Friday 19 February 2016

Acacia Stand United fc (CHAMA LA WANA) imejidhatiti Vilivyo kuelekea Mchezo Wake wa kesho

download (6)
Timu ya Acacia Stand United fc (CHAMA LA WANA) imejidhatiti vilivyo kuelekea mchezo wake wa kesho wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Maafande wa jeshi la kujenga taifa JKT Ruvu kutoka Pwani.

Afisa habari wa “CHAMA LA WANA”ISAAC EDWARD amesema wako vizuri kuwaangamiza Maafande hao na kuzoa pointi zote tatu ili kuwapa furaha mashabiki wao ambayo waliikosa katika mchezo wao uliopita walipofungwa nyumbani dhidi ya Simba sc.

“kiukweli tumejidhatiti vilivyo kuelekea mchezo wetu wa kesho dhidi ya JKT Ruvu,tuna kila Sababu ya kushinda mchezo huo licha ya kuwa maafande hao wana kikosi kizuri na benchi la Ufundi lenye watu wazoefu na soka la Tanzania lakini haitakuwa sababu ya kushindwa kuwapa kichapo”

Edward ameongeza kuwa kikosi chao kinazidi  kuimalika kila kukicha na pia ujio wa wachezaji wao Haruna Chanongo na Abuu Ubwa kambini umeongeza Morali kambini.
“Hali ya kikosi hivi sasa iko vizuri na Morali kwa wachezaji ni ya juu sana ukizingatia Haruna Chanongo na Abuu Ubwa wamejumuika na kikosi kambini toka siku ya jumatatu na wameendelea Na Programu za mwalimu kama kawaida,Hapana shaka panapo majaaliwa yake mwenyezi mungu Na kutokana na mfumo wa mwalimu Patrick Liewing na mahitaji yake basi siku ya kesho watashuka dimbani kuisaidia timu”

Pia amewaomba mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo pendwa mkoani shinyanga kujitokeza kwa Wingi kuishangilia kwani katika kipindi hiki cha mzunguko wa pili wa ligi,timu inahitaji sana kupata Ushirikiano mkubwa kutoka kwao ili ifanye vizuri katika michezo yake ijayo na hatimae kushika nafasi za juu pindi ligi itakapo fikia tamati.

“Nawaomba mashabiki na wapenzi wa Acacia Stand United Fc kujitokeza kwa wingi siku ya kesho katika uwanja wa kambarage kuishangilia timu yao ili iweze kupata matokeo mazuri ya ushindi ili tuweze kukaa katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi na hasa katika kipindi hiki cha Mzunguko wa pili wa ligi timu inahitaji sana sapoti ya mashabiki tufanikishe kushinda mechi zilizobaki na hatimae mwisho wa ligi tukae katika nafasi za juu”

Acacia Stand United Fc kesho inashuka dimbani katika uwanja wake wa nyumbani CCM Kambarage mjini shinyanga kucheza na JKT Ruvu ikiwa ni muendelezo wa michezo ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Mwenyekitiwa BMT amteua Mohamed Kiganja kuwa Katibu Mtendaji

BM2
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw. Dionis Malinzi wa pili kutoka kushoto akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu uteuzi wa ndugu Said Kiganja kuwa Kaimu Katibu Mtendaji mpya wa Baraza hilo, wa kwanza kulia ni Msemaji wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Zawadi Msala na wa kwanza kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu.
                                                                    
MohamedKIganjaBMT
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania Deonis Malinzi amemteua Mohamed Kiganja kuwa Katibu Mtendaji mpya wa baraza hilo baada ya aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo Bw. Henry Lihaya kutenguliwa.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti Malinzi ameeleza kuwa Uteuzi huo umekuja baada ya kuona mapungufu ya utendaji kwa aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo.
“Baraza la Michezo Tanzania limefikia maamuzi haya baada ya kutoridhishwa na utendaji wa Bw. Lihaya na hivyo Waziri wa habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye kufanya maamuzi ya kumtengua” alisema Bw. Malinzi

Uteuzi huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya BMT namba 12 ya mwaka 1967 kifungu namba 5(1) ambacho kinampa mamlaka Mwenyekiti wa BMT kuteua Katibu Mtendaji baada ya kupata idhini ya Waziri mwenye dhamana.

Aidha kabla ya uteuzi huo Kiganja alikuwani Afisa Michezo Mkuu katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuanzia mwaka 2015 mpaka uteuzi wake ulivyofanyika.
Pia aliwahi kufanya kazi kama Afisa Mwandamizi Michezo wa Baraza la Michezo Tanzania na Afisa Michezo Mkuu katika Ofisi wa Waziri Mkuu, anashahada ya kwanza ya Elimu katika masuala ya Michezo na Utamaduni kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment