Tuesday 26 April 2016

Je Tunaenzi Muungano Uliowekwa na Waasisi Wetu Hayati Karume na Mwalimu Nyerere?

 

Kuifufua Tanganyika ni kuiua Tanzania Sikubaliani kabisa na Suala hili, kwa Sifa tu na Uroho Wa Madaraka na Huku Wakishabikiwa na Mazuzu kuna Watu Watafanya kila hila Zanzibar ijitenge na Tanganyika. Nasema Dhambi hii ya Utengano na iwatafune, NaombaMungu Anisamehe, hakika Dhambi ya Utengano na iwatafute Hawatabaki salama”.

Maneno haya aliyasema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo Yamesaidia kudumisha na kuuenzi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hadi leo hii Umetimiza miaka 52 tangu kuasisiwa kwake na Abeid Amani Karume pamoja na Mwalimu Nyerere

Kwa kutambua hilo Mwenyekiti Taifa wa Chama Allience fo Democratic Party (ADC), Said Miraji anasema ili kuenzi na kudumisha kile Waasisi wa Muungano Walichotuachia ipo haja Ya kuepusha siasa katika Muungano kwa kuwapa uhuru Watanganyika na Wazanzibari kujadili Na kuamua kile wanachokitaka.

Anasema Muungano Haulindwi kwa Mtutu wa Bunduki kama ilivyosasa na kupelekea kubaguana kwa Misingi ya Udini, ukabila na kiitikadi bali Watanzania Wauenzi na kuuishi Sambamba na kuwa na Sera ya Watanganyika na Wazanzibari itakayohakikisha Chama chochote cha Siasa kinapoingia Madarakani Kinaheshimu na kuulinda Muungano.Pamoja na Mambo Mengine pia Kiongozi huyo amezungumzia Changamoto na faida Zitokanazo Na Muungano; Unaweza kumsikiliza hapa Chini akifafanua

No comments:

Post a Comment