KAMUSOKO MCHEZAJI BORA MWEZI DISEMBA
Mchezaji Thaban Kamusoko
amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa mwezi
Disemba, 2015 baada ya kumshinda mchezaji mwenzake wa Yanga (Amissi
Tambwe).
Kamusoko ameisaidia timu yake ya
Yanga katika michezo iliyochezwa mwezi Disemba kwa kushiriki dakika zote
katika michezo mitatu iliyochezwa mwezi wa Disemba.
Kwa kuchaguliwa kwake kuwa
mchezaji bora wa wa mwezi Disemba, Kamusoko atakabidhiwa zawadi ya fedha
taslimu shilingi milioni moja (1,000,000) kutoka kwa wadhamini wa ligi
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
MAHAKAMA YAPOKEA SH. BILIONI 12.3 ZILIZOAHIDIWA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT.JOHN POMBE MAGUFULI.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.
Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein
Katanga (kushoto) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya fedha hizo
mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.
Philip Mpango (katikati) akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba
na Sheria Amon Mpanju (kulia) mfano wa hundi wakati wa makabidhiano ya
fedha hizo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.
Philip Mpango (katikati) akiongea na waandishi wa habari wakati wa
makabidhiano ya fedha zilizotolewa kwa Mahakama leo jijini Dar es
salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon
Mpanju na kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango (kushoto).
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya
Katiba na Sheria Amon Mpanju (kulia) akitoa shukrani baada ya kupokea
mfano wa hundi aliyopokea kwa lengo la kusaidia mahakama leo jijini Dar
es salaam. Kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
No comments:
Post a Comment