Rais mteule wa Marekani Donald Trump amesema hataki kulipwa mshahara wa
rais wa $400,000 atakapochukua hatamu Januari mwakani. Badala yake
atakuwa akilipwa dola moja ya Marekani ($1) pekee kila mwaka sawa na
shilingi 2000 ya kitanzania.
Alifichua mpango wake huo wakati wa mahojiano na Lesley Stahl kipindi cha 60 Minutes cha CBS News.
Ingawa hakujua rais huwa analipwa pesa ngapi, Bw Trump alisema alidhani anahitaji kuchukua tu $1.
Baada ya Bi Stahl kumjulisha kwamba mshahara wa rais ni $400,000, alisema: "Hapana, sitaupokea mshahara huo. Sizichukui kamwe."
Rais huyo mteule anatimiza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni.
Aliambia waliohudhura mkutano wake Septemba kwamba mshahara wa rais si jambo kubwa kwake.
Kuna viongozi wengine walioukataa mshahara?
Bw Trump si kiongozi wa kwanza wa Marekani kukataa mshahara.
Herbert Hoover, aliyekuwa ametajirika kupitia biashara ya madini kabla
ya kuingia madarakani, na John F Kennedy, aliyerithi utajiri mwili, wote
walikataa kupokea mashahara na badala yake wakatoa pesa hizo zisaidie
wasiojiweza katika jamii.
Meya wa zamani Michael Bloomberg, gavana wa zamani wa California Arnold
Schwarzenegger na gavana wa zamani wa Massachusetts Mitt Romney pia
walikataa kupokea mishahara yao.
Mark Zuckerberg, mwanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook, ndiye
mfanyakazi anayelipwa mshahara wa chini zaidi katika kampuni hiyo.
Aidha, ni miongoni wa CEO (Afisa Mkuu Mtendaji) wengi ambao hulipwa mshahara wa $1 pekee.
No comments:
Post a Comment