
Pambano hilo lilimalizika kwa sare ya 1-1 baada ya dakika za nyongeza, Neymar akiwa ameifungia Brazil bao kwa mkwaju wa free-kick kipindi cha kwanza lakini goli hilo likasawazishwa na Max Mayer.

Ushindi huo umekuja miaka miwili baada ya Ujerumani kuidhalilisha Brazil kwa kipigo cha magoli 7-1 kwenye fainali za kombela dunia mwaka 2014 hatua ya nusu fainali.

Neymar ambaye ni mshambuliaji wa Barcelona aliyeukosa mchezo wa nusu fainali ya kombe la dunia kutokana na kuwa majeruhi, alifungua nyavu za Ujerumani kwa mpira wa adhabu ndogo mita 25 toka langoni na kufanikiwa kwenda mapumziko wakiwa mbele.

Hakuna timu yeyote iliyoweza kupata goli la ushindi kabla ya kufika kwenye changamoto za mikwaju ya penati ambazo zilimalizika kwa Brazil kutwaa medali ya dhahabu.

Neymar akaongeza: “Hiki ni miongoni mwa vitu muhimu ambavyo vimetokea maishani mwangu. Ni hivyo tu.”
Mechi ya kisasi
Miaka miwili iliyopita, wenyeji wa michunao ya kombe la dunia huku wakipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri, Brazil walijikuta wakiangukia kipigo kikubwa kuwahi kukutana nacho kwenye fainali za kombe la dunia baada ya kujikuta wamechakazwa goli 5-0 ndani ya dakika 29 kwenye kichapo cha bao 7-1 kutoka kwa wajerumani.

Alisema hakuna mchezaji wake aliyekuwepo kwenye mchezo wa nusu fainali ya kombe la dunia huku kikosi chake cha Olympic kikiwa na nafasi ya kuchezesha wachezaji watatu pekee waliovuka umri wa maiaka 23.
“That was the World Cup, this is the Olympic team,” said Micale. “Neymar never played in that match so there is nothing that could generate any type of feeling that we have to take revenge.
“It is a different time with different players and ages.”
“Wakati ule ilikuwa ni kombe la dunia, sasa ni Olympic,” alisema Micale. ”Neymar hakucheza kwenye mchezo ule kwahiyo hakuna kitakacholeta hisia za kulipa kisasi.”
“Ni wakati tofauti, timu tofauti na umri tofauti.”
Mashabiki wengi walijitokeza kuishangilia Brazil kwenye uwanja wa Maracana na walipata kile walichokitarajia kutoka kwa timu yao.”
Nigeria yatwaa medali ya shaba
Nigeria wameshinda medali yao ya kwanza kwenye mashindano ya Olympic mwaka 2016 baada ya kuifunga Honduras mabao 3-2 kwenye mchezo wa kuwania medali ya shaba ambapo Sadiq Umar alifunga mara mbili huku Aminu Umar akifunga bao moja.
Kiungo wa Chelsea John Mikel Obi, aliyekuwa nahodha wa Nigeria amesema: “Nimefurahishwa na hiki kikosi, vijana walijituma sana.”
“Ni muhimu sana kwasababu mchezo wa soka unapendwa sana Nigeria. Tulikuwa na presha nyuma yetu lakini tumejitahidi tumefanya kile tulichoweza kwa ajili yetu, familia zetu na Nigeria.”
No comments:
Post a Comment