Tuesday, 15 November 2016

Brazil imeisambaratisha Peru jumla ya magoli 2-0

17759763_303
Na.Alex Mathias.
Licha ya kuwa ugenini timu ya Taifa ya Brazil imeisambaratisha Peru jumla ya magoli 2-0 mchezo wa kufuzu kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi uliochezwa katika uwanja wa Estadio Nacional uliopo mji wa Lima nchini Peru.
Timu ya Peru walionekana kuwabana vilivyo Brazil kwa style yao ya kushambulia na kujilinda na kufanya timu hizo ziende mapumziko zikiwa hazijafungana.
Kipindi cha pili kilianza kwa Brazil kujaruka na kushambulia kwa kasi na kwa lengo la kupata pointi tatu muhimu ambazo zitawarahishia kwenda Urusi mapema alikuwa mshambuliaji Jesus Gabriel dakika ya 58 alifunga goli la kwanza na Renato Augusto aliipatia goli la pili Brazil na kuonesha njia nyeupe ya kufuzu michuano hiyo.
Kwa matokeo hayo Brazil wamendelea kung’ang’ania kileleni mwa msimamao wakiwa na pointi 27 na kujiweka katika hatua nzuri ya kuwapeleka nchini Urusi mwaka 2018 wakati Peru wanaonekana kupoteza matumaini ya kufuzu kwani wapo katika nafasi ya nane wakiwa na pointi 14.
Brazil watakuwa ugenini Machi 24,2017 kucheza na Timu ya Uruguay ya Luis Suarez ambayo imepoteza mchezo wake dhidi ya Argentina ya Lionel Messi.

No comments:

Post a Comment