Droo ya Nusu Fainali ya Kombe la
Shirikisho (Azam Sports Federation Cup), inatarajiwa kufanyika kesho
Jumanne saa 3 usiku moja kwa moja (live) kupitia kituo cha luninga cha
AzamTwo.
Hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la
Shirikisho (ASFC) itafanyika live katika kituo cha AzamTwo, ambao
kupitia Azamtv ndio wadhamini wa wakuu wa michuano hiyo iliyoibua Msisimiko wa mpira wa miguu na kushirikisha timu nyingi zaidi nchini.
Baada ya timu za Azam FC, Mwadui
FC, na Yanga SC kukata tiketi ya kucheza Nusu Fainali, Mshindi wa mchezo
kati ya Simba SC dhidi ya Coastal Union utakaochezwa leo katika uwanja
wa Taifa jijini Dar es salaam atungana na timu hizo tatu kwenye droo ya
kesho.
Michuano ya Kombe la Shirikisho
iliyoanza kwa kushirikisha timu 64 mwishoni mwa mwaka Jana, imefikia
hatua hatua ya nusu fainali, baada ya Azam FC kuindoa Prisons (3-1),
Mwadui FC kuiondosha Geita Gold (3-0) na Yanga SC kuwaondoa Ndanda FC
kwa mabao (2-1).
Mshindi wa Kombe la Shirikisho
(ASFC) msimu huu, ataiwakilisha Tanzania mwaka 2017 katika michuano ya
Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC).
Chama cha Mapinduzi (CCM) kitaendelea kuimarisha Miundombinu na mazingira rafiki kwa Wafanyakazi Wake
Na Mwandishi wetu , Zanzibar.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM)
kimesema kitaendelea kuimarisha Miundombinu na Mazingira rafiki ya
kiutendaji kwa kuwapatia vifaa vya kisasa jumuiya mbali mbali za taasisi
hiyo ili zifanye kazi kwa ufanisi.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar, Najma Murtaza Giga wakati
akikabidhi Vifaa mbali mbali kwa Uongozi wa Wazazi Mkoa wa Mjini, huko
Afisi ya CCM Amani.
Amesema taasisi hiyo inatakiwa kwenda sambamba na mabadilio ya sayansi na teknolojia kwa kutumia nyenzo za
Aidha amesema chama hicho
kitafanya kila kinachowezekana kuhakikisha kinawapatia Vitendea Kazi
Watendaji wa CCM kadri ya uwezo wa kifedha unaporuhusu.
Giga amewasihi viongozi mbali
mbali wa chama na jumuiya zingine kuunga mkono juhudi Zinazofanywa na
jumuiya ya wazazi katika kutoa malezi bora ya kitaaluma na kisaikolojia
kwa watoto kwa lengo la kutengeneza viongozi makini na weledi wa baadae.
Nae Katibu wa CCM mkoa wa mjini,
Mohamed Omar Nyawenga amewataka watendaji wa Chama hicho kuwa wabunifu
na kutumia weledi kwa kufanya kazi kwa bidi ili kusaiudia Chama
kutekeleza ilani ya uchaguzi ya 2015/2020 kwa ufanisi ili wananchi
waendelee kuiunga mkono CCM katika chaguzi zote zijazo.
Vifaa vilivyotolewa ni Komputa 2, mashine za Printer 2 na mashine za photocopy 4 kwa Jumuiya ya wazazi mkoa wa mjini kichama.
No comments:
Post a Comment