Saturday 24 December 2016

Miti mikali ya Christmas ya mastaa wa nje 2016

Krismas sio kula, kunywa wala kuvaa bali ni maadhimisho ya kuzaliwa kwa mwokozi Yesu Kristo mkombozi wa ulimwengu kwa mujibu wa imani ya Dini ya Kikristo. Mesia, Rabi, Emanuel hayo ni baadhi ya majina ambayo Yesu Kristo wa Nazareth alibatizwa enzi za uwepo wake hapa duniani kwa mujibu wa Kitabu Kitakatifu cha Biblia kinavyoeleza.
Kesho Wakristo wote ulimwenguni wanaungana kusherehekea kuzaliwa kwa mkombozi wao wa ulimwengu Emanuel yaani Mungu pamoja nasi. Sherehe hizi huambatana na shamrashamra za kila aina ingawa kimsingi kwa mujibu wa mafundisho ya Dini ya Kikristo Krismas sio kusherehekea kwa kula, kunywa na kufanya anasa za dunia bali ni kuruhusu Kristo azaliwe upya ndani ya mioyo ya wanadamu.

Bwana Yesu alipozaliwa MamaJusi walimpelekea manemane na uvumba kwa kuwa waliamini ndiye Mfalme wa Wayahudi na Mkombozi wa Dunia na ndio sababu hata siku hizi ukipita maeneo mbalimbali unapokaribia msimu wa sikukuu hii utakuta mapambo ya kila aina. Sasa leo nimekusogezea miti mikali ya Krismas ya mastaa ambayo inaaminika ni mizuri zaidi kwa mwaka huu wa 2016.
 Mti wa Krismas wa Kylie Kristen Jenner ambaye ni mbunifu wa mavazi, mtangazaji wa tv na model nchini Marekani.
 Mti wa Krismas wa (nph) Neil Patrick Harris ambaye ni muigizaji, mtangazaji na mwanamuziki nchini Marekani.

 Mti wa Krismas wa Amber Rose
 
 Mti wa Krismas wa Beyonce.
 Mti wa Krismas wa Kourtney Kardashian, dada wa Kimkardashian
 Mti wa Krismas wa  Kim kardashian.
Mti wa Krismas wa Kris Jenner mama yake na Kim Kardashian.

No comments:

Post a Comment