Monday 29 February 2016

Waziri mkuu Kassim Majaliwa Amepokea misaada kutoka Huawei

hal1
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa ambao unafanywa kwa ufadhili wa kampuni ya HUAWEI ya China , kijijini hapo, Februari 28, 2016. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Jordan Lugimbana. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
hal2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea hundi ya shilingi milioni tisa kutoka kwa Mtalaam wa Ufundi wa Kampuni ya simu ya Halotel wa mkoa wa Lindi, Tran The Hoang ili ziweze kugharimia malipo ya kadi za bima ya Afya kwa baadhi ya wakazi wa kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa. Alikuwa katika ziara ya siku moja wilayani humo Februari 29, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
hal3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa ma  Mwanaidi Mussa  na Mkussa Lukoloma (kushoto) wote wa kijiji cha Nandagala wilayani  Ruangwabaada ya kuwakabidhi kadi zao za bima ya Afya ambazo zimegharimiwa na Kampuni ya Simu ya Halotel iliyochangia shilingi milioni tisa kuwawezesha wakazi wa kijiji hicho kufaidi huduma za Bima ya Afya, Februari 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
hal4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea msaada wa vyakula na nguo kutoka kwa Eric Shigongo Mwenyekiti  watu waliojitotelea kusaidia waliopatwa na maafa ya mvua katika kijiji cha Mtondo wilayani Ruangwa wakati Waziri Mkuu alipokwenda kijijini hapo kuwapa pole wananchi Februari 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
hal5
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea msaada wa vyakula na nguo kutoka kwa Eric Shigongo Mwenyekiti  watu waliojitotelea kusaidia waliopatwa na maafa ya mvua katika kijiji cha Mtondo wilayani Ruangwa wakati Waziri Mkuu alipokwenda kijijini hapo kuwapa pole wananchi Februari 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
hal6
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wananchi wa Ruangwa baada ya kuwasili mjini hapo kwa ziara ya siku moja Februari 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
hal7
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wananchi wa Ruangwa baada ya kuwasili mjini hapo kwa ziara ya siku moja Februari 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Nape mgeni rasmi Tamasha la Pasaka Mwanza

PE2Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye Tamasha la Pasaka jijini Mwanza Machi 27.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maaandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama Waziri Nape amekubali kuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo ambalo litaanzia Geita Machi 26 na kumalizia Kahama Machi 28.
Msama alisema kamati yake inaendelea na maandalizi ya kuelekea tamasha hilo ambalo litashirikisha waimbaji mbalimbali hapa nchini.
“Maandalizi kuelekea Tamasha la Pasaka yanaendelea vema, hivyo wakazi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa wajiandae kupokea ujumbe wa neno la Mungu kupitia viongozi wa dini na waimbaji wa muziki wa Injili,” alisema Msama.
Msama alisema baadhi ya waimbaji  waliothibitisha kushiriki tamasha hilo ambao ni pamoja na Rose Muhando, Bonny Mwaitege, Upendo Nkone, Jesca BM Honore, Christopher Mwahangila, Joshua Mlelwa, Sifael Mwabuka, Jenipher Mgendi, Kwaya ya AIC Makongoro na Kwaya ya Wakorintho Wapili.
Aidha Msama alisema viingilio katika tamasha hilo ni shilingi 5000 kwa wakubwa na kwa watoto shilingi 2000.

No comments:

Post a Comment