Monday, 8 February 2016

KAMUSOKO MCHEZAJI BORA MWEZI DISEMBA

Mchezaji Thaban Kamusoko amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa mwezi Disemba, 2015 baada ya kumshinda mchezaji mwenzake wa Yanga (Amissi Tambwe).
Kamusoko ameisaidia timu yake ya Yanga katika michezo iliyochezwa mwezi Disemba kwa kushiriki dakika zote katika michezo mitatu iliyochezwa mwezi wa Disemba.
Kwa kuchaguliwa kwake kuwa mchezaji bora wa wa mwezi Disemba, Kamusoko atakabidhiwa zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni moja (1,000,000) kutoka kwa wadhamini wa ligi Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.

MAHAKAMA YAPOKEA SH. BILIONI 12.3 ZILIZOAHIDIWA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT.JOHN POMBE MAGUFULI.

mah1
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga (kushoto) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju.
mah2
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju (kulia) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga.
mah3
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (katikati) akiongea na waandishi wa habari wakati wa makabidhiano ya fedha zilizotolewa kwa Mahakama leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju na kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (kushoto).
mah4
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju (kulia) akitoa shukrani baada ya kupokea mfano wa hundi aliyopokea kwa lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
mah5

No comments:

Post a Comment