Thursday 18 February 2016

TAFEYOCO wamuomba Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli akutane na Vijana.

REUTERS1083589_Articolo
Dar es Salaam.
Na Kalonga Kasati
Shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Feminist and Youth Change Organization (TAFEYOCO) limemuomba Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzisha utaratibu wa kukutana na vijana ili kujadiliana mambo mbalimbali.

Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Shirika hilo Bw. Elvis Makumbo alipokuwa akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam katika mkutano  uliyolenga kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri aliyoifanya katika siku mia moja za uongozi wake.

“Vijana kwa sasa katika taifa ni wengi na ndiyo wenye uwezo wa kuleta maendeleo katika nchi na nguvu kazi ya Taifa na wanachangamoto nyingi  hivyo Mheshimiwa Rais  akijaribu kukutana nao nakuwasikiliza matatizo yao itasaidia kuleta mafanikio katika nchi na kujua nini kifanyike kuleta maendeleo katika Taifa,” alisema Bw. Makumbo.

Ameleza kuwa, Mheshimiwa Rais ameonyesha moyo wadhati wa kuwatumikia wananchi kwa kuwawajibisha watu wote walionekana wakitumia vibaya madaraka yao na kufanya ubadhirifu wa pesa za umma kinyume na taratibu za kiutumishi wa umma.

Mbali na hayo Bw.Makumbo amemuomba mheshimiwa Rais kufikiria kuanzisha mfumo au taasisi itakayohakiki mali za mtumishi wa umma na kuhoji ni namna gani mali hizo amezipata ili kupunguza wimbi la watumishi wa umma wanao tumia fedha za serikali vibaya kwa kujinufaisha wenyewe huku wakijiwekea utajiri mkubwa usiyolingana na kipato chao.

Mwenyekiti huyo aliendelea kumwomba Mheshimiwa Rais kuzidi kuzingozea nguvu taasisi za Serikali ili kuzijengea uwezo mkubwa wa kiutendaji mfano wa Taasisi hizo ni TAKUKURU na nyinginezo zinazosimamia mambo mbalimbali Yenye tija kwa Taifa.

Shirika hilo limesema Kauli Mbiu ya Mheshimiwa Rais ya Hapa Kazi Tu imeongeza hari kubwa ya utendaji kwa wananchi kwa kuwahimiza kuwajibika ikiwemo kwa watu wa sekta binafsi na taasisi

Prof Elisante Ole Gabriel akutana na Bodi ya Wakurugenzi ya TSN

man1
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (wa kwanza kulia) akizungumza na wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya magazeti ya Serikali ya Tanzania Standard Newspaper Ltd (TSN) kuhusu changamoto mbalimbali za kampuni hiyo  leo jijini Dar es Salaam. Kulia kwa katibu mkuu ni Prof Moses Warioba ambaye ni mwenyekiti wa bodi hiyo.
man2
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya magazeti ya Serikali ya Tanzania Standard Newspaper Ltd (TSN) Bw.Prof Moses Warioba (kushoto).
man3
Wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya magazeti ya Serikali ya Tanzania Standard Newspaper Ltd (TSN) wakimskiliza Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kuzungumzia changamoto mbali mbali za kampuni hiyo.kutoka kulia ni Dkt Consolatha Ishebabi,Dkt Evelyn Richard na Bw,Alfred Nchimbi.
Picha na Daudi Manongi-WHUSM

Kwaya mbili kusindikiza Tamasha la Pasaka

Kwaya ya Kekundu (2)
Na Mwandishi Wetu
KWAYA mbili za nyimbo za Injili zimethibitisha kushiriki Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika  mikoa ya Kanda ya Ziwa kuanzia Machi 26 hadi 28.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama tamasha hilo linaanza Geita katika ukumbi wa Desire ambalo litafanyika Machi 26, Mwanza kwenye uwanja wa CCM Kirumba litafanyika Machi 27 na Kahama Machi 28 kwenye uwanja wa Taifa.

Msama alizitaja kwaya hizo zinazotarajia kupanda jukwaani katika mikoa hiyo ni pamoja na AIC Makongoro Vijana ya jijini Mwanza sambamba na Wakorintho Wapili ya Mafinga ya Iringa.
Msama alitoa wito kwa wakazi wa mikoa hiyo kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo ambalo Malengo yake ni kusaidia wenye uhitaji maalum ambao ni walemavu, yatima na wajane.

“Nawaomba wakazi wa mikoa ya Kanda ya ziwa kujitokeza kwa wingi ili tuwasaidie wenzetu wenye Uhitaji maalum ambao ili wafikie malengo wanahitaji kutoka kwetu,” alisema Msama.
Aidha Msama alisema  bado wanaendelea kufanya mawasiliano na waimbaji mbalimbali wa Tanzania ambao kwa pamoja watafikisha ujumbe wa neno la Mungu kwa jamii.

No comments:

Post a Comment