Tuesday 27 December 2016

Ben wa bongo movie amepata ajali mbaya ya gari, alazwa Muhimbili

Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho,  Ben Branco Selengo amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari siku ya sikukuu ya Christmas.
Muigizaji Mboto ambaye ni rafiki wa karibu wa Ben, kupitia instagram ameandika:
Ajali ulioipata sio ndogo kwetu sisi wanadam, lakin kwa mungu ni ndooogo sana. Naamin ndogo kwa mungu kwasababu utapona kwa uwezo wake mungu. Utapona tu inshaallah (Benn Blanco Selengo)
Akiongea  ndugu wa karibu wa Ben kupitia simu ya Ben, alidai Ben alipata ajali mbaya ya gari juzi na hali yake bado ni mbaya.

“Ben hali yake siyo nzuri kusema kweli,” alisema dada huyo aliyejitambulisha kwa jina na Sarah. “Alipata ajali ya gari juzi na hapa tunapozungumza bado yupo Muhimbili hospitali,”

No comments:

Post a Comment