Thursday 28 April 2016

Aliyekuwa Mkurugenzi wa TIC Julieth Kairuki Hakuchukua Mshahara Miezi 36


 

Na Kalonga Kasati

Hali ya Utumbuaji wa Majipu ikiendelea kwa Wakurugenzi wa Taasisi za Serikali ikitofautina Mitazamo ya Watu wengi Hali hii Wanaipenda na Wengi Hawakubaliana na Hali hii ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kuwatumbua na akiacha Majipu Mengine kuyatumbua akiwemo Waziri wa Ujenzi wa Awamu ya nne na Marais Wastaafu akiwaacha na lingine Nikupata katiba Mpya Na Bunge kuonyeshwa live haya ni Baadhi ya Mambo yakiwakera Watanzania Walio Wengi

Licha ya kupingwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Baada ya kutangaza kupunguza Mishahara ya Watumishi wa Umma toka Milioni 40 hadi 15, leo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli ametengua Uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Juliet Kairuki.

Dk. Magufuli amefikia Maamuzi hayo baada ya kubaini Mkurugenzi huyo kutochukua Mshahara wa Serikali katika kipindi Miezi (36) tangu alipoajiriwa Aprili 2013  kwa Madai kuwa Mshahara huo ni mdogo.

Machi 29 mwaka huu Rais Magufuli akiwa mjini Chato wakati wa mapumziko ya wiki moja Alitangaza kupunguza mishahara ya juu kutoka Sh40 milioni hadi Sh15 milioni kwa mwezi na kusema wapo watumishi wa umma wanalipwa masilahi manono na kuishi kama wako peponi, Huku wanaolipwa Sh300,000 wakiishi kama wako jehanamu”.

Aidha taarifa hiyo inasema Rais Magufuli amemteua Clifford Katondo Tandari kukaimu Nafasi hiyo, huku mchakato wa kumpata Mkurugenzi mpya Ukianza Mara moja.
IMG-20160428-WA0013

No comments:

Post a Comment