Wednesday 30 November 2016

TFF ya kanusha taarifa ambazo zilisambaa katika mitandao

Zimekuweko taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari na mitandao kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limeandaa shindano maalum mwezi Desemba.
Mwezi Desemba hakuna shindano lolote jipya litakalaondaliwa na TFF zaidi ya mashindano yake ya kawaida ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) na Azam Sports Federation Cup (ASFC).
Michuano mingine inayosimamiwa na TFF ni Ligi Kuu ya Taifa ya Wanawake (TWPL), Ligi Kuu ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 (TFFU20L), Ligi Daraja la Kwanza (FDL), Ligi Daraja la Pili (SDL) na Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL).
Ikumbukwe tu kwamba kwa sasa, timu za VPL ziko likizo na ni wakati wa Klabu kufanya mchakato wa usajili wa Dirisha Dogo. Duru la pili lenye mizunguko 15 inatarajiwa kuanza Desemba 17, 2016 kama ilivyopangwa hapo awali.

No comments:

Post a Comment