Simon Siro:Kuwaondoa Ombaomba Dar Tutafuata Haki Zote za Binadamu Zinazostahili Kuzipata
Imepita wiki moja tangu Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam Paul Makonda alipotangaza kuwa Ombaomba wote inabidi
waondolewe maeneo ya mjini, macho na masikio ya watanzania yalikuwa
yanasubiri kitakacho fanyika leo Jumatatu ya Aprili 18, katika zoezi la
kuwaondoa ombaomba Jijini hapa.
Wakati Watanzania wakisubiri hatua
zitakazo chukuliwa na Jeshi la Polisi katika kuwaondoa Ombaomba, Kamanda
wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Jijini Dar es Salaam Simon Sirro
amesema hawatalianza zoezi hilo mpaka watakapo fanya taratibu stahiki
kwa kuzingatia haki za binadamu.
Kamanda Sirro amesema zoezi la kuwaondoa
Ombaomba litahusisha kamata kamata, hivyo kuna utaratibu wa kuwakamata
tofauti na unavyo wakamata watu wengine mfano Majambazi, Wafanyabiashara
ya ngono (Dada poa, Kaka poa) na wahalifu wengine.
Vilevile Kamanda Sirro ameeleza kuwa
zoezi la kuwaondoa ombaomba ni suala Mtambuka Hivyo litahusisha Idara na
Wizara mbalimbali kwa pamoja kwa kuwa Ombaomba hawa Watahitaji Chakula
na Usafiri, katika hatua nyingine Kamanda Sirro amesisitiza kuwa zoezi
la kuwaondoa ombaomba siyo nguvu ya soda, hivyo ni bora waondoke bila
nguvu ya Jeshi la Polisi kwani siyo vizuri.
No comments:
Post a Comment