Saturday 27 February 2016

Rais Mpya Wa FIFA ni Gianni Ifantiano

fi1
Gianni Infantino ndiye aliyechaguliwa kuwa rais mpya wa shirikisho la soka duniani Fifa
Raia wa Switzerland Gianni Infantino amechukua mahala pake Sepp Blatter kama rais wa shirikisho la soka duniani Fifa.katibu huyo mkuu wa Fifa alipata kura 115 katika raundi ya pili ikiwa ni kura 27 zaidi ya mpinzani wake wa karibu Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa.
Mwanamfalme Ali bin al-Hussein alikuwa wa tatu akiwa na kura nne huku Jerome Champagne akishindwa kupata hata kura moja. Tokyo Sexwale alijiondoa kabla ya kura kuanza kupigwa mjini Zurich.
fi2
Infantino akiwashukuru wajumbe wa Mkutano Mkuu wa FIFA
Raundi ya kwanza ya upigaji kura ilishindwa kum’baini mshindi wa moja kwa mojaWingi wowote wa kura[zaidi ya aslimia 50] katika raundi ya pili ya uchaguzi huo ulikuwa unaweza kumwezesha mgombea kutangazwa mshindi katika raundi ya pili.
Infantino ni wakili mwenye umri wa miaka 45 kutoka eneo la Brig jimbo la Valais nchini Switzerland ,ikiwa ni eneo lililopo chini ya maili sita kutoka nyumbani kwa Blatter.
Blatter ambaye aliliongoza shirikisho hilo tangu mwaka 1998 alijiondoa mwaka uliopita kabla ya kupigwa marufuku katika shughuli zozote za kandanda kwa kipindi cha miaka sita .
FI3
Infantino akiwahutubia wajumbe
Baada ya kutangazwa mshindi, Infantino aliwaambia wajumbe waliopiga kura kwamba hakuweza kujielezea kutokana na hisia alizokuwa nazo.
Lakini aliwaambia wajumbe kwamba ”kwa pamoja wataweza kuirudisha sura ya Fifa na heshima ya Fifa’

MWANAMUZIKI WA ZAMANI KASSIM MAPILI AZIKWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

map1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akiweka udogo kwenye kaburi la Mwanamuziki mkongwe hapa nchini, Mzee Kassim Said Mapili, wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye Makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo.
map2
Mwili wa mwanamuziki mkongwe hapa nchini, Mzee Kassim Said Mapili ukiwasili kwenye makabuli ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo.
map3
Mwili wa mwanamziki mkongwe hapa nchini, Kassim Said Mapili ukiwekwa katika kabuli wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makabuli ya Kisutu, jijini Dar es Salaam leo.
map4
Waombolezaji waliofika kumsindikiza kwenye nyumba ya milele  Mzee Kassim Said Mapili, wakipata mawaidha baada ya mazishi.
  Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akimfariji mtoto wa marehemu
  Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akimfariji mtoto wa marehemu
  Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akipeana mikono na mwanamuziki mkongwe Mjusi Semboja huku akiongea na Mzee Makassy na wanamuziki wengine
 Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akiongea na mchambuzi wa muziki wa dansi mahiri Zomboko na mdau wa muziki Hassan.

MAJALIWA AKUTANA NA VIONGOZI WA DINI

d02
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa dini kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salam Februari 26, 2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d01 d1
 Baadhi ya viongozi wa dini wanaunda kamati ya amani ya Dar es salam na baadhi ya mikoa nchini wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d2
 Baadhi ya viongozi wa dini wanaunda kamati ya amani ya Dar es salam na baadhi ya mikoa nchini wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa KKKT Mstaafu, Elinaza Sendoro baada ya kuzungumza na Viongozi wa Dini kwenye Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mkuu wa KKKT Mstaafu, Alex Molasses baada ya kuzungumza na Viongozi wa Dini kwenye Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d5
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini baada ya kuzungumza nao kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyererejijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d6
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini baada ya kuzungumza nao kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyererejijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
d7
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini baada ya kuzungumza nao kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyererejijini Dar es salaam Februari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAWAZIRI WOTE WAJAZA TAMKO LA MALI NA MADENI

c38d70b6-1ea3-40f3-a8b2-95c9813523f8
Na Kalonga Kasati
 Waziri MKUU Kassim Majaliwa amesema agizo lilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli la kuwataka mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wakamilishe kabla ya saa 12 leo jioni limetekelezwa.

Waziri Mkuu amepokea barua kutoka kwa Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji (Mst.) Salome Kaganda ikithibitisha kuwa mawaziri na naibu mawaziri wote wametekeleza agizo hilo.

“Hadi kufikia saa 9.30 leo alasiri (Ijumaa, Februari 26, 2016) mawaziri wote walikuwa wamekamilisha fomu zao za kuzikabidhi katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma,” alisema Waziri Mkuu.

Rais Magufuli leo asubuhi alitoa maelekezo kwamba Mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni ifikapo leo Ijumaa tarehe 26 Februari, 2016 saa 12.00 jioni wawe wamejaza na kurejesha Fomu ya Tamko la Rasilimali na Madeni katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam. Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake.

No comments:

Post a Comment