , nitafanya kazi kwa moyo na nguvu zangu zote” Amesema Rais Dkt. Magufuli.

Aidha Rais Dkt. Magufuli anasherehekea siku yake ya kuzaliwa ikiwa anakaribia kutimiza mwaka mmoja tangu alipoapa kuliongoza taifa la Tanzania Novemba 5, 2015.
Rais  Dkt. Magufuli alizaliwa Oktoba 29, 1959 katika Wilaya ya Chato ambayo ni mojawapo ya wilaya tano za mkoa mpya wa Geita uliopo kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Wilaya ya Chato ilikuwa sehemu ya Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera na ni mwaka 2012 tu ndipo ilipohamishiwa Mkoa wa Geita.

Kamati leo kupokea maoni ya wadau wa habari

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Peter Serukamba
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii inatarajia kukutana na wadau wa habari leo, kupokea maoni yao kwa ajili ya kuboresha Muswada wa Sheria ya Huduma ya Habari wa mwaka 2016, unaotarajiwa kusomwa bungeni kwa mara ya pili hivi karibuni.
Wadau hao, waliotakiwa kutoa maoni yao tangu wiki iliyopita mbele ya kamati hiyo, waligoma kutoa kwa madai kuwa walipatiwa taarifa za kuwasilisha maoni yao kwenye kamati hiyo katika kipindi kifupi hivyo hawakujiandaa vyema.
Wadau waliohudhuria kikao hicho na kuomba kuongezewa muda ni Jukwaa la Wahariri (TEF), klabu mbalimbali za waandishi wa habari, Baraza la Habari Tanzania (MCT), Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), MISATan, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).

Katika kikao hicho, wadau hao waliomba kuongezewa muda wa takribani miezi minne ili waweze kushirikisha wadau wengi zaidi kuupitia muswada huo na kutoa maoni yao kwa mrengo mmoja.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter Serukamba, aliongeza siku tisa ili wadau hao wajiandae kutoa maoni yao kwa ajili ya kuboresha muswada huo akibainisha kuwa muda uliotolewa kwa wadau hao tangu awali ulikuwa unatosha.
Mwenyekiti huyo alisema kamati hiyo haitaweza kukamilisha kazi yake ya kupitia na kuboresha muswada huo bila kupata maoni ya wadau ambayo nayo yatasaidia kuuboresha zaidi muswada huo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kitengo cha habari na mawasiliano jana, kamati hiyo imepanga kupokea maoni ya wadau hao mjini Dodoma.

Mechi za ligi daraja la kwanza msimu wa 2016/2017 kuendelea leo

Mechi za Ligi Daraja la Kwanza msimu wa 2016/2017 zitaendelea tena leo Oktoba 29, 2016 kwa michezo minane ya makundi A, B na C.
Katika kundi A kutakuwa na michezo miwili ambako Polisi Dar itacheza na Lipuli ya Iringa kwenye Uwanja wa Karume, ulioko Ilala jijini Dar es Salaam wakati Friends Rangers itasafieri hadi Tanga kupambana na African Sports kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Jumatatu Oktoba 31, mwaka huu kutakuwa pia na michezo miwili ya kundi hilo ambako Mshikamano na Ashanti zitachuana jijini Dar es Salaam kwenye kwenye Uwanja wa Karume, ulioko Ilala jijini.

Kundi B kutakuwa na michezo mitatu kwa siku ya leo Oktoba 29, 2016 ambako Mlale itaikaribisha Coastal Union ya Tanga kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea wakati Kurugenzi ya Mafinga itakuwa mwenyeji wa Kemondo ya Morogoro kwenye Uwanja wa Uwambi huko Iringa ilhali Njombe Mji itacheza na Mbeya Warriors ya Mbeya huko Makambako.

Katika kundi hilo, KMC ya Dar es Salaam itacheza Jumatatu Oktoba 31, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani.

Kadhalika Kundi C kutakuwa na mechi tatu. Mechi hizi ni kati ya Singida United itayocheza na Polisi Mara kwenye dimba la Namfua mjini humo wakati kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Polisi itakuwa mwenyeji wa Rhino ya Tabora ilhali Panone ya Kilimanjaro itacheza na Mgambo JKT ya Tanga kwenye Uwanja wa Ushisirika mjini Moshi.

Tony Pulis amesaini mkataba mpya wakuendelea kuifundisha West Brom

Kocha wa klabu ya West Brom, Tony Pulis amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja katika klabu hiyo ambao utamfanya aitumikie timu hiyo mpaka mwaka 2018.

Jeshi la Nigeria Lawaachilia Watoto 876

  Umoja wa Mataifa umefanikisha kuachiliwa kwa watoto 876 wanaozuiliwa na wanajeshi wa Nigeria na vikosi vya usalama baada ya kuteka ardhi iliyokuwa ikikaliwa na Boko Haram.
Watoto hao wamekuwa wakizuiliwa katika kambi za kijeshi kwenye mji wa Maiduguri ulio Kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Wanajeshi huwazuilia raia ambao wamekuwa wakiishi maeneo ambayo yamekuwa yakikaliwa na wanamgambo wa kiislamu, kwa kuwashukuwa kwa wana uhusiano na shughuli za wanamgambo hao.
Hata hivyo makundi ya kibinadamu yanalalamika kuwa hakuna sheria ya kuwafungulia mashtaka watu hao.
Baadhi yao hupelekwa kwa vituo vya kurekebisha tabia ambavyo makundi ya kibinadamu yanasema kuwa vinafanana na magereza.

Friday 28 October 2016

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiTHi76hCzcuaDzoxUyOYYWA23zkcpU2lTnlNjNJ51smhLDEcjAzYcyEX791aa5jl_I8NqjFeQk7LTEG2cl0UN596BUntB5HxKITQhzVU6FVnUaD9-o2HUSQVeJjOmVeqDFW8k0-S0rLly-/s1600/1.PNG

Dkt. Ali Mohamed Shein, kesho tarehe 29/10/2016 anatarajia kukiongoza Kikao cha Kamati

shein
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi (BLM), Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, kesho tarehe  29/10/2016 anatarajia kukiongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar – Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Waride Bakar Jabu, amesema kikao hicho cha kawaida cha siku moja kitafanyika Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Amesema kikao pamoja na mambo mengine, kitapokea na kujadili taarifa mbali mbali kutoka Idara na Vitengo vya Chama hicho na kuongeza kuwa maandalizi yote yamekamilika.
Aidha, Katibu Waride amesema kikao hicho kilitanguliwa na Kikao cha Sekretarieti ya Kamati Maalum ya NEC, kilichokutana tarehe 26 Octoba, mwaka huu, chini ya Mwenyekiti wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Mhe. Vuai Ali Vuai, kwa lengo la kuandaa Agenda za kikao hicho.
                               “KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI”
Waride Bakar Jabu
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC
Idara ya Itikadi na Uenezi – CCM
ZANZIBAR.
28/10/2016

Uzinduzi wa Ligi ya Taifa ya Wanawake unatarajiwa kufanyika Novemba 1 2016

karuma
Uzinduzi wa Ligi ya Taifa ya Wanawake unatarajiwa kufanyika Novemba 1, 2016 kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma katika mchezo ambao Baobao itacheza na Victoria Queens ya Kagera.
Ligi hiyo ya kwanza kufanyika nchini Tanzania, lakini pia kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati imetokea kuvutia wadau kadhaa wakiwamo Azam Tv ambao wamedhamini kwa kuonyesha mubashari (live), michezo hiyo 30 itakayofanyika viwanja mbalimbali.
TFF imepeleka uzinduzi huo Dodoma ikiwa na lengo la kuhamasisha soka mikoani tofauti na Dar es Salaam ambako ilizoeleka zaidi miaka ya nyuma kabla ya kuwa na mpango wa mashindano ya aina hiyo yanayoshirikisha timu 12 kutoka kona mbalimbali za nchi.
Kadhalika, kwa siku ya Novemba mosi ya uzinduzi huo vingozi wengi wa Serikali wakiwamo wabunge wanatajiwa kuwa Dodoma ambako watapata fursa pekee ya kushuhudia burudani ya mpira wa miguu wa ushindani itakayosukuma hamasa ya kutoa michango yao mbalimbali kwa ajili ya soka la wanawake.
Mbali ya mchezo huo wa kundi B kati ya Baobao na Victoria, michezo mingine itakuwa ni kati ya Sisterz na Panama utakaofanyika Uwanja wa Tanganyika huko Kigoma wakati Marsh Academy ya Mwanza itacheza na Majengo Women ya Singida kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kundi A kutakuwa na michezo mitatu ambako Viva Queens ya Mtwara itacheza na Mburahati Queens ya Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona wakati Fair Play ya Tanga itapambana na Evergreen ya Dar Salaam katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga huku JKT Queens ikiwa ni wenyeji wa Mlandizi Queens ya Pwani kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Habari Picha

nun1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akisalimiana na Meya wa manispaa ya Dodoma, Jafar Mwanyemba  na Sheikh Shabaan Kitila baada ya Sala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Nunge mjini Dodoma Oktoba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
nun2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya waumini wa dini ya Kiislam baada ya Sala ya Ijumaa kwenye msikiti wa Nunge mjini Dodoma Oktoba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
nun3
Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislam  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati    alipozungumza baada ya sala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Nunge mjini Dodoma Oktoba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
nun4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki katika Dua ya kuwaombea wanafunzi wote wa Tanzania wanaotarajia kufanya mtihani wa Kidato cha Nne ili wafanye vizuri akiwa katika  Sala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Nunge mjini Dodoma Oktoba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
nun5
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya Sala ya Ijumaa kwenye Msikiti wa Nunge mjini Dodoma Oktoba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)