Monday 15 February 2016

Waziri wa Elimu Sayansi Tecknolojia na Ufundi Pro Joyce Ndalichako Aongoza Mamia katika Mazishi ya Waziri wa Elimu wa zamani Isalia Elinewinga

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ,Baba Askofu Dkt Fredrick Shoo akitoa heshima ya mwisho kwa marehemu Isalia Elinewinga wakati wa shughuli ya Mazishi iliyofanyika kijiji cha  Losaa Masama Magharibi wilayani Hai.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Isalia Elinewinga.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Anthony Mtaka akitoa heshima za mwisho kwa Waziri wa Elimu wa zamani ,Isalia Elinewinga aliyezikwa nyumbani kwake kijiji cha Losaa wilaya ya Hai.
Baadhi ya waombolezaji walifika kwenye msiba huo.
Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi ,Prof Joyce Ndalichako akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Amosi Makala wakiwa katika mazishi ya Marehemu Isalia Elinewinga.nyuma yao ni Mkuu wa wilaya ya Hai,Anthony Mtaka.
Mbunge wa Jimbo la Hai,Freeman Mbowe pamoja na Mkewe Dkt Lilian Mtei wakiwa katika mazishi ya Marehemu Elinewinga.
Familia ya Marehemu Elinewinga wakiwa wenye huzuni kando ya Jeneza lenye Mwili wa Mpendwa Baba yao mzee Isalia Elinewinga.


Siku 100 Za JPM Usafi Wapewa kipaumbele.

REUTERS1083589_Articolo
Na Kalonga Kasati
Mnamo tarehe 5 Novemba 2015 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilishuhudia Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano katika sherehe zilizofanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam. Huu ndio ulikuwa mwanzo mpya wa Tanzania ya uwajibikaji na maendeleo ya mtu wa hali ya chini ambayo watanzania wengi walisubiri kwa muda mrefu vizazi na vizazi kuiona.

Siku 100 tangu Rais wa awamu ya tano aiingie madarakani mambo mengi yametiliwa mkazo kama vile Elimu, Afya, Biashara, Viwanda,Kilimo,Ufugaji,Uvuvi na mengine mengi ambayo serikali imeamua kuyaangalia kiundani zaidi ili kufanikisha azma yake ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Katika makala hii tuangalie jinsi uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano katika siku 100 ulivyojikita  kuimarisha usafi wa mazingira ili kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yanayotokea mara kwa mara katika mikoa mbalimbali nchini kwa kuhamasisha usafi katika maeneo hayo. Hapa tunamsikia Mhe. Rais John Pombe Magufuli akisema, “Hatuwezi kufanya sherehe huku watu wetu bado wanakufa kwa ugonjwa wa kipindupindu ambao unatokana na uchafu, badala yake nchi nzima tufanye usafi siku hiyo”.

Kwa kuliona hilo kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alitangaza rasmi kuwa siku ya tarehe 9 Desemba mwaka 2015, itakuwa ni siku ya uhuru na kazi na maadhimisho ya miaka 54 ya  Uhuru wa Tanganyika  kuwa yatafanyika kwa watu kufanya usafi katika maeneo yao siku hiyo, ikiwa ni jitihada za Serikali kuimarisha usafi na kupambana na magonjwa ya mlipuko kama vile Kipindupindu.

Kero ya uchafu ilimfanya Mhe. Rais kufanya tendo la kihistoria ambalo halijawahi kufanyika kwa takribani zaidi ya nusu karne ya uhai wa Tanzania. Tukio hili ni kuhamisha maadhimisho tuliozoea ya kuona gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama pamoja na halaiki na lakini sasa tunashuhudia machepe, troli, ndoo, fyekeo na zana nyinginezo za usafi zikitumika siku hiyo. Ama kweli Dr. Magufuli ni kiongozi mwenye uthubutu.

Naibu Waziri  Wa Afya DK. Kigwangalla Aupa  Siku 90 Uongozi Wa  Hospitali Ya Mkoa Wa Njombe

DSC_0068

Naibu Waziri Dk. Kigwangalla akikagua mahabara ya hospitali hiyo ambayo alikutana na matatizo mbalimbali ikiwemo mashine na vifaa kutotumika ipasavyo na kuagiza uongozi wa kufanya maboresho ndani ya miezi mitatu huku akiahidi kuifungia endapo itashindwa kutekeleza maagizo hayo.

kigwangaccszz

Naibu Waziri wa Afya, Dk Kigwangalla akiangalia moja ya maeneo ya wodi hizo ambapo alikuta hali ya uchafu pamoja na kuwa na mpangilio mbovu wa namna ya utoaji wa huduma.

kigwanj

Dk. Kigwangalla akitoa maelezo kwa Mganga mkuu wa hospitali ya Mkoa wa Njombe-Kibena, Dk. Samwel Mgema wakati wa maagizo hayo ndani ya siku 90 na endapo hawatafanya utekelezaji ataichukuia hatua ya kuifungia.

kigwaza

Naibu Waziri wa Afya, Dk Kigwangalla akielekea kwenye baadhi ya majengo ya hospitali hiyo wakati wa ukaguzi huo.

Kigwangala

Naibu Waziri wa Afya, Dk Kigwangalla akikagua eneo la kutolea huduma ikiwemo wagonjwa Wanaoingia kumuonna Daktari.

Uongozi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Njombe umepewa muda wa siku 90 kurekebisha mapungufu ya utoaji wa huduma za afya, lazima hospitali hiyo itafungwa.
Kauli hiyo imetolewa jana jioni na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na viongozi Mganga Mkuu wa Mkoa, Samwel Mgema na na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Imelda Mwenda na watumishi wa hospitali hiyo.
 
Dkt. Kigwangalla alitoa agizo kufuatia ziara yake ya ukaguzi wa hospitali, vituo vya afya na zahati ili kuweza kubaini changamoto na mafanikio waliyoyapata baada maagizo mbalimbali kutolewa na Serikali.
 
Miongoni mwa maagizo hayo ni uboreshaji wa huduma kwa kuwepo na vifaa tiba na vya maabara za kisasa, dawa za kutosha, kuaanza malipo ya mtandao.
Katika ziara hiyo Naibu Waziri huyo alibaini kwamba hospitali hiyo haina baadhi ya vifaa vya maabara, ambavyo ni muhimu kwa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali, ikiwemo mashine ya CT-Scan na kuwepo kwa vifaa vibovu ambayo havijafanyiwa matengenezo, ukiwemo mfumo mbovu wa ukusanyaji taka ngumu na nyepesi.
 
“Sijaridhishwa na uendeshaji wa hospitali hii na utoaji wa huduma zinazotolewaa ninakuagiza Mganga Mkuu wa Wilaya, John Luanda kurekebisha mapungufu yaliyopo baada ya miezi mitatu nitarudi nikikuta huduma bado hairidhishi nitakifunga kituo.,” alisema Dkt.Kigwangalla.
 
Aliongeza kuwa akikuta huduma hadhirishi atafunga hospitali hiyo licha ya kuwa ya Serikali, hivyo hatasubiri kutumbuliwa jipu.
 
Dkt. Kigwangalla aliutaka uongozi wa hospitali hiyo kuandaa mpango kazi na mkakati wa kuboresha mapungufu yaliyopo katika hospitali hiyo na kuuwasilisha kwake.
Aliutaka uongozi wa hospitali huo kujenga chumba cha upasuaji cha wakina mama na watoto.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa Njombe, Mgema alisema watatekeleza maagizo hayo.

No comments:

Post a Comment