Wednesday 30 November 2016

Zaidi ya watu 16,000 wakosa makazi nchini Syria

Baadhi ya familia zilizokosa makazi nchini Syria
  Umoja wa matifa umesema takribani raia 16,000 wametawanyika nchini Syria baada ya majeshi ya serikali kusonga mbele kuukamata mji wa Aleppo uliokuwa ukishikiliwa na waasi.
Mkuu wa misaada ya kibinadamu wa umoja wa mataifa Stephen O'Brien amesema maelfu ya watu wengine wanatarajiwa kuukimbia mji huo kutokana na mapigano yanayoendelea na kuimarika katika siku zijazo.
 O'Brien ameonesha wasiwasi kuhusu hatma ya raia hao wanaoyakimbia mapigano na kuainisha kuwa yanatia shaka.majeshi na wapiganaji wa jeshi la Syria wamekamata theluthi mbili ya mji uliokuwa ukishikiliwa na waasi Mashariki ya Aleppo tangu mwishoni mwa juma.

No comments:

Post a Comment