Saturday, 9 April 2016

Majaliwa atemblea Hospitali ya Benjamini Mkapa

lil1
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa kaikagua mashine ya MRI katika hospitali ya Benjamin Mkapa kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma wakati Alipoitembela  Aprili 9, 2016. Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Afya, , Dkt. Hamis Kigangwala. (Picha na Ofisi ya Wziri Mkuu.)
lil2
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Khamis Kigangwala wakikagua mashine ya Mobile Digital xray wakati  walipotembelea hospitali ya Benjamin Mkapa kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma Aprili 9, 2016. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Hospitali hiyo Profesa Gesai. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Taasisi Ya  Kufundisha  Lugha  Ya “International Language Training  Centre ” Yaboreshwa Zaidi Mazingira Ya Kujifunza.

Charles Mombeki ambae ni Mkurugenzi wa
Taasisi ya Kufundisha Lugha mbalimbali ikiwemo za Kitaifa na Kimataifa Jijini Mwanza ya “International Language
Training Centre” akiwa amesimama katika jengo la taasisi hiyo iliyopo Isamilo (barabara ya Medical Research) Jijini Mwanza.
 
Mombeki anasema taasisi hiyo imeboresha zaidi mazingira ya kujifusia ili kukidhi mahitaji wasomaji. Pia anaongeza kwamba Taasisi hiyo imeboresha mazingira kujifunzia kwa ajili ya Kituo chake cha Elimu ya Makuzi kwa Watoto Wadogo (Day Care Centre) ambapo anawasihi wananchi kutembelea taasisi hiyo ili kunufaika na fursa iliyopo hivi sasa kabla haijafikia ukomo.
 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kufundisha Lugha mbalimbali ikiwemo za Kitaifa na Kimataifa Jijini Mwanza ya “International Language Training Centre” akitoa ufafanuzi kwa wanaohitaji kusoma katika taasisi yake. Pembeni ni eneo rafiki kwa ajili ya mapumziko mafupi baada ya masomo au majadiliano baada ya masomo. 
 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kufundisha Lugha mbalimbali ikiwemo za Kitaifa na Kimataifa Jijini Mwanza ya “International Language Training Centre” akionyesha baadhi ya maeneo kwa ajili ya michezo ya watoto.
 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kufundisha Lugha mbalimbali ikiwemo za Kitaifa na Kimataifa Jijini Mwanza ya “International Language Training Centre” akionyesha baadhi ya maeneo kwa ajili ya michezo ya watoto.
 
Wasiliana na International Language Training Centre kwa nambari 0784 66 49 33 au 0754 66 49 33
Ili Usipitwe.

Waziri Ummy Mwalimu atembelea Hospitali za Mkoa wa Mbeya

8e796dee-b674-43f7-97f8-3bad1046087d
Na Catherine Sungura, Mbeya
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Mhe. Ummy Mwalimu amefanya ziara katika hospitali zilizopo Mbeya na kuzitaka hospitali zinazotumia mfumo wa ukusanyaji mapato wa kieletroniki wasibweteke na mapato wanayoyakusanya kila siku.
Rai hiyo imetolewa na aziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee Na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali ya rufaa ya kanda ya mjini Mbeya.

Ummy alisema ukusanyaji wa mapato kwa mfumo huu unasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha huduma za afya nchini ikiwemo ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba pamoja na utoaji wa motisha kwa watumishi.

“Bado tunatambua hali ya uhaba wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kuanzia ngazi zote, tukiweza kusimamia vizuri hili tutafanikiwa,” alisema.

Aidha alisema wanatarajia katika serikali ya awamu hii bajeti ya dawa itaongezeka zaidi ya mara tatu kulinganisha na bajeti za nyuma, hivyo Wameishauri Bohari Kuu ya Dawa (MSD) wanunue dawa toka kwa wawekezaji wa hapa nchini ambapo itakua na bei nafuu na itaongeza tija na upatikanaji wa dawa kwa haraka.

Waziri Ummy Mwalimu aliutaka Mkoa kufuatilia, kuwafichua na kuwachukulia hatua wale wote watakaojihusisha na wizi wa dawa.
“Tunao watumishi wachache wa afya ambao wanahujumu na kuiba dawa na kuzipeleka kwenye maduka ya dawa binafsi, hao hatutowafumbia macho na kuwapeleka mahakamani”
Kuhusu upungufu wa watumishi wa kada ya afya nchini, Waziri wa afya alisema, nchi ina upungufu wa asilimia 52, hivyo serikali inatarajia kuajiri watumishi takribani elfu kumi hivi karibuni ambao watatawanywa nchi nzima ikiwemo mikoa iliyo pembezoni.
Katika hospitali ya uzazi ya Meta, waziri huyo ameguswa na ufinyu wa wodi za wazazi na kupelekea mama wajawazito na waliojifungua kulala chini na wawili wawili kwenye kitanda kimoja na hivyo kuwataka kufanya haraka ujenzi wa jengo jipya litakaloondoa mrundikano wa mama wajawazito na watoto njiti.
Hospitali ya Kanda ya Rufaa Mbeya inakusanya kwa mwezi kiasi cha shilingi Milioni mia tano na pia inahudumia mikoa saba nchini na kuhudumia zaidi ya watu milioni mbili.
46e02c3a-bc41-4fed-9ff6-a180f42fa264
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akisalimia na watumishi mara alipofika kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mbeya.
afc64d2e-46a1-49a8-be9b-59340b6d8a8a
Waziri Ummy akimsalimia mtoto Jenifer Joel (9) mkazi wa Chunya aliyelazwa hospitalini hapo.
5f7ab771-5109-4c0c-95e6-83931c8ec108
Waziri wa afya akimjulia hali mtoto Baraka Jekonia (1) mkazi wa Chunya aliyelazwa wodi ya watoto, Waziri Ummy ameitaka hospitali hiyo kuwachaji pesa wagonjwa wote wanaofika hospitali ya rufaa moja kwa moja bila kupatiwa rufaa kutoka vituo vya afya vilivyopo jirani na wananchi ili kupunguza msongamano kwenye hospitali za rufaa nchini.
8e796dee-b674-43f7-97f8-3bad1046087d
Katika hospitali ya uzazi ya Meta, Waziri Ummy Mwalimu alimsalimia Binti Kanisia Komba aliyejifungua mtoto wa kike katika hospitali hiyo mama wajawazito wote wanatibiwa kwa kadi ya bima ya afya inayodhaminiwa mpango wa kusaidia akina mama wajawazito wa KFW toka Banki ya Ujerumani.
9518e21d-3e1e-43ad-a96a-c9b85ce91018
Hospitali ya Meta tayari imetekeleza maagizo ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ya kutoa kipaumbele kwa wazee wote nchini wanapofika kwenye vituo vya kutolea huduma.
974627cc-137b-436b-996a-f364952f7580
Waziri Ummy akiwasalimia wazazi waliolazwa kwenye moja ya wodi Hospitali ya Meta kutokana na ufinyu wa wodi inawalazimu akinamama wengine kulala chini hospitali hiyo inatarajia kuanza ujenzi wa jengo jipya ambalo litaondoa msongamano wa wazazi hospitalini hapo.
5b44d003-a727-495c-bde5-dea332ef407f
Waziri wa Afya akiwasalimia wagonjwa waliofika Hospitali ya Uzazi ya Meta kupata matibabu.

TRA Yakamata  Bidhaa Za Magendo, Ni  Sukari Na Mafuta Ya Kula

Nyumba hii ndiyo Ofisi ya Bosi ambayo utumika kuweka bidhaa kabla ya kusambazwa sokoni iliyopo Somanga njia nne eneo la Kikanda Wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi.
sehemu ya kuweka sukari na kupima.
Nyumba inayotumika kuweka sukari
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Richard Kayomboakionesha ndoo zinazotarajiwa kuwekwa mafuta.
Sukari na viroba vya kuweka kwa matayarisho ya kuingizwa sokoni.
Hii ni Sukari iliyomwangwa chini kabla ya kuwekwa kwenye viroba
Askari wakisimamia zoezi la kuvunja mlango
 
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Richard Kayombo akizungumza na waandishi.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA akionesha sukari.
Mkurugenzi wa Elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA
Aina ya mafuta kutoka nje ya nchi tayari kuwekwa kwenye ndoo kwa kupeleka Sokoni
Polisi akilinda viroba vyenye sukari kutoka nje ya nchi.
Madumu yaliyokua na mafuta ya kula na ndoo zinazotarajiwa kuwekwa mafuta
Nyumba ya mtuhumiwa Yusuf Sareh iliyopo Somanga Njia nne Kikanda.
………………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu-Kilwa
Siku ya tarehe 6/4/2016 maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kikosi cha (FAST)  wakiwa na maofisa wa Polisi walifanya upekuzi kwa lengo la kutafuta magendo kwenye nyumba ya mfanyabiashara Yusuf Barkat Sareh,  Upekuzi huo ulifanyika baada ya kupata taarifa za kiintelijensia zilizofanyiwa kazi muda mrefu. Bidhaa mbalimbali kutoka nje ya nchi zilikamatwa kama zifuatazo.
 
Sukari ya India kilo 50 jumla mifuko762 Sukari ya nje iliyokamatwa kwenye mifuko ya viwanda vya hapa nchini kilo 25 jumla mifuko 135
Mafuta ya kula lita ishirini (20) aina mbalimbali kutoka nje jumla madumu 49 Betri aina ya tigger katoni 223 Amira katoni 135
Sabuni za kufulia katoni 48 Vitu mbalimbali vilivyokamatwa kama ushahidi wa biashara haramu ya magendo ya sukari.
 
Mashine mbili (2) za kushonea kwenye mifuko ya iliyowekwa sukari inatoka nje ya nchi na kuwekwa kwenye mifuko ya viwanda vya nchini nya sukari vya Kilombero,TPC na Mtibwa Sugar. Mifuko mitupu mipya ya sukari kilo 25 toka India  2000 Mifuko iliyotumika ya kilo 50 mitupu ya sukari36,000 mifuko ya sukari iliyotumika ya Viwanda vya Tanzania ya kilo25 kiasi cha 1150 Madumu mafuta ya nje mchanganyiko ya kula lita 20 kiasi cha 609 Madumu matupu ya lita 10 ya nje kiasi cha 310.

Waziri Ummy mwalimu atembela hospitali mbeya

indexnnNa. Mwandishi Wetu

Hospitali zinazotumia mfumo.wa ukusanyaji mapato wa  kielectronik wametakiwa wasibweteke na mapato wanayoyakusanya kila siku.
Rai hiyo.imetolewa na waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na Watoto Mh.Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali ya rufaa ya kanda ya mjini Mbeya

Ummy alisema ukusanyaji wa mapato kwa mfumo huu unasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha huduma za afya nchini ikiwemo Ununuzi wa dawa,vifaa na vifaa tiba pamoja na utoaji wa motisha kwa Watumishi

“Bado tunatambua hali ya uhaba wa upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kuanzia ngazi zote,tukiweza kusimamia vizuri hili tutafanikiwa”alisema
Aidha alisema wanatarajia katika serikali ya awamu hii bajeti ya dawa itaongezeka zaidi ya mara tatu kulinganisha na bajeti za nyuma,hivyo wameishauri bohari kuu ya dawa wanunue dawa toka kwa wawekezaji Wa hapa nchini ambapo itakua na bei nafuu na itaongeza tija na upatikanaji wa dawa kwa haraka

waziri Ummy Mwalimu aliutaka Mkoa kufuatilia,kuwafichua na kuwachukulia hatua wale wote watakaojihusisha na wizi wa dawa
“Tunao watumishi wachache wa afya ambao wanahujumu na kuiba dawa Na kuzipeleka kwenye maduka ya.dawa binafsi,hao hatutowafumbia macho na kuwapeleka mahakamani”
Kuhusu upungufu wa watumishi wa kada ya afya nchini ,Wazirini wa Afya alisema,nchi ina upungufu wa asilimia 52,hivyo.serikali inatarajia kuajiri watumishi takribani elfu kumi hivi karibuni ambao watatawanywa nchi nzima ikiwemo mikoa iliyo pembezoni
Katika hospitali ya uzazi ya Meta,waziri huyo ameguswa na ufinyu wa wodi za wazazi na kupelekea mama wajawazito na waliojifungua kulala chini na wawili wawili kwenye kitanda kimoja na hivyo kuwataka kufanya haraka ujenzi wa jengo jipya litakaloondoa mrundikano wa mama wajawazito na watoto njiti
Hospitali ya kanda ya rufaa Mbeya inakusanya kwa mwezi kiasi cha shilingi mia tano,inahudumia mikoa saba nchini na kuhudumia zaidi ya watu milioni mbili.

No comments:

Post a Comment