Tuesday 16 February 2016

Mkurugenzi Bodi ya Mikopo afukuzwa kazi

NDE
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof.Joyce Ndalichako akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Tarishi Maimuna Kibenga. Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO

Na Kalonga Kasati
Waziriwa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi Prof.Joyce Ndalichako amesitisha mkataba wa ajira wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo, George Nyatega pamoja nakuwasimamisha kazi Wakurugenzi watatu.

Ameyasema hayo leo Jijini Dar es salaam alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu matatizo ya kiutendaji na matumizi mabaya ya fedhazaUmmayanayofanyikaBodiyaMikopo.

Prof.Joyce Ndalichako amesema kuwa Taasisi ya Bodi ya Mikopo imeonesha utendaji usioridhisha kiasi kwamba kumekuwa na matatizo mengina yanayojirudiarudia kwa wateja wao mara kwa mara.

“Mikopo kwa wanafunzi imekuwa ikichelewa kuwafikia bila sababu za msingi kiasi kwamba imejengeka taswira kwa wanafunzi kwamba hadi walalamike wizara ni ndipo matatizo yao yashughulikiwe hivyo, tatizo sio ukosefu wa fedha bali ni uzembe wa watendaji katika kuwapatia wanafunzi mikopo yao kwa wakati.”AlisemaNdalichako.

Amewataja watumishi aliowasimamisha kazi kuwa ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Yusuph Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaj iMikopo Juma Chagonja pamoja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo Onesmo Laizer.

Aidha,amezitaja baadhi ya sababu zilizosababishwa kufukuzwa na kusimamishwa kazi kwa watumishi hao zikiwemo za kufanya malipo yasiyo sahihi kwa baadhi ya wanafunzi wanaosoma ndani na nje ya nchi pamoja udhaifu uliobaini kakatika mifuko ya fedha.

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu inajukumu la kutoa mikopo kwaajili ya wanafunzi wa elimu ya juu na kusimamia urejeshaji wa mikopo hiyo, kwa mwaka wa masomo 2015/2016 jumla ya Shillingi Bilioni 459 imetolewa mikopo kwa wanafunzi 122,486 wanaosoma katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Kiingilio Cha Simba, Yanga Elfu Saba

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo limetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Jumamosi kati ya watani wa jadi Simba SC dhidi ya Yanga SC utakaochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, huku kiingilio cha chini kikiwa ni Shilingi elfu saba tu (7,000).

Kiingilio cha juu cha mchezo huo kitakua shilingi Elfu Thelathini (30,000) kwa VIP A, Elfu Ishirini (20,000) VIP B & C, Elfu Kumi (10,000) kwa viti vya rangi ya machungwa (Orange), na Elfu Saba (7,000) kwa viti vya rangi ya bluu na kijani.

Tiketi za mchezo huo zitaanza kuuzwa siku ya Ijumaa saa 2 kamili asubuhi katika vituo vya TFF (Karume), Buguruni Olicom, Ubungo Oilcom, Kidongo Chekundu (Mnazi Mmoja), Posta (Agip), Dar Live (Mbagala), Uwanja wa Taifa, Makumbusho Stand, Kivukoni Ferry.

Mchezo huo utachezeshwa na waamuzi wote wenye beji za FIFA, mwamuzi wa katikati Jonesia Rukyaa (Kagera), akisaidiwa na Josephat Bulali (Tanga), Samwel Mpenzu (Arusha), mwamuzi wa akiba Elly Sasii (Dar) huku Kamisaa wa mchezo huo akiwa Khalid Bitebo (Mwanza).

Ligi hiyo ya Vodacom itaendelea Jumamosi kwa michezo sita, Young Africans v Simba (Taifa), Mbeya City v Azam (Sokoine), Stand United v JKT Ruvu (Kambarage), Toto Africans v Kagera Sugar (CCM Kirumba), Mgambo Shooting v Tanzania Prisons (Mkwakwani) na Majimaji FC v Mtibwa Sugar (Majimaji).

Jumapili ligi hiyo itaendelea kwa michezo miwili, Mwadui FC v Coastal Union uwanja wa Mwadui Complex, huku Ndanda FC wakicheza dhidi ya African Sports uwanja wa Nagwanda Sijaon mjini Mtwara.

No comments:

Post a Comment