Friday 30 December 2016

Barakah The Prince ataja anachokiona kwenye label ya WCB

Barakah The Prince ameisifia label ya WCB inayomilikiwa na Diamond Platnumz na kudai kuwa iko wazi inafanya vizuri.
Alikuwa akizungumza na mtangazaji wa Jembe FM, JJ.
“Wapo vizuri kwasababu wana empire yao, wana mashabiki wao wanafanya muziki wana mashabiki. Mtu yeyote ambaye yupo na empire yake na mashabiki wake ina maana anafanya kazi nzuri,” alisema muimbaji huyo.
“Kwahiyo wanajitahidi kufanya kazi nzuri na kuufikisha muziki sehemu,” aliongeza.

Hivi karibuni hitmaker huyo wa Siwezi alidai kuanzisha label yake mwenyewe iitwayo BANA na wasanii wa kwanza walio chini yake ni Lord Eyez na Naj.

No comments:

Post a Comment