Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein
Katanga akitoa shukrani baada ya kupokea mfano wa hundi aliyopokea kwa
lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar es salaam. Katikati ni Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na kulia ni
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
Baadhi ya waandishi wa habari
wakiendelea na kazi yao wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO
………………………………………………………………………………………………………..
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO.
Dar es salaam.
Serikali imeikabidhi Mahakama ya
Tanzania kiasi cha Sh.bilioni 12.3 zilizoahidiwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Maadhimisho
ya Siku ya Sheria kwa lengo la kuiwezesha Mahakama kuimarisha utendaji
kazi na kutekeleza majukumu yake inapasavyo.
Akikabidhi fedha hizo mbele ya
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Fedha na Mipango
Dkt. Philip Mpango amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa kwa Mahakama ni
mwitikio wa kutekeleza ahadi ya Rais aliyoitoa wakati wa maadhimisho ya
Siku ya Sheria Duniani Januari 4, 2016.
“Ni matumaini ya Serikali fedha hizo zitatumika vizuri na zitatumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa” alisema Dkt. Mpango.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu
Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju amemshukuru Mhe. Rais kwa kwa
kutekeleza ahadi aliyoitoa ndani ya siku nne na kuudhihirishia umma kuwa
kauli mbiu ya “Hapa Kazi Tu” anaisimamia kwa vitendo.
Naye Mtendaji Mkuu wa Mhakama
Hussein Katanga amesema kuwa fedha walizokabidhiwa zitasaidia ujenzi wa
mahakama nchini na zipo ndani ya bajeti ya mwaka 2015/2016 na
watazitumia kulingana na malengo yaliyokusudiwa.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu yatoa taarifa ya mfumuko wa bei leo
Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na
Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ephrahim Kwesigabo
akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa
taarifa ya hali ya mfumuko wa bei mapema hii leo jijini Dar es Salaam,
kulia ni Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira Bi. Ruth Minja.(Picha zote na
Eliphace Marwa – Maelezo)
Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira
toka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Ruth Minja akifafanua jambo kwa
waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa taarifa ya hali ya
mfumuko wa bei mapema hii leo jjijjini Dar es Salaam, kushoto ni
Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya
Takwimu, Ephrahim Kwesigabo.
Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na
Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ephrahim Kwesigabo
akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa
taarifa ya hali ya mfumuko wa beimapema hii leo jijini Dar es Salaam,
kulia ni Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira Bi. Ruth Minja.
Na Kalonga Kasati
Matumizi ya kaya kwenye biadhaa
za vyakula imepungua hadi asilimia 38.5 mwaka 2011/12 kutoka asilimia
47.8 ya mwaka 2007.ambapo kwa ujumla wake mfumuko wa Bei umepungu
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi
wa Takwimu za jamii na Sensa ya Watu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu,
Bw. Ephraim Kwesigabo alipokuwa akizunguza na waandishi wa habari kuhusu
mfumuko wa bei leo jijini Dar es Salaam.
Kwesigabo alisema kuwa kutokana
na mwenendo huo kunaashiria kupungua kwa Umasikini Wa kipato kwenye kaya
kwa kuelekeza matumizi mengine bidhaa zisizo za vyakula kama usafiri,
mawasiliano, makazi, maji na nishati.
“Matokeo yanaonyesha kwamba
mizania ya matumizi ya kaya kwenye bidhaa za vyakula imepungua hadi
asilimia 38.5 mwaka 2011/12 kutoka asilimia 47.8 mwaka 2007” Alisema
Kwesigabo.
Aliongeza kuwa makundi mengi
mengine yaliyoonyesha kuwa na mizania mikubwa ya Matumizi ya kaya mwaka
2011/12 kuwa ni pamoja na Usafi asilimia 12.5 kutoka asilimia 9.5 Mwaka
2007, Makazi Maji na Nishati asilimia 11.6 kutoka asilimia 9.2 mwaka
2007 na Mavazi na Viatu asilimia 8.3 kutoka asilimia 6.7 mwaka 2007.
Aidha kumekuwa na ongezeko la
Zaidi ya mara mbili ya matumizi ya kaya kwenye kundi la Mawasiliano
asilimia 5.6 ikilinganishwa na asilimia 2.1 ya mwaka 2007
Kwa upande wake Meneja wa Takwimu
za Bei na Ajira kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bibi. Ruth Minja
amevitaja baadhi ya vigezo muhimu vinavyotumika kupata Fahirisi za Bei
zinzoonyesha uhalisia wa matumizi ya kaya binafsi kuwa ni pamoja na
mizania katikia bidhaa na huduma muhimu ikiwemo Vyakula, afya, Usafiri
,Maji na Nishati.
Aliongeza kuwa ili kupata matokeo
ya mfumuko wa Bei kumekuwa na mtindo wa kufanya marejeo baada ya kila
miaka mitano ambapo marejeo ya mwisho yalifanyika mwaka 2007 na
kuonyesha matumizi makubwa ya kaya yalikuwa kwenye bidhaa za vyakula
zikiwa na asilimia 47.8 ya matumizi yote yakifuatiwa na usafiri asilimia
9.5 huku matumizi madogo zaidi Yalikuwa ni huduma za afya kwa asilimia
0.9.
Takwimu hizi zimekuwa zikitolewa
kwa mujibu wa sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 na Zimekuwa zikisaidia
katika kupima na kuboresha sera za kifedha na mipango ya kiuchumi ya
kuthibiti mfumuko wa bei, kukadiria pato la Taifa,kuboresha mishahara ya
wafanyakazi na Mafao ya wafanyakazi waliostaafu.
TAARIFA KUHUSU MKUTANO WA WADAU WA UWEZESHAJI UTAKAOFANYIKA TAREHE 9/02/2016
Baraza la Taifa la Uwezeshaji
Wananchi Kiuchumi (NEEC) lilianzishwa mwaka 2005 kwa Sheria ya Taifa ya
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (Sheria na. 16 ya Mwaka 2004) chini ya
Ofisi ya Waziri Mkuu. Baraza ni chombo cha juu kitaifa cha kuratibu,
kusimamia, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Sera ya Taifa ya
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004.
Katika kutekeleza Sera ya Taifa
ya Uwezeshaji, Baraza limeshaandaa Mkakati wa Taifa wa Uwezeshaji
Wananchi Kiuchumi na Mwongozo wake unaohusisha sekta zote nchini. Ili
kufanikisha utekelezaji wa mkakati huo, Baraza limeandaa Mkutano wa
Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ambao ni muundo rasmi katika
kutekeleza Mkakati wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. Mkutano huu ni
sehemu ya Uratibu na utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji ambao
unahusisha wadau mbali mbali ambao ni Wizara, Idara na Taasisi za
Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa, mashirika yasiyo ya kiserikali
na sekta binafsi.
Mkutano huu wa Wadau wa
Uwezeshaji utafunguliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mh Majaliwa Kassim Majaliwa (MB), tarehe 9/02/2016 katika
Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere.
MAJUKUMU YA BARAZA
- Kuandaa Mpango Mkakati wa Kisekta na kuhamasisha matumizi ya rasilimali kwa shughuli za uwezeshaji wananchi;
- Kuhamasisha na kuhimiza uwekaji wa akiba, uwekezaji na ushirikishwaji makini wa wananchi kwenye shughuli za kiuchumi;
WAZIRI UMMY MWALIMU AWASHUKIA WANAOTOA HUDUMA ZA AFYA KINYUME CHA SHERIA
N
Dar es salaam
Na Kalonga Kasati
Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameyataka Mabaraza na Bodi
za kitaalamu za masuala ya afya kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya
wataalam na vituo vinavyotoa huduma za afya kinyume cha Sheria.
Waziri Ummy ametoa agizo hilo
alipokuwa akizindua Baraza la Optimetria, Baraza la wataalamu wa
Radiolojia pamoja na Bodi ya Maabara binafsi leo jijini Dar es salaam.
Alisema kisheria Mabaraza na Bodi
za Kitataalam ndivyo vyombo vinavyofuatilia ubora wa huduma za Afya
pamoja na kutoa elimu kwa wananchi kuwaepuka watoa huduma batili
wasiokuwa na utaalam na ujuzi wala kukidhi vigezo vya utoaji huduma
vilivyowekwa kisheria.
“Siku hizi kumekuwa na matumizi
makubwa ya vyeti vya kugushi vikiwemo vya vituo vya kutolea huduma na
wataalamu, watu wasio na taaluma wanatoa huduma kinyume na sheria hivyo
Mabaraza na Bodi mna mamlaka ya kuwachukulia hatua za kinidhamu,”
Alisema Waziri Ummy.
Aidha, alisema kuwa Serikali
haitasita kuyachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuvunja Bodi au
Mabaraza yatakayoshindwa kutekeleza majukumu yaliyoainishwa katika
sheria iliyohusika kuyaanzisha.
Aliyataka mabaraza hayo
kuhakikisha kuwa yanatoa Elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari
ili kuhakikisha wananchi wanakuwa na ufahamu kuhusu huduma bora za afya
zitolewazo na wataalamu husika.
“Wananchi wakielimishwa wataepuka
watoa huduma batili wasiokuwa na utaalamu na ujuzi hivyo mabaraza na
Bodi vinapaswa kuhakikisha mambo haya hayatokei kwani vinauwezo mkubwa
wa kufuatilia masuala haya kwa mujibu wa Sheria”alifafanua Waziri Ummy.
Akizungumza kuhusu utendaji kazi
wa wataalamu hao Waziri Ummy amewataka wataalamu hao kujiendeleza
kielimu kwani utaalamu bila kuwa na ujuzi ni butu hivyo suala la elimu
lipewe kipaumbele.
Mbali na hayo Waziri ameitaka
Mabaraza na Bodi kuhakikisha wataalamu wote, vifaa na vitendanishi
vinasajiliwa kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa.
No comments:
Post a Comment