Saturday, 6 February 2016

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AMOS MAKALLA -AKAGUA MPAKA WA TANZANIA NA KENYA

New Picture (1)Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amos Makalla na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na usalama Mkoa wamekagua mpaka wa Tanzania na Kenya amekagua alama za mpaka (mawe) ameridhishwa na hali ya usalama wa mpaka na kuagiza kamati ya ulinzi na usalama wiilaya kuwa na mikutano ya ujirani mwema
Aidha Mkuu wa Mkoa ameshiriki kuteketeza mitambo 6 ya kutengeneza pombe haramu ya Gongo, lita 140 za gongo, pipa 33 za maloweko ya gongo
Pia amewataka wananchi kuacha unywaji na upikaji gongo.
New Picture (2)New Picture (3)Baadhi ya mitambo  ya kutengeneza pombe haramu ya Gongo,

MWENYEKITI WA CCM, KIKWETE AOMBA WAZEE KUUNGA MKONO UONGOZI WA RAIS MAGUFULI

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akilakiwa na  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye.baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Singida leo, kaba ya kukutana na kuzungumza na wazee wa Singida Mjini. Kulia ni Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Mary Maziku.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akisubiri kuvalishwa skafu baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Singida leo. Kushoto ni Mama Salma Kikwete. na Kulia ni Kaimu Katibu wa CCM mkoa wa Singida Mary Maziku na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye.
 Chipukizi wakimvalisha Skafu Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akienda katika Ofisi ya CCM mkoa wa Singida, akiwa na Mkewe Mama Salma

No comments:

Post a Comment