Thomas Ulimwengu Anazidi Kuzifuma Nyavu
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania,
Thomas Ulimwengu anaendelea kung’ara katika klabu yake ya TP Mazembe ya
Jamhuri ya Kongo, baada ya usiku wa Alhamisi kufunga bao katika ushindi
wa mabao 2-0 dhidi ya Shark XI FC.

Katika
mchezo huo wa Ligi Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo uliochezwa
kwenye Uwanja wa Martys mjini Kinshasa, Ulimwengu alifunga bao hilo
dakika ya 68 baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Rogger Asale dakika 57.
Ulimwengu alifunga bao hilo akimalizia
pasi ya Rainfrod Kalaba, wakati bao la kwanza la Mabingwa hao wa Afrika
lilifungwa na Luyindama dakika ya 65 kwa pasi ya Joseph Bolingi. Mazembe
inarejea Lubumbashi kujiandaa na mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora
Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco Aprili 20
mwaka huu.
Mazembe inahitaji ushindi wa 3-0 ili
kusonga mbele baada ya kufungwa mabao 2-0 katika Mchezo wa kwanza
mwishoni mwa wiki mjini Casablanca.
No comments:
Post a Comment