Thursday 29 December 2016

Aunty Ezekiel aiachia sokoni filamu mpya ‘Christmas Eve

Mara nyingi kwenye msimu wa sikukuu za Christmas na mwaka mpya, waigizaji duniani huingiza sokoni filamu zinazoendana na wakati huo. Ni nadra sana kwa waigizaji wa Tanzania kuja na filamu za aina hiyo. Lakini si kwa Aunty Ezekiel, ambaye mwaka huu ameachia filamu iitwayo, Christmas Eve.
Muigizaji huyo na mama wa mtoto mmoja aliyezaa na dancer wa Diamond, Mose Iyobo, ameshirikiana waigizaji wengine wakiwemo Husna Iddy, Lissa Tarimo, Vivian Minja na wengine kucheza filamu hiyo.

“Usiamini kila kitu unachokiona au kusikia….. Kwasababu kila hadithi Ina pande Tatu yao, yako, Na ukweli,….. Christmas eve bonge LA movie iko mtaanii now …. Go get ur og copy,” ameandika muigizaji huyo kwenye Instagram.

No comments:

Post a Comment