Wednesday 30 November 2016

Msajili: Haiwezekani watumishi wa umma kuiba fedha za kwenye akaunti maalum

  Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru amesema haiwezekani kwa watumishi wa umma kuiba fedha zinazowekwa kwenye fixed deposit accounts(akaunti maalum) kwa sababu miamala ya benki ni ya uwazi.
 Akizungumza leo jijini Dar es salaam, Mafuru alisema hizo ni tuhuma tu na Serikali imemwagiza CAG kuchunguza.
"Nimefanya kazi kazi kwenye taasisi za benki kwa miaka 20, sijawahi kuona watumishi wa umma wakichota hela kwenye fixed deposit account.
 Pale kwenye benki kuna miamala ya aina mbili tu, ya kuweka na kutoa. Usipoweka wazi wakati wa kuweka, siku utakapozitoa itaonyesha tu," alisema Mafuru.
 Alisema hakuna kosa kwa taasisi za serikali kuweka fedha kwenye akaunti hizo, lakini serikali sasa imeamua kuzihamishia BOT ili iwe rahisi kuzifuatilia.

No comments:

Post a Comment