Saturday, 9 April 2016

Muogeleaji Nyota wa Tanzania Sonia Tumiotto asema Mashindano Yalikuwa Magumu

freestyle-f-31
Muogeleaji wa Tanzania aliyeshinda medali tatu katika michezo ya kutafuta kufuzu mashindano ya Olimpiki Sonia Tumiotto amesema Haikuwa kazi rahisi kwa yeye kupata mafanikio hayo zaidi ya kujituma zaidi.
 
Sonia ni na waogeleaji Hilal Hilal, Collins Saliboko na Aliasghar Karimjee waliwakilisha nchi katika mahindano hayo na yeye kufanikiwa kushinda medali tatu na wenzake hawakufanikiwa kushinda medali pamoja na kufanya vyema katika kuongeza viwango vyao katika mchezo huo.
 
 Sonia alisema kuwa mashindano hayo yalikuwa magumu sana kutokana na kushirikisha waogeleaji wengi ambao nao walikuwa wanasaka tiketi ya kushiriki mashindano ya kimataifa.
“Nashukuru Mungu kwa kunifanikisha kuwa  na nguvu na kushinda, kwa kweli haikuwa kazi rahisi, kila muogeleaji alikuwa anataka medali, anataka kufuzu mashindano ya Olimpiki, ushindani ulikuwa mkubwa sana, nawashukuru wote walionipa moyo na kufanya vizuri,”
“Waogeleaji wenzangu nawashukuru kwa kunipa hamasa, kwa kweli tulikuwa na pamoja muda wote, yoyote aliyekuwa anashindana tulikuwa nyuma yake, ushindi wangu ni wa watanzania wote japo ilikuwa mara yangu ya kwanza kushiriki katika mashindano makubwa ya kutafuta tiketi ya kufuzu Olimpiki,  “ alisema Sonia.
 
Meneja wa timu ya Taifa ya kuogelea,  Leena Kapadia  alisema kuwa ushindani ulikuwa mkubwa na jumla ya nchi 60 na waogeleaji 900 walishiriki katika mashindano hayo. Leena alisema kuwa mashindano hyakuwa ya kawaida na juhudi ziliwafanya wao kufanya vizuri.
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Kuogelea (TSA)  Ramadhan Namkoveka alisema kuwa Sonia amekuwa muogeleaji wa kwanza Tanzania kushinda medali tatu katika mashindano ya kimataifa yanayotambuliwa na Shirikisho la mchezo huo Duniani (Fina) tokea kupata Uhuru mwaka 1961.
 
“Kwa kweli tumefarijika sana na matokeo haya, hii ni historia, nampokengeza Sonia na waogeleaji wote kwani walikuwa timu ya Tanzania, hii ni ishra tosha kuwa mchezo unakuwa,” alisema Namkoveka.
 
Alisema kuwa lengo lao lilikuwa kupata uzoefu wa mashindano ya kimataifa mbali ya kutafuta tiketi za kufuzu kayika mashindano ya Olimpiki. “Mchezo wetu una changamoto nyingi sana na bila juhudi za wadau kwa kushirikiana na serikali za kujenga bwawa la kuogelea la Mita 50, bado tutaedelea kusota kufikia lengoletu, tunahitaji bwawa na vifaa bora,” alisema .
Kocha wa klabu ya Dar Swim Club ambayo ndiyo Sonia anatokea, Michael Livingstone alisema kuwa moyo wa kujituma ndiyo nyenzo pekee iliyomfanya Sonia kushinda. Michael alisema kuwa Sonia ana kipaji cha hali ya juu na ana amini kuwa Tanzania ina waogeleaji wenye vipaji  kama vya Sonia ambavyo wao kama makocha wanahitaji kuviendeleza.
 
Katibu Mkuu wa klabu ya Dar Swim Club, Inviolata Itatiro  Aliwapongeza waogeaji hao kwa kufanya vizuri katika mashindan hayo na kuwaomba wazazi kuwaruhusu watoo wao kujifunza mchezo huo.Inviolata  alisema kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni vifaa pamoja na bwawa, lakini klabu yake ipo tayari kuwafundisha watoto wanaotaka kujifunza mchezo huo bure ili kuwaendeleza.
 
“Nawaomba wazazi kuitikia wito wangu, nina makocha wazuri ambao wamemfundisha Sonia kabla ya kupata nafasi ya kusoka Uingereza, Makocha wao tayari kujitolea kuwafundisha kwani lengo letu ni kuona kila Mtanzania anajua kuogelea,” alisema Inviolata.

Ndanda  Kosovo  AFariki Dunia

KOS Mwanamuziki mkongwe aliyewahi kujizolea sifa kem kem katika miondoko ya dansi hapa  nchini wakati akiwa na bendi ya FM miaka ya nyuma kabla ya kujiengua na kuunda kundi lake lililojulikana kwa jina la Stono Musica a.k.a Wajela Jela Gwaa, Ndanda Kosovo ‘Kichaa’ amefariki Dunia leo asubuhi,baada ya kuugua kwa siku chache

Taarifa kutoka kwa mtu wake wa Karibu ambaye pia ni Mwanamuziki wa dansi,Kardinal Gento amethibitisha kutokea kwa kifo hicho na ameongeza kuwa Ndanda Kosovo amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Muhimbili alikokuwa amelazwa tangu juzi kutokana na matatizo ya tumbo.

Nwanko Kanu Ashiriki Mafunzo Na Watoto Wa Kituo CHa Jakaya Kikwete

nw1
Mchezaji nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Naijeria, Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akiwaelekeza watoto katika mafunzo ya mpira wa miguu wakati Alipotembelea katika kituo cha michezo ya Jakaya Kikwete kilichopo Kidongo Chekundu jijini Dar es salaam.
nw2
Mchezaji nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Naijeria, Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akiwaelekeza watoto katika mafunzo ya mpira wa miguu wakati alipotembelea katika kituo cha michezo ya Jakaya Kikwete kilichopo Kidongo Chekundu jijini Dar es salaam.
nw3
Mchezaji nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Naijeria, Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akizungumza na watoto mara baada ya  mafunzo ya mpira wa miguu wakati alipotembelea katika kituo cha michezo ya Jakaya Kikwete kilichopo Kidongo Chekundu jijini Dar es salaam.
nw4
Mchezaji nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Naijeria, Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika akizungumza na watoto mara baada ya  mafunzo ya mpira wa miguu wakati alipotembelea katika kituo cha michezo ya Jakaya Kikwete kilichopo Kidongo Chekundu jijini Dar es salaam.
………………………………………………………………………………………
Mchezaji nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria, Nwanko Kanu ambaye kwa sasa ni balozi wa makampuni ya StarTimes barani Afrika ametembelea na kushiriki kwenye mafunzo na watoto kwenye kituo cha Jakaya Mrisho Kikwete cha jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Kanu ambaye amekuja kwa shughuli za kampuni hiyo atakuwepo nchini Tanzania kwa muda wa siku tano alifurahi sana kuona watoto wameandaliwa mazingira mazuri kwa ajili ya michezo mbalimbali kwani sio wote waliopata fursa hiyo.

“Wakati mimi ninaanza kucheza mpira hakukuwa na kituo kizuri kama hiki wala jezi, viatu na walimu wazuri mlio nao sasa. Hii ni fursa ya kipekee kwenu nyinyi kuweza kuonyesha juhudi za kujifunza ili mje kuwa kama mimi siku za mbeleni. Leo mimi nimekuwa maarufu ni kwa sababu nilikuwa na nidhamu, bidii, dhamira na kuwasikiliza walimu wangu walipokuwa wananifundisha. Hatimaye leo hii nina mafanikio makubwa, ninaishi maisha mazuri, wazazi wangu pia wanaishi mahali pazuri, wanasafiri na kupata wanachokitaka kwa sababu tu ya mimi kufanikiwa.” Kanu aliwaambia watoto wa kituo cha Jakaya Kikwete
Kampuni ya StarTimes ambayo imo zaidi ya nchi kumi barani Afrika imemtua mchezaji huyo kama balozi katika kuwawakilisha katika shughuli mbalimbali. Kanu anatarajia kuwa chachu kwa katika kampuni Hiyo hususani katika kuboresha na kuongeza vipindi na chaneli za michezo kwani waafrika wengi wanapenda soka.

“Ninaamini mchezo wa soka ndio unaopendwa na watu wengi zaidi duniani na waafrika ni miongoni mwao. StarTimes mpaka sasa wamepiga hatua kubwa katika kulisimamia hili, mpaka sasa tayari wana haki miliki za kuonyesha ligi za Budensiliga na Serie A za Ujerumani na Italia. Hiyo ni hatua kubwa kwani wateja wanafurahia michezo hiyo inyoonekana moja kwa moja kwa vifurusushi vya bei nafuu. Kama balozi ninaahidi kushirikiana na kampuni katika kuboresha zaidi vipindi vyake na pia kuishauri kujikita zaidi na michezo ya nyumbani. Kama Mnavyoona kwa mara ya kwanza tumedhamini ligi daraja la kwanza.” Aliongezea mchezaji Kanu
Kanu alihitimisha kwa kuwataka watoto wa kituoni hapo kuonyesha bidii, utii na dhamira ya dhati kwa kila wanachokifanya, “Ningependa kuwashauri wadogo zangu kuwa popote utakapokwenda duniani kwenye Mchezo wa soka, viwanja na mipira inayotumika ni hii hii wala hakuna Tofauti yoyote. Hivyo basi sioni kama kuna kitu cha kuwazuia na nyinyi msifanikiwe. Kama nilivyowaambia awali, bidii, nidhamu, dhamira na Utii kwa walimu wenu ndio msingi wa mafanikio ya mwanasoka yeyote Yule duniani. Nawatakia kila la kheri na siku nyingine nikija Tanzania naahidi kuwatembelea tena.”

Naye kwa upande wake Kocha Mkuu wa Kituo cha Vijana cha Jakaya Mrisho Kikwete, Bw. Eduard Tamayo alielezea furaha yake kwa kampuni ya StarTimes kuandaa kitu kama hiko na kukiteua kituo hiko kuwa mwenyeji wa ugeni wa Kanu nchini Tanzania.

“Nimefurahi sana kwa ujio aliyekuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Naijeria na vilabu vikubwa barani Ulaya kama vile Ajax, Inter Milan na Arsena, Nwanko Kanu kutembelea hapa na kushiriki mafunzo na watoto. Hii ni bahati kubwa sana kwa watoto hawa kwani ni nadra sana kutokea, kupata mafunzo, kuzungumza, kupata ushauri na kuuliza maswali moja kwa moja kwa Kanu. Ninatumaini itakuwa imewapa motisha kubwa sana.” Alisema Bw. Tamayo

Kocha Mkuu huyo kituoni hapo alihitimisha kwa kuwataka wazazi kuwapeleka na kuwasajili watoto kituoni hapo kwa mafunzo kwani Wanapokelewa na kuwapatia mafunzo mazuri kwa kuviendeleza vipaji vyao. Na kwamba kituo hiko ni fursa kwa watanzania hivyo ni vema kukitumia vizuri.


No comments:

Post a Comment