Saturday 23 April 2016

Wanahabari Wanavyominywa Wasihabarishe Jamii na Watawala

 

 

 

Jumuiya ya Maripota Wasio na Mipaka (RSF) imewakosoa viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kuwakandamiza waandishi habari.

Jumuiya hiyo imesema uhuru wa wanahabari  nchini humo unakandamizwa kwa lengo la kuwanyamazisha, kutokana na Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika huku Rais Joseph Kabila akitazamiwa kugombea kwa mara nyingine kiti hicho.

Jumuiya hiyo imesema waandishi wa habari wanakabiliwa na vitisho vya kuuawa, kutiwa Nguvuni kwa sababu za kisiasa ikiwemo kupigwa na vyombo vya dola kwa sababu ya kupinga Jaribio la Rais Kabila kutaka kugombea kwa mara nyingine kiti hicho mara ya tatu mfululizo.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inashika nafasi ya 158 kati ya nchi 180 kwenye orodha Uhuru wa vyombo vya habari duniani.

No comments:

Post a Comment