Wednesday 30 November 2016

Mamia kupoteza ajira vituo mafuta

MAMIA ya watu walioajiriwa katika vituo mbalimbali vya kuuzia mafuta maarufu kama ‘petrol stations’ wako katika hatari ya kupoteza ajira zao , imefahamika.
Hali hiyo inatokana na kusuasua kwa mauzo ya bidhaa hiyo, huku chanzo kimojawapo kikitajwa kuwa ni matokeo ya hatua mbalimbali za Serikali ya awamu ya tano katika kubana matumizi.
Uchunguzi uliofanywa na Fofam-mediablog kwa siku kadhaa umebaini kuwa tishio hilo ni kubwa zaidi katika baadhi ya vituo baada ya wastani wa mauzo yake kwa siku kuporomoka katika siku za hivi karibuni hadi kwa kiwango cha takribani asilimia hamsini.
Aidha, uchunguzi huo umebaini kuwa hadi sasa, tayari baadhi ya kampuni zinazomiliki vituo vya bidhaa hiyo zimeanza kuchukua uamuzi mgumu wa kuviuza au kuvikodisha kwa watu wengine.

No comments:

Post a Comment