Mtendaji Mkuu kutoka Taasisi ya Sanaa na
Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Hubert Makoye akifundisha mada ya
umuhimu wa weledi na taaluma katika filamu kwa washiriki wa warsha
walioshiriki mafunzo ya kujengewa uwezo wadau wa sekta ya filamu leo
Mkoani Mara.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao akizungumza na washiriki
wa mafunzo ya kujengewa uwezo wadau wa sekta ya filamu (hawapo pichani)
wakati wa warsha ya mafunzo hayo leo Mkoani Mara
Mshiriki wa warsha ya mafunzo ya
kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu Bw. Felix Mayoka akichangia
wakati wa warsha hiyo leo Mkoani Mara
Baadhi ya washiriki wa warsha ya mafunzo
ya kujengewa uwezo wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza
wakifuatilia kwa makini mada zilizokua zikiendelea wakati wa warsha hiyo
leo Mkoani Mara.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce
Fissoo akitoa ufafanuzi kwa wanakikundi alipokua akikagua majadiliano
yaliyokua yakiendelea katika vikundi wakati wa warsha ya kuwajengea
uwezo wadau wa sekta ya filamu leo Mkoani Mara.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Millao (mwenye koti la Blue)
akichezo ngoma maarufu ya wakurya ijulikanayo kwa jina la litungi wakati
wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya filamu na
michezo ya kuigiza leo Mkoani Mara. Kushoto ni Mtendaji Mkuu kutoka
Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Hubert Makoye
Picha na: Genofeva Matemu – WHUSM.
Wadau wa sekta ya filamu Mkoani Mara wametakiwa kuzingatia weledi na ubora wakati wa kuandaa filamu.
Na: Genofeva Matemu – WHUSM
Tarehe: 15/12/2016
Wadau wa sekta ya filamu na michezo ya
kuigiza Mkoani mara wametakiwa kushirikiana kwa pamoja kuwajibika na
kukuza tasnia ya filamu nchini kwa kuzingatia weledi na ubora wakati wa
kuandaa filamu kuanzia uandishi wa miswada ya filamu hadi pale filamu
inapokamilika.
Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji Bodi ya
Filamu Bibi. Joyce Fissoo wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea
uwezo wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza leo Mkoani Mara.
“Tumekua tukitoa filamu nyingi sana hadi
kuifanya Tanzania kuwa nchi ya pili kwa bara la Afrika katika kuzalisha
wingi wa filamu lakini filamu hizo hazizingatii weledi hivyo kuzifanya
zisiweze kuvuka mipaka ya nchi yetu” amesema Bibi. Fissoo
Akizungumza wakati wa warsha hiyo Mtendaji
Mkuu kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Hubert
Makoye amesema kuwa warsha za kuwajengea uwezo wadau wa filamu ni njia
mojawapo ya kuimarisha taaluma na kuinua vipaji hivyo ni vyema washiriki
wakatumia warsha hizo kuvuka hatua na kuwa na vitu vipya vya kuendeleza
tasnia ya filamu nchini.
Naye Rais wa shirikisho la filamu Tanzania
Bw. Simon Mwakifwamba amesema kuwa Serikali imeona uhitaji wa
kuwajengea uwezo wanatasnia wa filamu hivyo ni vyema mafunzo haya
yakachukuliwa kwa mtazamo chanya kwani kumekuwa na changamoto kubwa ya
masuala ya weledi kwa wanatasnia wa filamu nchini inayopelekea kuandaa
filamu nyingi zisizokuwa na ubora hivyo warsha iliyotolewa na Bodi ya
filamu Mkoani Mara imetoa fursa kwa wanatasnia kujengewa uwezo kwenye
masuala ya elimu na weledi vitakaowawezesha kuendana na soko la
ushindani la kitaifa na kimataifa.
Aidha Bw. Mwakifwamba ameyataka makampuni
mbalimbali nchini kujitokeza kuwekeza kwenye masuala ya filamu nchini
kwani filamu ni kiwanda kinachokua kwa kasi na kutoa ajira kwa vijana
wengi nchini.
Kwa upande wake muigizaji kutoka Tanzania
Drama and Film Arts Association (TDFAA) Bi. Jaqueline Frank amesema kuwa
wadau wa sekta ya filamu na michezo ya kuigiza wa Mkoa wa Mara wamekua
wakitumia vipaji vyao kuandaa filamu bila ya kuwa na weledi hivyo
mafunzo waliyoyapata yatawasaidia kuboresha kazi zao kwa kuziandaa kwa
weledi na ubora wa hali ya juu na kuziwezesha kuvuka mipaka ya Mkoa wa
Mara na hata nchi za jirani.
No comments:
Post a Comment