Wednesday 24 February 2016

Rais Dkt Mohamed Ali Shein Amekutana na Balozi Mteule wa Kuwait


mah2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza  na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Kuwait Mahadhi Juma Maalim leo alipofika Ikulu Mjini Unguja kujitambulisha,[Picha na Ikulu.]
maha1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Kuwait Mahadhi Juma Maalim leo alipofika Ikulu Mjini Unguja kujitambulisha,[Picha na Ikulu.]

Mpinzani wa Cheka awasili na kutema cheche, Amwita Cheka Babu

ngu2
Bondia Mserbia anayeishi Uingereza, Geard Ajetovic (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Advanced Security, Juma Ndambile (kushoto) na Promota Jay Msangi (kulia) katika mkutano na  waandishi wa habari jana.  Ajetovic atapigana na Francis Cheka Jumamosi kwenye viwanja vya leaders club kuwania mkanda wa uzito wa Super Middle wa Mabara wa chama cha WBF
ngu3
Bondia Mserbia anayeishi Uingereza, Geard Ajetovic (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jana tayari kwa pambano lake la jumamosi dhidhi ya Franci Cheka. kushoto ni Mkurugenzi wa Advanced Security, Juma Ndambile na kulia ni promota Jay Msangi. Ajetovic atapigana na Francis Cheka Jumamosi kwenye viwanja vya leaders club kuwania mkanda wa uzito wa Super Middle wa Mabara wa chama cha WBF.
ngu4
Mkurugenzi wa Advanced Security, Juma Ndambile (katikati) akizungumza katika mkutano huo.

Na Mwandishi wetu
Bondia Geard Ajetovic amewasili nchini na kumuita bondia nyota wa ngumi za kulipwa nchini ,Francis “SMG” Cheka kuwa ni ‘babu’ na hawezi kupigwa na bondia huyo pamoja na kupigana katika ardhi ya Tanzania.
 
Ajetovic alisema kuwa anamjua Cheka  kwani amemuona kwenye pambano lake dhidi ya Thomas Mashali na kusema kuwa ‘amekwisha’ na kamwe si bondia wa kupambana naye.
Alisema kuwa Cheka amepigwa na bondia ambaye si lolote wala chochote na atampiga kabla ya raundi ya tano katika pambano hilo la ubingwa wa Mabara la uzito wa Super Middle unaotambuliwa na chama cha WBF.
 
 
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya  Advanced Security, Juma Ndambile aliwahakikishia mashabiki  wa ngumi za kulipwa nchini kuwa maandalizi ya pambano hilo yamekamilika bada ya ujio wa Ajetovic.
Ndambile alisema kuwa maofisa wa Chama cha WBF, ikiwa pamoja na Rais wake, Howard Goldberg na mwamuzi wa pambano hilo ambao watawasili leo.
 
“Kama nilivyosema hapo awali, dhamira kubwa ya kampuni ya Advanced Security in kuendeleza mchezo wa ngumi za kulipwa nchini hasa kwa mabondia kufaidika na vipaji vyao na si vinginevyo,”
“Ili kufikia lengo letu, Advanced Security imeamua kuwashirikisha mabondia chipukizi katika mapambano ya utangulizi. Mabondia hao chipukizi wanatarajia kutoa changamoto kwa mabondia maarufu ambao pia watashiriki katika pambano hilo,” alisema Ndambile.
 
Alisema kuwa wameandaa mabondia chipukizi ili kupamba siku hiyo. Alisema kuwa Mohamed Bakari atapambana na Cosmas Cheka katika pambano la uzito wa feather la raundi nane (8) huku Mohamed Matumla ataonyeshana kazi na Mustapha Dotto katika pambao la uzito wa Light la raundi nane pia.
 
Bondia mkongwe na maarufu nchini, Mada Maugo ataingia ulingoni kwa kupambana na bondia kutoka Mbeya, Baraka Mwakansope baadala ya bondia Abdallah “Dulla Mbabe” Pazi kama ilivyotangazwa awali.
 
Alisema kuwa pia siku hiyo, bondia wa kike, Lulu Kayage atazichapa na bondia nyota kutoka mkoa wa Mbeya, Mwamne Haji katika pambano la uzito wa fly lilillopangwa kuwa la raundi sita.

Bodi ya Mikopo yatoa utaratibu wa kuwasilisha malalamiko

ven1
Meneja wa Habari , Elimu na Mawasiliano Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB)  Bw. Omega Ngole akiongea  na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko ya wanafunzi kuhusu upatikanaji wa mikopo elimu ya juu uliofanyika Jijini Dar es salaam.

Na Kalonga Kasati
Dar es salaam
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa  utaratibu wa kushughulikia  malalamiko ya wanafunzi wanaopata mikopo katika taasisi za elimu ya juu nchini.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano Omega Ngole alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko ya wanafunzi wa elimu ya juu nchini.

 “Utaratibu huu ulioboreshwa, ni msisitizo na maelekezo ya Serikali ya mwezi Agosti 2011 kupitia iliyokuwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambayo ilielekeza Taasisi zote za Elimu ya Juu nchini zinazopata mikopo kutoka Bodi ya Mikopo kuanzisha Madawati ya Mikopo ili kuongeza ufanisi katika utoaji mikopo”,Alisema Ngole.
Ameongeza kuwa, dawati hilo linatakiwa kusimamiwa na mtumishi teule wa chuo husika mwenye sifa na uhusiano mzuri na jamii na linapaswa kuwa chini ya Makamu Mkuu wa chuo husika anayeshughulikia taaluma.

Meneja Ngole amesisitiza kuwa kwa sasa vyuo vyote vina Maofisa Mikopo ambao wanawajibika kutafuta suluhisho la suala linalowasilishwa na kulitolea majibu.
Akifafanua hatua zinazotakiwa kufuatwa na Maofisa hao katika kutafuta suluhisho la malalamiko ya wanafunzi amesema kuwa, baada ya malalamiko kufika kwa Ofisa Mikopo yanatakiwa yapate suluhisho ndani ya siku mbili tangu kuwasilishwa kwake,ikiwa hatakua na ufumbuzi atatakiwa kuwasiliana na uongozi  wa juu wa chuo husika.

Endapo uongozi  wa juu wa chuo hautokuwa na ufumbuzi, malalamiko hayo yatatakiwa kupelekwa kwenye Ofisi za Kanda ambazo zinapatikana katika Mikoa ya Mwanza, Dodoma, Arusha na Zanzibar au ofisi za makao ya makuu ya Bodi  zilizoko jijini Dar es Salaam.

Bodi ya Mikopo ilianzishwa kwa sheria ya Bunge namba 9 ya mwaka 2004 na kuanza rasmi mwezi Julai 2005 kwa majukumu ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji waliodahiliwa katika Taasisi za Elimu ya Juu pamoja kukusanya marejesho ya mikopo yote iliyotolewa tangu mwaka 199

No comments:

Post a Comment