Friday 25 November 2016

Darassa adai muziki wake hauwezi kuchuja

Rapper Darassa amedai kuwa muziki anaofanya ni wa kuishi milele ndio maana nyimbo zake haziwezi kuchuja.
Akiongea na Times FM, Darassa amesema, “Natengeneza muziki wa kuishi milele, ndio maana ‘Utanipenda’ na ‘Too Much’ hazichuji.”
Kwa sasa Darassa ni mmoja kati ya rapper wa kizazi kipya ambao wanafanya vizuri huku wimbo wake aliouachia siku chache zilizopita ‘Muziki’ aliomshirikisha Ben Pol ukionekana kufanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya redio na runinga.

No comments:

Post a Comment