Saturday 26 December 2015

Waraghabishi Wakoleza Kasi Ya Mabadiliko Wilayani Kishapu


 Watendaji wa Kituo cha Maendeleo Cha Jamii ya Uchunga Wilayani Kishapu wakiwa katika Picha ya pamoja na Wanafunzi Mbele ya Jengo la kituo Hicho likiwa limekamilika kutokana na Michango yao ya fedha Na Nguvu kazi. 

Na Mwandishi Wetu

Mabadiliko katika Jamii yoyote kwa kiasi kikubwa Huchangiwa na Ongezeo la Mahitaji ya Binadamu katika Mambo Mbalimbali. Kwamba, kadri Dunia inavyopitia Mabadiliko, kadiri ile ile Changamoto, Mahitaji na Huduma katika Jamii Husika Huongezeka.

Ili kufikia Malengo Yanayotokana na Misukumo na Mageuzi Yasiyokwepeka, Binadamu Amelazimika kubuni Mikakati Mbalimbali ya Maendeleo.

 Si hivyo tu, Mabadiliko Haya Yamemfungulia Binadamu fursa ya Uthubutu wa kujaribu Mambo Mbalimbali, Siyo tu kwa faida yake, Bali Jamii Nzima inayomzunguka.

"Sikutegemea kama siku Moja katika Maisha yangu Nitapata wazo Ambalo lingebadili na kushawishi Watu kuchukua Hatua kwa Mustakabali wa Jamii.” 

Hiyo ni kauli ya Mraghbishi Revocatus Richard ambaye pia, kitaaluma ni Mwalimu katika Shule ya msingi Uchunga. Richard Alitoa kauli hiyo Baada ya kupitia Mafunzo ya Uraghbishi na Mwalimu Mwenzake, Restusta Katobesi, ambao Baadaye kwa pamoja, Walianzisha Kituo cha Kimaju (Kituo cha Maendeleo cha Jamii ya Uchunga) kwa kushirikiana Na Uongozi wa kijiji na Wananchi.

 Na Hilo Ndiyo lilifanya Achaguliwe kuwa Mkurugenzi wa kituo Hicho

No comments:

Post a Comment