Monday, 8 February 2016

Tamko la Waziri Ummy Mwalimu kuhusu Ugonjwa Wa kipindupindu

UM2
TAMKO KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI PAMOJA NA TAHADHARI YA UGONJWA WA HOMA YA ZIKA, LILILOTOLEWA NA MHE. UMMY MWALIMU (MB); WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO Y
A JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, TAREHE 8 FEBRUARI 2016.
Na Tabu Mullah
Kuhusu ugonjwa wa kipindupindu, huu ni mwendelezo wa taarifa ya wiki kwa umma, ya Mwenendo wa Ugonjwa huu hapa nchini. Hadi kufikia tarehe 7 Februari 2016, jumla ya watu 15325 wameugua ugonjwa huo, na kati yao watu  238 wamepoteza maisha kwa ugonjwa huu.  
Takwimu za Kuanzia tarehe 1 hadi 7 Februari 2016, zinaonyesha kuwa idadi ya wagonjwa Walioripotiwa wiki hii imepungua kutoka 459 ya wiki iliyoishia tarehe 31 Januari hadi 258 Ambapo ni sawa na punguzo la asilimia 44. Kuna vifo 5, sawa na idadi ya vifo vilivyoripotiwa katika wiki iliyopita.

Jumla ya mikoa ambayo imeripoti kuwa na wagonjwa ni 13 ambapo mkoa wa  Mara ndio umeongoza kwa kuripoti idadi kubwa zaidi ya wagonjwa ukilinganishwa na mikoa mingine, ukiwa na wagonjwa 73 (Musoma Vijijini 33,  Musoma mjini 5, Bunda 1, Butiama 13, na Tarime Vijijini 21), ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza (70)- (Ukerewe 21, Nyamagana 24, Ilemela 8, Sengerema 5 na Buchosa 12). Mikoa mingine ni pamoja na Simiyu (30), Morogoro (26) na Kilimanjaro (16). 
Katika mapambano ya kudhibiti mlipuko huu wa Kipindupindu, kuna changamoto mbalimbali zilizobainishwa na Wizara yangu kupitia wataalam ambao wanashirikiana na timu zilizopo katika mikoa na wilaya zilizoathirika. Mojawapo wa changamoto ni utoaji wa idadi pungufu ya wagonjwa au kutotoa kabisa taarifa za wagonjwa wa Kipindupindu. Hii inapelekea kusababisha mikakati iliyowekwa kutokuwa na mafanikio hivyo ugonjwa kuendelea kuwa ni tishio katika jamii. Ninapenda kusisitiza kuwa, taarifa za wagonjwa wa Kipindupindu zitolewe bila kuficha, na watendaji watakaoficha taarifa za wagonjwa watawajibishwa ipasavyo.

Changamoto nyingine iliyopo ni ushiriki mdogo wa sekta nyingine katika kupambana na ugonjwa huu. Ninaomba ieleweke kuwa mapambano dhidi ya Kipindupindu yatafanikiwa ikiwa sekta nyingine kama Maji, miundombinu, biashara, elimu, mazingira n.k zitashirikiana. Wizara yangu imeendelea kusisitiiza ushirikiano huu katika ngazi ya Taifa, Mkoa na Wilaya, ili mipango ya kupambana na Kipindupindu ishirikishe sekta mbalimbali na pia Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Taasisi za Dini na Vyombo ya Habari. 

KAMATI KUU YAFANYA UTEUZI WA WAGOMBEA WATAKAOZIBA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI CC

Katibu wa Itikadi na Uenezi Mhe. Nape Nnauye akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa NEC, Makao Makuu ya CCM, Ofisi Ndogo Lumumba.
Jana tarehe 07/02/2016 Kamati Kuu ya
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ilikuwa na kikao maalum cha siku moja mjini
Dodoma. Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho
Kikwete. Kikao hicho kilikuwa na kazi ya kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali
zilizo wazi za uongozi ndani ya CCM mikoani na wilayani ambazo uteuzi wake upo
kwenye Mamlaka ya Vikao vya Chama Taifa.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YAANZA KAZI RASMI – YAPOKEA TAARIFA YA UTENDAJI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHINI

TI1
  1. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akijitambulisha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kabla ya Kamati hiyo kuipokea taarifa ya Wizara hiyo katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo baada ya kuundwa na Bunge hivi karibuni. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu anayefuatia ni Makamu wake, Kanali Masoud Khamis. Kulia kwa Masauni ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
TI2
  1. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Mohamed Rajabu akizungumza jambo na Wajumbe wa Kamati yake pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika kikao chao kwanza tangu Kamati hiyo iundwe na Bunge hivi karibuni. Wapili kulia mstari wa mbele ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni, na kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Kanali Masoud Khamis. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
TI3
  1. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akitoa taarifa ya Wizara katika kikao cha kwanza cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kikao hicho kilichohudhuriwa na Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na Maafisa wa Wizara, kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi M
TI4Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Injinia Hamad Masauni (hayupo pichani) alipokuwa anawasilisha taarifa ya Wizara kwa Kamati hiyo katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
TI5Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni (katikati) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira wakiiweka sawa taarifa ya wizara yao kabla ya kuiwasilisha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu. Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na Watendaji wa Wizara walikutana katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo, kwa ajili ya kujadili Masuala mbalimbali ya Ulinzi na Usalama.

No comments:

Post a Comment