Thursday 24 November 2016

Man City yatinga hatua ya mtoano kwa mara ya nne mfululizo

David Silva akiifungia City goli
Mchezaji kiungo David silva ameithibitishia klabu ya Manchester City kuingia hatua ya mtoano kwa mara nne mfululizo kwa kutoka sare ya goli 1-1 dhidi ya Borussia Monchengladbach.
Mchezo huo uliokuwa wa vuta nikutute ulishuhudia kila timu ikimaliza na wachezaji 10 kiungo Lars Stindl akilimwa kadi nyekundu dakika ya 51 kabla ya Fernandinho wa man city kuzawadiwa kadi nyekundu dakika ya 63.

Kocha wa timu ya Manchester City Pep Guardiola amesema amefurahishwa na kiwango cha timu yake na kuongeza kuwa kwa matokeo waliyoyayapata moja kwa moja wameepuka kupangiwa na Bayern Munich

Matokeo ya michezo mingine
Besiktas 3-3 Benfica
FC Rostov 3-2 Bayern Mun
Arsenal 2-2 Paris St G
PFC Ludogorets Razgrad 0 -0 Basel
Napoli 0 -0 Dynamo Kiev
Borussia Mönchengladbach 1-1 Manchester City F.C.
Celtic 0-2 Barcelona
Atlético Madrid 2-0 PSV Eindhoven

No comments:

Post a Comment