Friday 30 December 2016

Waziri Nchemba atembelea WCB

 Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba wiki hii alitembelea ofisi ya WCB iliyopo Tandale jiji Dar es salaam na kujionea uwekezaji uliofanywa na label hiyo ambayo ipo chini ya Diamond Platnumz.
Waziri huyo kijana aliweza kuzungumza na viongozi wa label hiyo na kuangalia namna ambavyo serikali inaweza kudhibiti wizi wa kazi za wasanii.
Baada ya kumaliza mazungumza hayo, Waziri Nchemba kupitia instagram yake aliandika:
#Wizi wa kazi za wasanii #Jeshi la polisi kuongeza nguvu

Pia alisema kuwa serikali haitasita kuwapa msaada pale watakapokwama na kuhitaji usaidizi wa serikali.

No comments:

Post a Comment