Saturday 26 December 2015

Gwajima Amekataa Kuwa Hakuwahi Kumuunga Mkono Lowassa


Image result for askofu gwajima
Mchungaji Josephat Gwajima wa Ufunuo

Na Kalonga Kasati

Mchungaji Kanisa la Ufufuo na Uzima,Josephat Gwajima Amejitokeza Hadharani  na kukana kwamba Hakuwahi kumuunga Mkono Edward Lowassa Wakati Wa kampeni za Urais.

Akiongea katika Mahojiano Maalumu na kituo Cha Azam Tv, Gwajima Amesema yeye Hakuwahi kuwa Mshirika wa Lowassa wala Chama chochote, Bali Aliitwa Jijini Arusha na Jangwan Dar es Salaam  kwa Ajili ya Maombi Tu na SiVinginevyo

Amesema kitendo cha kukubali Wito huo wa Maombi kimewafanya Watanzania Walihisi kwamba Yeye alikuwa Team Lowassa, kitu Ambacho sio kweli.

Amedai yeye alikuwa Mfuasi wa Mabadiliko ya nchi, Alikuwa Akiunga Mabadiliko ya nchi Na Sio Personality ya Mtu au chama cha Mtu.

Wakati Gwajima Akikana kumuunga mkono Lowasaa, kumbukumbu Zinaonyesha kuwa Mchungaji Huyo Alikuwa ni Team Lowassa na  Alikuwa Mstari wa Mbele kuhakikisha Mheshimiwa Lowassa Anashinda kiti cha Urais.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Gwajima Alitumia Nguvu kubwa Sana Wakati wa kampeni kupambana na Dr Slaa ambaye Wakati huo Alikuwa Akishusha Makombora Mazito kuhakikisha Lowassa Hashindi huku Akimtuhumu Gwajima kuwa Mshenga wa Lowassa Aliyemfuata kumpigia debe Wampokee Chadem
a

No comments:

Post a Comment