Tuesday, 9 February 2016

Uzagaaji Wa Silaha na Risasi Sheria Mpya Ya kudhibiti

ge1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wa Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara hiyo, Marlin Komba. Kulia ni Mwakilishi wa Katibu Mtendaji wa  Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika Mapambano ya Kuzuia na Kudhibiti Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA), Esaka Mugasa. Katika hotuba yake, Katibu Mkuu aliwataka watu wanaomiliki silaha nchini isivyo halali kuzisalimisha haraka iwezekanavyo kabla ya operesheni ya kuwakamata haijaanza.
ge2
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wa Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam, kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu ili aweze kuifungua warsha hiyo ya siku mbili.
ge3
Mwakilishi wa Katibu Mtendaji wa  Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika Mapambano ya Kuzuia na Kudhibiti Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA), Esaka Mugasa akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wa Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Watatu kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira na wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara hiyo, Marlin Komba. Katibu Mkuu katika hotuba yake ya ufunguzi wa warsha hiyo, aliwataka watu wanaomiliki silaha nchini isivyo halali kuzisalimisha haraka iwezekanavyo kabla ya operesheni ya kuwakamata
ge4
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (wapili kulia) akitoka katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam mara baada ya kufungua Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara hiyo, Marlin Komba, wapili kushoto ni Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi-Makao Makuu, Hezron Gyimbi na kulia ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Yusuph Ilembo.
ge5
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akizungumza na wajumbe wa Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake, Katibu Mkuu aliwataka watu wanaomiliki silaha nchini isivyo halali kuzisalimisha haraka iwezekanavyo kabla ya operesheni ya kuwakamata haijaanza
ge6
Sehemu ya wajumbe wa Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza na wajumbe hao katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam kabla ya kuwafungulia warsha yao ya siku mbili itakayojadili umasishaji wa Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha ya Mwaka 2015. Hata hivyo, katika hotuba yake, Katibu Mkuu aliwataka watu wanaomiliki silaha nchini isivyo halali kuzisalimisha haraka iwezekanavyo kabla ya operesheni ya kuwakamata haijaanza
ge7
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati waliokaa), Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara hiyo, Marlin Komba (wapili kushoto waliokaa), Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi-Makao Makuu, Hezron Gyimbi (wapili kulia), Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Yusuph Ilembo (kulia) na kushoto ni Mwakilishi wa Katibu Mtendaji wa  Baraza la Mawaziri wa Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika katika Mapambano ya Kuzuia na Kudhibiti Uzagaaji wa Silaha Haramu (RECSA), Esaka Mugasa, wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Warsha ya Kuhamasisha Sheria Mpya ya Udhibiti wa Silaha na Risasi. Warsha hiyo ya siku mbili ilifunguliwa na Katibu Mkuu, Rwegasira katika Ukumbi wa Bwalo la Maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

WAKAZI WA RUFIJI MKOANI PWANI WAKUMBWA NA MAFURIKO WAKOSA SEHEMU YA KUISHI

bb
Na Tabu Mullah
WANANCHI  zaidi ya 5000 katika Wilaya ya rufiki Mkaoani Pwani kwa sasa  hawana mahali pakuishi kutokana na nyumba zao kukumbwa na mafuriko kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali hapa nchini.  
 Kufuatia kutokea kwa mafuriko hayo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injiania Evarist Ndikilo amekwenda katika eneo la tukio  na kujionea athari zilizojitokeza kwa wananachi hao wa wilyani rufiji kutokana na mvua hizo zilizosaababisha mafuriko.
Akizungumza na wahanga wa mafuriko hayo Ndikio alisema kwamba kutokana na hai hiyo serikali Mkoa wa Pwani imechukua hatua za haraka kuwasaidia wananci hao kwa kutoa chakula cha dharura tani 1283 za mahindi kwa ajili ya wananchi hao.
 
Ndikilo alisema kuwa  mbali na serikali kutoa tani hizo za mahindi pia imetoa mbegu za mahindi tani 10 sambamba na tani 5 za mtama ambazo zinastawi kwa kipindi cha mudamfupi ii wannaachi waweze kuzipanda katika ukanda wa juu ii ziweze kuwasaidia katika upatikanaji wa chakula.
“Kwanza kabisa mimi nawapa pole wale wote ambao wamepata na maafa haya ya mafuriko na wengine kukosa sehemu ya kuishi lakini nataka kuwahakikishia kuwa serikali yenu ipo pamoja nanyi katika kuhakikisha unawasaidia huduma zote muhimu ambazo zinastaili ikiwemo kuwapatia chakula kw ahiyo msiwe na hofu yoyote,”
 
“Lakini ombi langu kubwa kwa kipindi hiki kwa wanaanchi ni kuwa makini sana kwani mvua bado zinaendelea kunyesha na na zimeleta maafa makubwa kama mnavyoona kwa hiyo cha msingi kama kuwa wnanchi bado wanaendelea na shughuli za kulima karibu na mabonde ya mito wasiendelee kulima  katika maeneo hayo kwani wanaweza kusombwa na maji,”alifafanua Ndikilo.
Pia Ndikio aliwaomba wahanga hao wa mafuriko kuhakikisha wanakitumia vizuri chakula amabcho kimetolewa na serikali kwani katika kipindi hiki uende mahitaji ya chakula yakaongezeka zaidi kutokana na mahitaji mwengi ya wananchi wenywe hivyo ni vema kuwa na matumizi mazuri.
 
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa alisema kwa sasa kazi kubwa inayofanywa na serikali ni kutoa elimu kwa wananachi na kuwahamasisha wale wote waliokumbwa na mafuriko watoke mara moja katika maeneo ya  mashamba kwani ni hatari kwa masiha yao pindi mvua inaponyesha.
Akizungumzia kuhusina na baadhi ya wafanyabiashara amabo wamekuwa na tabia ya kupandisha bei ya vyakula pindi wnapoona maafa kama hayo yamejitokeza waacha mara moja kufanya hivyo kwani ni kwakandamiza wananchi.
 ” Wafanyabiashara wasiowaungwana wasitumie janga hili kujinufaisha kwa kupandisha bei ya vyakula, kwa kutambua hilo tumewapa vibali wafanyabishara 6 wenye uwezo ili wanunue  tan 10 za mahindi na kusaga unga na kuwauzia wananchi kwa bei nafuu kwa jimbo la kibiti na ikwiriri,” alisema.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Rufiji Nurdin Babu aibainisha kuwa kutoka ana mvua hizo zinazoendelea kunyesha tayari jumla ya hekta 8138.4 za mpunga na tani 7171.2 za mahindi zimeathirika na maji na kuwa mazao hayo yalikuwa katika hatua za mwisho kwa ajii ya kuvunwa.
Babu aliongeza mafuriko  yaliyotokea katika wilaya yake  yalianza tangu  juzi usiku na kuvikumba vijiji mbali mbali ikiwemo kijiji cha uwe na mhoro na kusababisha daraja la muhoro kuvunjika na hivyo wananchi kuvuka kwa kutumia mitumbwi pamoja na  boti.

Rais Magufuli ampa pole mke wa Waziri mkuu Mstaafu mama Tunu Pinda

tunu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za pole Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda aliyepatwa na ajali ya gari, iliyotokea jana tarehe 08 Februai, 2016 akiwa safarini kutoka Dodoma kwenda Dar es salaam.
Ajali hiyo imetokea katika eneo la Mkundi lililopo katika Manispaa ya Morogoro ambapo gari aliyokuwa akisafiria Mama Tunu Pinda, ilipinduka baada ya kumgonga mwendesha pikipiki aliyeingia ghafla barabarani.

Katika salamu hizo alizozituma kupitia kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko taarifa za kutokea kwa ajali hiyo na amemuombea Mama Pinda na Majeruhi wengine kupona haraka.

“Kupitia kwako Mheshimiwa Waziri Mkuu Mstaafu Pinda, naomba unifikishie pole nyingi kwa mkeo Mama Pinda kwa kuumia katika ajali hii, na namuomba Mwenyezi Mungu awaponye majeruhi wote ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku” alisema Rais Magufuli.
Mama Tunu Pinda anaendelea kupata matibabu Jijini Dar es salaam, na hali yake inaendelea vizuri.

No comments:

Post a Comment