Tuesday 29 November 2016

Uchaguzi wa urais Somalia waahirishwa tena

Rais anayeondoka Hassan Sheikh Mohamud
Uchaguzi wa urais nchini Somalia, ambao ulikuwa umeahirishwa kwa mara mbili awali, umeahirishwa tena kwa muda usiojulikana.
Mwenyekiti wa bodi ya uchaguzi nchini humo Omar Mohamed Abdulle ameambia wanahabari mjini Mogadishu kwamba haiwezekani kwa uchaguzi huo kufanyika Jumatano wiki hii kama ilivyokuwa imepangwa awali.
Sababu kuu ni kuchelewa kwa uchaguzi wa wabunge ambao wanafaa kukutana na kumchagua ras wa taifa hilo.
"Tarehe kamili haiku mbali. Wabunge watakapomaliza kuchaguliwa na wasajiliwe mnamo tarehe 6 au 7 Desemba, kila mmoja atafahamu tarehe kamili ya uchaguzi," alisema.
"Hautaki kugusia hilo kwa sasa. Hiyo itakuwa shughuli ya bunge na bunge ndilo litakaloamua ni wakati gani wa kumchagua spika wa bunge na rais. Lakini nawahakikishia jambo moja, kwamba uchaguzi huu usio wa moja kwa kwa moja unaitwa uchaguzi wa 2016, hii ina maana kwamba utafanyika 2016."

No comments:

Post a Comment