Tuesday 16 February 2016

Watoto 60 wenye Umri wa chini ya Miaka mitano (5) kisiwani Pemba Wamepatiwa Kinga ya kifua kifuu

PE
Na Tabu Mullah
JUMLA ya watoto 60 wenye umri wa chini ya miaka mitano (5) kisiwani Pemba wamepatiwa kinga dhidi ya ugonjwa wa kifua kifuu (Isonizid Prevent Therapy ) kwa kipindi cha kuanzia janauri hadi disemba mwaka 2015 .
 
Akizungumza na mtandao huu jana  huko Ofisini kwake Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba , Ofisi wa habari , elimu na mawasiliano kutoka Kitengo cha kifua kikuu Wizara ya Pemba Hasnuu Fakih Hassan amesema kuwa watoto hao  wale ambao wazazi wao wanaugonjwa wa kifua kikuu .
 
Amesema kwamba matibabu hayo  ambayo yameanzishwa kwa watoto hao  yamesaidia katika  kuwakinga watoto  hado dhidi ya maambukizi ya Ugonjwa huo ambapo hali zao zinaendelea vyema .
Hasnuu alizidi kufafanua kwamba  watoto hao ishirini (20)  wanatoka Mkoa wa Kaskazini Pemba na arobaini (40)  wanatoka Mkoa wa Kusini Pemba
“Tunao watoto zaidi ya sitini walio chini ya umri wa miaka mitano , tumewaanzishi kinga dhidi ya ugonjwa kifua kikuu Isonized Prevent Therapy , matibabu ambayo yanawahusu watoto ambao wazazi wao wanaugonjwa wa kifua kikuu ” alifahamisha .
Aidha alifahamisha kwamba Kitengo hicho kimeweza kuwafikia wagonjwa wa kifua kikuu katika maeneo wanayoishi , ambapo baada ya kuwapatia huduma wagonjwa pia  wanatalaamu hutumia muda huo kwa ajili ya kutoa elimu kwa jamii .
 
Akizungumzia maambukizi ya Ugonjwa huo Kisiwani Pemba Hasnuu  alisema kwamba idadi ya wagonjwa wa kifua kikuu imeongezeka kutokana na jamii kuwa na mwamko wa kupima afya zao mara kwa mara .
 
Alisema kwama katika kipindi cha oktoba hadi disemba Mkoa wa Kusini Pemba ulikuwa na wagonjwa 74 ambapo Mkoa wa Kaskazini Pemba ulipatikana wagonjwa 36 .
Alifahamisha kwamba ongezeko la wazazi katika Mkoa wa Kusini Pemba imechangiwa na uwepo na kituo cha maabara ya afya ya jamii , ambacho wamekuwa wakifanya kazi kwa ushirikiano wa karibu .
“Unaweza kushangaa kuona kwamba Idadi ni kubwa Mkoa wa Kusini Pemba , hii ni kutokana na uwepo na maabara ya afya ya jamii ambayo imekuwa ikishirikiana nasi katika kutoa Taaluma na uchunguzi wa maradhi hayo ” alifahamisha .
 
Hivyo ameitaka jamii kufika haraka katika vituo vya afya kwa ajili ya kufanya uchunguzi pindi wanapobaini kwamba wanadalili ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu , na kuongeza kwamba malengo ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 , Pemba kusiwepo na mgonjwa wa kifua kikuu .

DK. KIGWANGALLA ADHURU KAMBI YA WAGONJWA WA KIPINDUPINDU YA IRINGA

kigwa5
Eneo la vijiji vya Pawaga linavyoonekana kwa picha za angani wakati wa Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla alipo dhuru kwa kutumia Chopa.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangallla amekuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi za juu kufika katika eneo lililokumbwa na mafuriko katika vijiji vya Mbolimboli, Tarafa ya Pawaga iliyopo Iringa vijijini Mkoani hapa ambapo mbali na kutoa pole pia ameweza kutoa huduma za kitabibu kwa baadhi ya watu waliozidiwa waliokuwa bado hawajaokolewa.

Awali Dk. Kigwangalla alipodhuru kwa wananchi waliopo kwenye kambi ya muda baada ya kunusurika na mafuriko hayo, aliwaeleza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao bega kwa bega kwani Serikali ya “Hapa Kazi Tu” haina ngoja ngoja ndio maana yeye ameweza kufika haraka kuakikisha wananchi wapo salama na wanapatiwa huduma zote za msingi na za kijamii ikiwemo matibabu na elimu ya kijikinga na milipuko ya magonjwa ikiwemo magonjwa ya kipindupindu ambacho kimewakumba wananchi hao.

Dk. Kigwangalla ameweza kufanya hilo baada ya Chopa iliyokuwa ikimtembeza angani kufika katika maeneo yaliyozingirwa, alimuru rubani wake kushusha chini na kisha kutoa msaada wa Haraka kwa akina mama na watoto waliokuwa wamezingirwa kwenye moja ya maeneo hayo zaidi ya siku tatu bila kuokolewa ambapo alitoa huduma na kisha Chopa hiyo iliwabeba hadi katika eneo maalum waliopo wahanga wengine waliookolewa

Pia Dk. Kigwangalla aliweza kutoa elimu na maelekezo mbalimbali kwa wahanga hao kujiepusha na masuala ya kutumia mahitaji salama ilikuepukak kipindupindu kisienee zaidi kwani hadi sasa eneo hilo limeweza kupatikana wagonjwa wa ugonjwa huo zaidi ya 220 huku Hadi wanatembelea katika kambi ya Mtakatifu Lucas iliyopo Pawaga, ilikuwa na wagonjwa zaidi ya 40.
kigwazz
Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla alipo dhuru kwa kutumia Chopa katika eneo lililokumbwa na mafuriko hayo kijiji cha Mbolimboli

No comments:

Post a Comment